< Yeremia 44 >
1 Neno hili lilimjia Yeremia kuhusu Wayahudi wote waishio Misri, huko Migdoli, Tahpanhesi na Memfisi, katika nchi ya Pathrosi kusema:
Riječ koja se javi Jeremiji za sve Judejce što življahu u zemlji egipatskoj, što življahu u Migdolu, u Tafnisu, u Memfisu i u zemlji Patrosu.
2 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Mliona maangamizi makubwa niliyoyaleta juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda. Leo imeachwa ukiwa na magofu
Ovako govori Jahve nad Vojskama, Bog Izraelov: “I sami vidjeste svu nesreću koju sam svalio na Jeruzalem i na sve gradove judejske: evo danas su to gomile ruševina, a u njima nitko više ne živi,
3 kwa sababu ya uovu waliokuwa wameufanya. Walinikasirisha kwa kufukiza uvumba na kwa kuabudu miungu mingine ambayo kamwe wao, wala ninyi, wala baba zenu hawakuifahamu.
zbog nedjela njihovih što ih učiniše da bi mene vrijeđali, polazeći drugim bogovima kojih nisu poznavali ni oni, ni vi, ni oci vaši, da im kade i da im služe.
4 Tena na tena, niliwatuma watumishi wangu manabii ambao walisema, ‘Msifanye jambo hili la kuchukiza ambalo nalichukia!’
A ja sam vam jednako slao svoje sluge proroke da vam kažu: 'Ne činite tih gnusoba koje su mi ogavne!'
5 Lakini hawakusikiliza wala hawakujali, hawakugeuka ili kuuacha uovu wao, wala hawakuacha kufukiza uvumba kwa miungu mingine.
Ali me oni nisu slušali, niti su uho svoje priklonili da se okane zloće svoje i prestanu kaditi tuđim bogovima.
6 Kwa hiyo hasira yangu kali ilimwagika, ikawaka dhidi ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, na kuifanya ukiwa na magofu kama ilivyo leo.
Zato se izli gnjev moj i srdžba moja i rasplamtje se u gradovima judejskim i po ulicama jeruzalemskim, te se pretvoriše u pustoš i razvaline, kao što su danas.
7 “Basi hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kwa nini kujiletea maafa makubwa kama haya juu yenu kwa kujikatilia mbali kutoka Yuda wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, hata kujiacha bila mabaki?
Zašto sami svaljujete na se tako golemu nesreću” - govori Jahve, Bog nad Vojskama, Bog Izraelov - “te sami do korijena istrebljujete iz Judeje sve muško i žensko, djecu i dojenčad, te vam ni ostatka ostati neće,
8 Kwa nini kuichochea hasira yangu kwa kile ambacho mikono yenu imekitengeneza, mkaifukizia uvumba miungu mingine huko Misri, mahali mlipokuja kuishi? Mtajiangamiza wenyewe na kujifanya kitu cha kulaania na shutumu miongoni mwa mataifa yote duniani.
jer me vrijeđate djelima ruku svojih, kadeći tuđim bogovima u zemlji egipatskoj, u koju ste došli prebivati, a bit ćete iskorijenjeni i postat ćete kletva i ruglo među svim narodima na zemlji?
9 Je, mmesahau uovu uliotendwa na baba zenu, na wafalme na malkia wa Yuda, na uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na barabara za Yerusalemu?
Jeste li zaboravili bezakonja otaca svojih, bezakonja kraljeva judejskih, bezakonja knezova svojih i žena njihovih i bezakonja svoja, bezakonja žena svojih, počinjena u zemlji judejskoj i po ulicama jeruzalemskim?
10 Mpaka leo hawajajinyenyekeza au kuonyesha heshima, wala hawajafuata sheria yangu na amri nilizoweka mbele yenu na baba zenu.
Do dana današnjega nisu se pokajali, nisu se bojali, nisu živjeli po Zakonu mojemu ni po odredbama mojim, koje dadoh vama i ocima vašim.”
11 “Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Mimi nimekusudia kuleta maafa juu yenu, na kuiangamiza Yuda yote.
Zato ovako govori Jahve nad Vojskama, Bog Izraelov: “Evo, okrećem svoje lice vama, na nesreću vašu, da zatrem svu zemlju judejsku.
12 Nitawaondoa mabaki ya Yuda waliokusudia kwenda Misri kukaa humo. Wote wataangamia huko Misri, wataanguka kwa upanga au kufa kwa njaa. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana, watakufa kwa upanga au njaa. Watakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha laumu na shutumu.
