< Yeremia 44 >

1 Neno hili lilimjia Yeremia kuhusu Wayahudi wote waishio Misri, huko Migdoli, Tahpanhesi na Memfisi, katika nchi ya Pathrosi kusema:
La parole qui vint à Jérémie pour tous les Juifs qui habitaient dans le pays d’Égypte, qui habitaient à Migdol, et à Takhpanès, et à Noph, et dans le pays de Pathros, disant:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Mliona maangamizi makubwa niliyoyaleta juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda. Leo imeachwa ukiwa na magofu
Ainsi dit l’Éternel des armées, le Dieu d’Israël: Vous avez vu tout le mal que j’ai fait venir sur Jérusalem et sur toutes les villes de Juda; et voici, elles sont aujourd’hui un désert, et personne n’y habite,
3 kwa sababu ya uovu waliokuwa wameufanya. Walinikasirisha kwa kufukiza uvumba na kwa kuabudu miungu mingine ambayo kamwe wao, wala ninyi, wala baba zenu hawakuifahamu.
à cause de l’iniquité qu’ils ont commise pour me provoquer à colère, en allant brûler de l’encens pour servir d’autres dieux, qu’ils n’ont pas connus, eux, ni vous, ni vos pères.
4 Tena na tena, niliwatuma watumishi wangu manabii ambao walisema, ‘Msifanye jambo hili la kuchukiza ambalo nalichukia!’
Et je vous ai envoyé tous mes serviteurs les prophètes, me levant de bonne heure et [les] envoyant, disant: Ne faites point cette chose abominable que je hais.
5 Lakini hawakusikiliza wala hawakujali, hawakugeuka ili kuuacha uovu wao, wala hawakuacha kufukiza uvumba kwa miungu mingine.
Et ils n’ont pas écouté, et n’ont pas incliné leur oreille pour se détourner de leur iniquité, afin de ne pas brûler de l’encens à d’autres dieux;
6 Kwa hiyo hasira yangu kali ilimwagika, ikawaka dhidi ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, na kuifanya ukiwa na magofu kama ilivyo leo.
alors ma fureur et ma colère ont été versées [sur eux], et ont brûlé dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem; et elles sont devenues un désert, une désolation, comme [il paraît] aujourd’hui.
7 “Basi hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kwa nini kujiletea maafa makubwa kama haya juu yenu kwa kujikatilia mbali kutoka Yuda wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, hata kujiacha bila mabaki?
Et maintenant, ainsi dit l’Éternel, le Dieu des armées, le Dieu d’Israël: Pourquoi faites-vous un grand mal contre vos âmes, pour vous faire retrancher du milieu de Juda, homme et femme, enfant et celui qui tète, en sorte qu’il ne vous demeure aucun reste;
8 Kwa nini kuichochea hasira yangu kwa kile ambacho mikono yenu imekitengeneza, mkaifukizia uvumba miungu mingine huko Misri, mahali mlipokuja kuishi? Mtajiangamiza wenyewe na kujifanya kitu cha kulaania na shutumu miongoni mwa mataifa yote duniani.
en me provoquant par les œuvres de vos mains, en brûlant de l’encens à d’autres dieux dans le pays d’Égypte où vous êtes venus pour y séjourner, en sorte que vous soyez retranchés, et que vous deveniez une malédiction et un opprobre parmi toutes les nations de la terre?
9 Je, mmesahau uovu uliotendwa na baba zenu, na wafalme na malkia wa Yuda, na uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na barabara za Yerusalemu?
Avez-vous oublié les iniquités de vos pères, et les iniquités des rois de Juda, et les iniquités de leurs femmes, et vos iniquités, et les iniquités de vos femmes, commises dans le pays de Juda et dans les rues de Jérusalem?
10 Mpaka leo hawajajinyenyekeza au kuonyesha heshima, wala hawajafuata sheria yangu na amri nilizoweka mbele yenu na baba zenu.
Ils ne se sont pas humiliés jusqu’à ce jour, et ils n’ont pas eu de crainte, et ils n’ont pas marché dans ma loi et dans mes statuts, que j’ai mis devant vous et devant vos pères.
11 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Mimi nimekusudia kuleta maafa juu yenu, na kuiangamiza Yuda yote.
C’est pourquoi, ainsi dit l’Éternel des armées, le Dieu d’Israël: Voici, je mets ma face contre vous pour le mal, et pour retrancher tout Juda!
12 Nitawaondoa mabaki ya Yuda waliokusudia kwenda Misri kukaa humo. Wote wataangamia huko Misri, wataanguka kwa upanga au kufa kwa njaa. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana, watakufa kwa upanga au njaa. Watakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha laumu na shutumu.
