< Yeremia 44 >

1 Neno hili lilimjia Yeremia kuhusu Wayahudi wote waishio Misri, huko Migdoli, Tahpanhesi na Memfisi, katika nchi ya Pathrosi kusema:
The word that came through Jeremiah to all the Jews who were living in the land of Egypt, living at Migdol, and at Tahpanhes, and at Memphis, and in the land of Pathros, saying:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Mliona maangamizi makubwa niliyoyaleta juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda. Leo imeachwa ukiwa na magofu
“Thus says the Lord of hosts, the God of Israel: You yourselves have seen all this evil that I have led over Jerusalem and over all the cities of Judah. And behold, they are desolate to this day, and there is no inhabitant in them,
3 kwa sababu ya uovu waliokuwa wameufanya. Walinikasirisha kwa kufukiza uvumba na kwa kuabudu miungu mingine ambayo kamwe wao, wala ninyi, wala baba zenu hawakuifahamu.
because of the wickedness which they have done, so that they provoked me to wrath, and because they went to offer sacrifice and worship to strange gods, which neither they, nor you, nor your fathers knew.
4 Tena na tena, niliwatuma watumishi wangu manabii ambao walisema, ‘Msifanye jambo hili la kuchukiza ambalo nalichukia!’
And I sent to you all my servants, the prophets, rising in the night, and sending, and saying: ‘Do not choose to do this abominable word, which I hate.’
5 Lakini hawakusikiliza wala hawakujali, hawakugeuka ili kuuacha uovu wao, wala hawakuacha kufukiza uvumba kwa miungu mingine.
But they did not listen, nor did they incline their ear, so that they would convert from their evil, and so that they would not sacrifice to strange gods.
6 Kwa hiyo hasira yangu kali ilimwagika, ikawaka dhidi ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, na kuifanya ukiwa na magofu kama ilivyo leo.
And so my indignation and my fury was fanned and kindled in the cities of Judah and in the streets of Jerusalem. And they have been turned into desolation and devastation, just as it is this day.
7 “Basi hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kwa nini kujiletea maafa makubwa kama haya juu yenu kwa kujikatilia mbali kutoka Yuda wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, hata kujiacha bila mabaki?
And now, thus says the Lord of hosts, the God of Israel: Why do you commit this great evil against your own souls, so that, among you, man and woman, child and infant would pass away from the midst of Judah, and so that no remnant at all would be left behind of you?
8 Kwa nini kuichochea hasira yangu kwa kile ambacho mikono yenu imekitengeneza, mkaifukizia uvumba miungu mingine huko Misri, mahali mlipokuja kuishi? Mtajiangamiza wenyewe na kujifanya kitu cha kulaania na shutumu miongoni mwa mataifa yote duniani.
For you have provoked me by the works of your hands, by sacrificing to strange gods in the land of Egypt, into which you have entered in order to live there, and so that you would perish and become a curse and a disgrace before all the nations of the earth.
9 Je, mmesahau uovu uliotendwa na baba zenu, na wafalme na malkia wa Yuda, na uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na barabara za Yerusalemu?
How could you have forgotten the evils of your fathers, and the evils of the kings of Judah, and the evils of their wives, and your own evils, and the evils of your own wives, which they have done in the land of Judah and in the regions of Jerusalem?
10 Mpaka leo hawajajinyenyekeza au kuonyesha heshima, wala hawajafuata sheria yangu na amri nilizoweka mbele yenu na baba zenu.
They have not been cleansed, even to this day. And they have not feared, and they have not walked in the law of the Lord and in my precepts, which I have given before you and before your fathers.
11 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Mimi nimekusudia kuleta maafa juu yenu, na kuiangamiza Yuda yote.
For this reason, thus says the Lord of hosts, the God of Israel: Behold, I will set my face upon you for evil. And I will disperse all of Judah.
12 Nitawaondoa mabaki ya Yuda waliokusudia kwenda Misri kukaa humo. Wote wataangamia huko Misri, wataanguka kwa upanga au kufa kwa njaa. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana, watakufa kwa upanga au njaa. Watakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha laumu na shutumu.