Odnijet ću ostatak Judeje koji je odlučio da ide u zemlju egipatsku da se ondje stani; svi će izginuti u zemlji egipatskoj, past će od mača, od gladi će pogibati, poginut će svi, malo i veliko, pomrijet će od mača i gladi, i bit će prokletstvo, užas, kletva i poruga.
13 Nitawaadhibu wale waishio Misri kwa upanga, njaa na tauni kama nilivyoiadhibu Yerusalemu.
Kaznit ću sve koji budu u zemlji egipatskoj, kao što sam kaznio Jeruzalem: mačem, glađu i kugom.
14 Hakuna hata mmoja wa mabaki ya Yuda ambaye amekwenda kuishi Misri atakayeepuka au kunusurika ili kurudi katika nchi ya Yuda, ambayo wanaitamani sana kurudi na kuishi ndani yake, hakuna hata mmoja atakayerudi isipokuwa wakimbizi wachache.”
A od ostatka Judeje koji je došao da se stani u Egiptu, nitko neće uteći ni preživjeti da bi se mogao vratiti u zemlju judejsku za kojom im duše čeznu, da se u nju vrate i ondje nastane. Jer se nitko neće vratiti, osim izbjeglica.”
15 Kisha wanaume wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakifukiza uvumba kwa miungu mingine, pamoja na wanawake wote waliokuwako, yaani, kusanyiko kubwa na watu wote walioishi nchi ya Misri na Pathrosi, wakamwambia Yeremia,
I tada svi muškarci koji su znali da im žene kade tuđim bogovima, i sve nazočne žene, u velikom mnoštvu, i sav narod što življaše u zemlji egipatskoj i u Patrosu odgovoriše Jeremiji:
16 “Hatutausikiliza ujumbe uliotuambia katika jina la Bwana!
“Riječi koje si u ime Jahvino nama objavio mi ne slušamo;
17 Hakika tutafanya kila kitu tulichosema tutakifanya: Tutafukiza uvumba kwa Malkia wa Mbinguni na tutammiminia sadaka zetu za kinywaji kama vile sisi na baba zetu, wafalme wetu na maafisa wetu tulivyofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Wakati ule tulikuwa na chakula tele, tulikuwa matajiri wala hatukupata dhara lolote.
naprotiv, i dalje ćemo se držati zadane riječi: kadit ćemo nebeskoj kraljici i lijevati ljevanice, kao što smo i mi i oci naši, naši kraljevi i knezovi činili u gradovima judejskim i po ulicama jeruzalemskim: tada imadosmo kruha izobila, bijasmo sretni i ne trpjesmo nikakvih nesreća.
18 Lakini tangu tulipoacha kumfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka za kinywaji, hatupati chochote, na tumekuwa tukiangamizwa kwa upanga na njaa.”
Ali otkako prestadosmo kaditi nebeskoj kraljici i lijevati joj ljevanice, u svemu smo oskudijevali i od mača i gladi pogibali.”
19 Wanawake wakaongeza kusema, “Wakati tulipomfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka zetu za kinywaji, je, waume zetu hawakujua kwamba tulikuwa tukitengeneza maandazi kwa mfano wake, na kummiminia yeye sadaka za kinywaji?”
A žene rekoše: “Kad kadimo kraljici nebeskoj i lijevamo joj ljevanice, zar joj bez znanja svojih muževa pečemo kolače u obliku lika njezina i lijevamo ljevanice?”
20 Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake waliokuwa wakimjibu,
Tada Jeremija svemu narodu, muškarcima i ženama, i svim ljudima koji su mu tako govorili reče:
21 “Je, Bwana hakukumbuka na kufikiri juu ya uvumba uliofukizwa katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu na ninyi pamoja na baba zenu, wafalme wenu, maafisa wenu na watu wa nchi?
“Nije li se Jahve spomenuo i nije li ga u srce dirnuo tamjan što ste ga palili po ulicama jeruzalemskim, vi i oci vaši, vaši kraljevi, knezovi i puk zemaljski?
22 Bwana alipokuwa hawezi kuendelea kuvumilia matendo yenu maovu na mambo ya machukizo mliyoyafanya, nchi yenu ilikuwa kitu cha kulaania na kuachwa ukiwa pasipo wakazi, kama ilivyo leo.