Et je prendrai le reste de Juda qui a tourné sa face pour aller dans le pays d’Égypte pour y séjourner; et ils seront tous consumés; ils tomberont dans le pays d’Égypte; ils seront consumés par l’épée [et] par la famine, depuis le petit jusqu’au grand; ils mourront par l’épée et par la famine, et ils seront une exécration, une désolation, et une malédiction, et un opprobre.
13 Nitawaadhibu wale waishio Misri kwa upanga, njaa na tauni kama nilivyoiadhibu Yerusalemu.
Et je punirai ceux qui habitent dans le pays d’Égypte, comme j’ai puni Jérusalem par l’épée, par la famine, et par la peste;
14 Hakuna hata mmoja wa mabaki ya Yuda ambaye amekwenda kuishi Misri atakayeepuka au kunusurika ili kurudi katika nchi ya Yuda, ambayo wanaitamani sana kurudi na kuishi ndani yake, hakuna hata mmoja atakayerudi isipokuwa wakimbizi wachache.”
et, du reste de Juda qui est venu dans le pays d’Égypte pour y séjourner, il n’y aura ni réchappé ni résidu pour retourner dans le pays de Juda, où ils avaient le désir de retourner pour y habiter; car ils ne retourneront pas, sauf [quelques] réchappés.
15 Kisha wanaume wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakifukiza uvumba kwa miungu mingine, pamoja na wanawake wote waliokuwako, yaani, kusanyiko kubwa na watu wote walioishi nchi ya Misri na Pathrosi, wakamwambia Yeremia,
Et tous les hommes qui savaient que leurs femmes brûlaient de l’encens à d’autres dieux, et toutes les femmes qui se tenaient là, un grand rassemblement, et tout le peuple qui demeurait dans le pays d’Égypte, à Pathros, répondirent à Jérémie, disant:
16 “Hatutausikiliza ujumbe uliotuambia katika jina la Bwana!
Quant à la parole que tu nous as dite au nom de l’Éternel, nous ne t’écouterons pas;
17 Hakika tutafanya kila kitu tulichosema tutakifanya: Tutafukiza uvumba kwa Malkia wa Mbinguni na tutammiminia sadaka zetu za kinywaji kama vile sisi na baba zetu, wafalme wetu na maafisa wetu tulivyofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Wakati ule tulikuwa na chakula tele, tulikuwa matajiri wala hatukupata dhara lolote.
mais nous ferons certainement toute parole qui est sortie de notre bouche, en brûlant de l’encens à la reine des cieux, et en lui faisant des libations, comme nous avons fait, nous et nos pères, nos rois et nos princes, dans les villes de Juda, et dans les rues de Jérusalem; et nous étions rassasiés de pain, et nous étions à notre aise, et nous ne voyions pas de malheur.
18 Lakini tangu tulipoacha kumfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka za kinywaji, hatupati chochote, na tumekuwa tukiangamizwa kwa upanga na njaa.”
Mais depuis que nous avons cessé de brûler de l’encens à la reine des cieux et de lui faire des libations, nous manquons de tout, et nous sommes consumés par l’épée et par la famine.
19 Wanawake wakaongeza kusema, “Wakati tulipomfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka zetu za kinywaji, je, waume zetu hawakujua kwamba tulikuwa tukitengeneza maandazi kwa mfano wake, na kummiminia yeye sadaka za kinywaji?”
Et si nous avons brûlé de l’encens à la reine des cieux, et si nous lui avons fait des libations, est-ce sans nos maris que nous lui avons fait des gâteaux à son image, ou que nous lui avons fait des libations?
20 Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake waliokuwa wakimjibu,
Et Jérémie parla à tout le peuple, aux hommes et aux femmes, et à tout le peuple qui lui avait répondu [cette] parole, disant:
21 “Je, Bwana hakukumbuka na kufikiri juu ya uvumba uliofukizwa katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu na ninyi pamoja na baba zenu, wafalme wenu, maafisa wenu na watu wa nchi?
Ne sont-ce pas ces encensements que vous avez faits dans les villes de Juda et dans les rues de Jérusalem, vous et vos pères, vos rois et vos princes et le peuple du pays, que l’Éternel s’est rappelés, et qui lui sont montés au cœur?
22 Bwana alipokuwa hawezi kuendelea kuvumilia matendo yenu maovu na mambo ya machukizo mliyoyafanya, nchi yenu ilikuwa kitu cha kulaania na kuachwa ukiwa pasipo wakazi, kama ilivyo leo.