And I will take the remnant of Judah, who had set their faces so that they would enter into the land of Egypt and live there, and they will all be consumed in the land of Egypt. They will fall by the sword and by famine. And they will be consumed, from the least, even to the greatest. By sword and by famine shall they die. And they will be an oath, and a wonder, and a curse, and a disgrace.
13 Nitawaadhibu wale waishio Misri kwa upanga, njaa na tauni kama nilivyoiadhibu Yerusalemu.
And I will visit against those who are living in the land of Egypt, just as I have visited against Jerusalem: with the sword, and with famine, and with pestilence.
14 Hakuna hata mmoja wa mabaki ya Yuda ambaye amekwenda kuishi Misri atakayeepuka au kunusurika ili kurudi katika nchi ya Yuda, ambayo wanaitamani sana kurudi na kuishi ndani yake, hakuna hata mmoja atakayerudi isipokuwa wakimbizi wachache.”
And there will be no one who escapes, of those who remain among the remnant of the Jews, those who have gone to sojourn in the land of Egypt. And they wish to be returned to the land of Judah, for they lift up their souls so that they might return and live there. But there will be no one who may return, except those who will flee.”
15 Kisha wanaume wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakifukiza uvumba kwa miungu mingine, pamoja na wanawake wote waliokuwako, yaani, kusanyiko kubwa na watu wote walioishi nchi ya Misri na Pathrosi, wakamwambia Yeremia,
Then all the men, knowing that their wives were sacrificing to strange gods, and all of the women, a great multitude of whom were standing there, and all of the people who were living in the land of Egypt at Pathros, responded to Jeremiah, by saying:
16 “Hatutausikiliza ujumbe uliotuambia katika jina la Bwana!
“Concerning the word that you have spoken to us in the name of the Lord, we will not heed you.
17 Hakika tutafanya kila kitu tulichosema tutakifanya: Tutafukiza uvumba kwa Malkia wa Mbinguni na tutammiminia sadaka zetu za kinywaji kama vile sisi na baba zetu, wafalme wetu na maafisa wetu tulivyofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Wakati ule tulikuwa na chakula tele, tulikuwa matajiri wala hatukupata dhara lolote.
But we will continue to do every word which proceeds from our own mouth, so that we sacrifice to the queen of heaven, and we pour out libations to her, just as we and our fathers have done, our kings and our leaders, in the cities of Judah and in the streets of Jerusalem. For we were filled with bread, and it was well with us, and we saw no evil.
18 Lakini tangu tulipoacha kumfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka za kinywaji, hatupati chochote, na tumekuwa tukiangamizwa kwa upanga na njaa.”
But since the time that we ceased to offer sacrifice to the queen of heaven, and to pour out libations to her, we have been in need of all things, and we have been consumed by the sword and by famine.
19 Wanawake wakaongeza kusema, “Wakati tulipomfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka zetu za kinywaji, je, waume zetu hawakujua kwamba tulikuwa tukitengeneza maandazi kwa mfano wake, na kummiminia yeye sadaka za kinywaji?”
But when we offer sacrifice to the queen of heaven and pour out libations to her, do we make cakes for her worship and offer libations to her without our husbands?”
20 Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake waliokuwa wakimjibu,
And Jeremiah spoke to all the people, facing the men, and facing the women, and facing all the people who had responded this word to him, saying:
21 “Je, Bwana hakukumbuka na kufikiri juu ya uvumba uliofukizwa katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu na ninyi pamoja na baba zenu, wafalme wenu, maafisa wenu na watu wa nchi?
“Was this not the sacrifice that you offered in the cities of Judah and in the streets of Jerusalem, you and your fathers, your kings and your leaders, and the people of the land, which has been called to mind by the Lord and which has entered into his heart?
22 Bwana alipokuwa hawezi kuendelea kuvumilia matendo yenu maovu na mambo ya machukizo mliyoyafanya, nchi yenu ilikuwa kitu cha kulaania na kuachwa ukiwa pasipo wakazi, kama ilivyo leo.