Jahve više nije mogao podnositi zlodjela vaših i gnusoba koje počiniste, i zato se zemlja vaša pretvorila u pustoš i ruševine, u prokletstvo, bez stanovnika, kao što je i danas.
23 Kwa sababu mmefukiza uvumba na kufanya dhambi dhidi ya Bwana, nanyi hamkumtii wala kufuata sheria yake au amri zake au maagizo yake, maafa haya yamekuja juu yenu, kama mnavyoona sasa.”
Zbog toga što ste, prinoseći tamjan, zgriješili Jahvi, što Jahvina glasa ne slušaste i Jahvina se Zakona i njegovih se naredaba i svjedočanstava ne držaste, snađe vas ova nevolja, kakva je danas.”
24 Kisha Yeremia akawaambia watu wote, pamoja na wanawake, “Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mlioko Misri.
Zatim reče Jeremija svemu narodu, osobito ženama: “Čujte riječ Jahvinu, svi Judejci koji ste u zemlji egipatskoj:
25 Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Ninyi na wake zenu mmeonyesha kwa matendo yenu kile mlichoahidi mliposema, ‘Hakika tutatimiza nadhiri tulizoziweka za kumfukizia uvumba na kummiminia sadaka za kinywaji Malkia wa Mbinguni.’ “Endeleeni basi, fanyeni yale mliyoahidi! Timizeni nadhiri zenu!
Ovako govori Jahve nad Vojskama, Bog Izraelov: 'Vi žene, ono što vaša usta obećaju, to vaše ruke moraju i izvršiti. Rekoste: 'Mi ćemo se tvrdo držati zavjeta što ih učinismo: kaditi kraljici nebeskoj i lijevati joj ljevanice.' Držite se samo svojih zavjeta i lijevajte revno ljevanice!
26 Lakini sikieni neno la Bwana, enyi Wayahudi wote mnaoishi Misri: ‘Ninaapa kwa Jina langu lililo kuu,’ asema Bwana, ‘kwamba hakuna hata mmoja atokaye Yuda anayeishi popote Misri ambaye kamwe ataomba tena kwa Jina langu au kuapa, akisema, “Hakika kama Bwana Mwenyezi aishivyo.”
Ali čujte zato riječ Jahvinu, svi vi Judejci nastanjeni u zemlji egipatskoj! Evo, zaklinjem se velikim imenom svojim,' govori Jahve. 'U svoj zemlji egipatskoj nijedna usta judejska neće više izustiti mojega imena; nitko neće reći: 'Živoga mi Jahve!'
27 Kwa maana ninawaangalia kwa ajili ya madhara, wala sio kwa mema. Wayahudi walioko Misri wataangamia kwa upanga na njaa, hadi wote watakapoangamizwa.
Evo, bdim nad njima, na nesreću, a ne na dobro njihovo: svi ljudi judejski što su u zemlji egipatskoj poginut će od mača i gladi do potpunog istrebljenja.
28 Wale watakaonusurika upanga na kurudi katika nchi ya Yuda kutoka Misri watakuwa wachache sana. Ndipo mabaki wote wa Yuda waliokuja kuishi Misri watakapojua ni neno la nani litakalosimama, kwamba ni langu au lao.
I bit će malo onih koji će izbjeći maču i vratiti se iz egipatske zemlje u zemlju judejsku. Onda će sav ostatak judejski, svi koji dođoše u zemlju egipatsku da ondje žive, spoznati čija riječ vrijedi, moja ili njihova.
29 “‘Hii itakuwa ndiyo ishara kwenu kwamba nitawaadhibu mahali hapa, asema Bwana, ili mpate kujua kuwa onyo langu la madhara dhidi yenu hakika litatimizwa.’
A ovo neka vam bude znamenje - riječ je Jahvina - da ću vas kazniti na ovome mjestu, da biste znali da će se vama na nesreću ispuniti prijetnje moje protiv vas.'
30 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitamtia Farao Hofra mfalme wa Misri mikononi mwa adui zake wanaoutafuta uhai wake, kama vile nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, adui aliyekuwa akiutafuta uhai wake.’”
Ovako govori Jahve: 'Gle, predat ću faraona Hofru, kralja egipatskoga, u ruke njegovim neprijateljima i u ruke onih koji mu rade o glavi, baš kao što sam Sidkiju, kralja Judejskoga, predao u ruke Nabukodonozora, kralja babilonskoga, neprijatelja njegova, koji mu je radio o glavi.'”