Et l’Éternel ne put plus le supporter, à cause de l’iniquité de vos actions, [et] à cause des choses abominables que vous avez faites, et votre pays est devenu un désert, et une désolation, et une malédiction, de sorte qu’il n’y a pas d’habitant, comme [il paraît] aujourd’hui.
23 Kwa sababu mmefukiza uvumba na kufanya dhambi dhidi ya Bwana, nanyi hamkumtii wala kufuata sheria yake au amri zake au maagizo yake, maafa haya yamekuja juu yenu, kama mnavyoona sasa.”
Parce que vous avez brûlé de l’encens, et que vous avez péché contre l’Éternel, et que vous n’avez pas écouté la voix de l’Éternel, et n’avez point marché dans sa loi, ni dans ses statuts, ni dans ses témoignages, à cause de cela ce mal vous est arrivé, comme [il paraît ] aujourd’hui.
24 Kisha Yeremia akawaambia watu wote, pamoja na wanawake, “Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mlioko Misri.
Et Jérémie dit à tout le peuple et à toutes les femmes: Écoutez la parole de l’Éternel, vous, tout Juda, qui êtes dans le pays d’Égypte:
25 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Ninyi na wake zenu mmeonyesha kwa matendo yenu kile mlichoahidi mliposema, ‘Hakika tutatimiza nadhiri tulizoziweka za kumfukizia uvumba na kummiminia sadaka za kinywaji Malkia wa Mbinguni.’ “Endeleeni basi, fanyeni yale mliyoahidi! Timizeni nadhiri zenu!
Ainsi parle l’Éternel des armées, le Dieu d’Israël, disant: Vous et vos femmes, vous avez parlé de votre bouche, et vous avez accompli de vos mains, disant: Certainement nous accomplirons nos vœux que nous avons voués, pour brûler de l’encens à la reine des cieux et lui faire des libations. Vous ferez certainement selon vos vœux, et vous accomplirez certainement vos vœux.
26 Lakini sikieni neno la Bwana, enyi Wayahudi wote mnaoishi Misri: ‘Ninaapa kwa Jina langu lililo kuu,’ asema Bwana, ‘kwamba hakuna hata mmoja atokaye Yuda anayeishi popote Misri ambaye kamwe ataomba tena kwa Jina langu au kuapa, akisema, “Hakika kama Bwana Mwenyezi aishivyo.”
C’est pourquoi, écoutez la parole de l’Éternel, vous, tout Juda, qui habitez dans le pays d’Égypte: Voici, j’ai juré par mon grand nom, dit l’Éternel, que mon nom ne sera plus réclamé par la bouche d’aucun homme de Juda, dans tout le pays d’Égypte, disant: Le Seigneur, l’Éternel, est vivant!
27 Kwa maana ninawaangalia kwa ajili ya madhara, wala sio kwa mema. Wayahudi walioko Misri wataangamia kwa upanga na njaa, hadi wote watakapoangamizwa.
Voici, je veille sur eux pour le mal, et non pour le bien; et ils seront consumés, chaque homme de Juda qui est dans le pays d’Égypte, par l’épée et par la famine, jusqu’à ce qu’il n’y en ait plus.
28 Wale watakaonusurika upanga na kurudi katika nchi ya Yuda kutoka Misri watakuwa wachache sana. Ndipo mabaki wote wa Yuda waliokuja kuishi Misri watakapojua ni neno la nani litakalosimama, kwamba ni langu au lao.
Et ceux qui échapperont à l’épée retourneront du pays d’Égypte dans le pays de Juda, un fort petit nombre; et ils sauront, tout ce reste de Juda, ceux qui sont venus dans le pays d’Égypte pour y séjourner, de qui, de moi ou d’eux, la parole s’accomplira.
29 “‘Hii itakuwa ndiyo ishara kwenu kwamba nitawaadhibu mahali hapa, asema Bwana, ili mpate kujua kuwa onyo langu la madhara dhidi yenu hakika litatimizwa.’
Et ceci sera pour vous le signe, dit l’Éternel, que je vous punirai dans ce lieu, afin que vous sachiez que mes paroles s’effectueront certainement contre vous en mal.
30 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitamtia Farao Hofra mfalme wa Misri mikononi mwa adui zake wanaoutafuta uhai wake, kama vile nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, adui aliyekuwa akiutafuta uhai wake.’”
Ainsi dit l’Éternel: Voici, je livre le Pharaon Hophra, roi d’Égypte, en la main de ses ennemis et en la main de ceux qui cherchent sa vie, comme j’ai livré Sédécias, roi de Juda, en la main de Nebucadretsar, roi de Babylone, son ennemi, celui qui cherchait sa vie.

< Yeremia 44 >