And the Lord could no longer bear this, because of the evil of your intentions, and because of the abominations that you have done. And so, your land has become a desolation, and an astonishment, and a curse, and it is without an inhabitant, even to this day.
23 Kwa sababu mmefukiza uvumba na kufanya dhambi dhidi ya Bwana, nanyi hamkumtii wala kufuata sheria yake au amri zake au maagizo yake, maafa haya yamekuja juu yenu, kama mnavyoona sasa.”
This is because you have sacrificed to idols, and you have sinned against the Lord. And you have not heeded the voice of the Lord, and you have not walked in his law, and in his precepts, and in his testimonies. It is for this reason that these evils have happened to you, just as it is today.”
24 Kisha Yeremia akawaambia watu wote, pamoja na wanawake, “Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mlioko Misri.
Then Jeremiah said to all the people and to all the women: “Listen to the word of the Lord, all you of Judah who are in the land of Egypt:
25 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Ninyi na wake zenu mmeonyesha kwa matendo yenu kile mlichoahidi mliposema, ‘Hakika tutatimiza nadhiri tulizoziweka za kumfukizia uvumba na kummiminia sadaka za kinywaji Malkia wa Mbinguni.’ “Endeleeni basi, fanyeni yale mliyoahidi! Timizeni nadhiri zenu!
Thus says the Lord of hosts, the God of Israel, saying: You and your wives have spoken it with your mouth, and have fulfilled it with your hands, saying: ‘Let us perform our vows that we have made, so that we may offer sacrifice to the queen of heaven, and pour out libations to her.’ You have fulfilled your vows and accomplished their works.
26 Lakini sikieni neno la Bwana, enyi Wayahudi wote mnaoishi Misri: ‘Ninaapa kwa Jina langu lililo kuu,’ asema Bwana, ‘kwamba hakuna hata mmoja atokaye Yuda anayeishi popote Misri ambaye kamwe ataomba tena kwa Jina langu au kuapa, akisema, “Hakika kama Bwana Mwenyezi aishivyo.”
Because of this, listen to the word of the Lord, all you of Judah, who live in the land of Egypt: Behold, I have sworn by my great name, says the Lord, that my name will never again be invoked by the mouth of any man of Judah in the land of Egypt, saying: ‘As the Lord God lives.’
27 Kwa maana ninawaangalia kwa ajili ya madhara, wala sio kwa mema. Wayahudi walioko Misri wataangamia kwa upanga na njaa, hadi wote watakapoangamizwa.
Behold, I will be vigilant over them for harm, and not for good. And all the men of Judah who are in the land of Egypt will be consumed, by the sword and by famine, until they are thoroughly consumed.
28 Wale watakaonusurika upanga na kurudi katika nchi ya Yuda kutoka Misri watakuwa wachache sana. Ndipo mabaki wote wa Yuda waliokuja kuishi Misri watakapojua ni neno la nani litakalosimama, kwamba ni langu au lao.
And a few men, who will flee from the sword, will return from the land of Egypt into the land of Judah. And all the remnant of Judah, who had entered into the land of Egypt so as to live there, will know whose word will be completed, mine or theirs.
29 “‘Hii itakuwa ndiyo ishara kwenu kwamba nitawaadhibu mahali hapa, asema Bwana, ili mpate kujua kuwa onyo langu la madhara dhidi yenu hakika litatimizwa.’
And this will be a sign to you, says the Lord, that I will visit against you in this place, so that truly you may know that my words will be completed against you for harm.”
30 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitamtia Farao Hofra mfalme wa Misri mikononi mwa adui zake wanaoutafuta uhai wake, kama vile nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, adui aliyekuwa akiutafuta uhai wake.’”
Thus says the Lord: “Behold, I will deliver Pharaoh Hophra, the king of Egypt, into the hand of his enemies, and into the hand of those who are seeking his life, just as I delivered Zedekiah, the king of Judah, into the hand of Nebuchadnezzar, the king of Babylon, his enemy and the one who was seeking his life.”

< Yeremia 44 >