< Yeremia 43 >

1 Yeremia alipomaliza kuwaambia watu maneno yote ya Bwana Mungu wao, yaani kila kitu Bwana alichokuwa amemtuma kuwaambia,
And it was when had finished Jeremiah to speak to all the people all [the] words of Yahweh God their which he had sent him Yahweh God their to them all the words these.
2 Azaria mwana wa Hoshaya, na Yohanani mwana wa Karea, na watu wote wenye kiburi wakamwambia Yeremia, “Wewe unasema uongo! Bwana Mungu wetu hajakutuma kusema, ‘Kamwe msiende Misri kukaa huko.’
And he said Azariah [the] son of Hoshaiah and Johanan [the] son of Kareah and all the people arrogant saying to Jeremiah falsehood you [are] speaking not he has sent you Yahweh God our saying not you must go Egypt to sojourn there.
3 Lakini Baruku mwana wa Neria anakuchochea dhidi yetu ili ututie mikononi mwa Wakaldayo, ili watuue au watuchukue uhamishoni Babeli.”
For Baruch [the] son of Neriah [is] inciting you against us so as to give us in [the] hand of the Chaldeans to put to death us and to take into exile us Babylon.
4 Basi Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi, na watu wote wakakataa kutii amri ya Bwana ya kukaa katika nchi ya Yuda.
And not he listened Johanan [the] son of Kareah and all [the] commanders of the armies and all the people to [the] voice of Yahweh to remain in [the] land of Judah.
5 Badala yake, Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi wakawaongoza mabaki yote ya Yuda waliokuwa wamerudi kuishi katika nchi ya Yuda kutoka mataifa yote ambayo walikuwa wametawanywa.
And he took Johanan [the] son of Kareah and all [the] commanders of the armies all [the] remnant of Judah who they had come back from all the nations where they had been driven away there to sojourn in [the] land of Judah.
6 Pia wakawaongoza wanaume wote, wanawake na watoto, na binti za mfalme ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha na Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, na nabii Yeremia, na Baruku mwana wa Neria.
The men and the women and the little one[s] and [the] daughters of the king and every person whom he had left Nebuzaradan [the] chief of [the] bodyguards with Gedaliah [the] son of Ahikam [the] son of Shaphan and Jeremiah the prophet and Baruch [the] son of Neriah.
7 Kwa hiyo wakaingia Misri kwa kutokumtii Bwana, wakaenda mpaka Tahpanhesi.
And they went [the] land of Egypt for not they had listened to [the] voice of Yahweh and they came to Tahpanhes.
8 Huko Tahpanhesi neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to Jeremiah in Tahpanhes saying.
9 “Wayahudi wakiwa wanaona, chukua baadhi ya mawe makubwa na kuyazika katika udongo wa mfinyanzi katika njia iliyojengwa kwa matofali katika ingilio la jumba la kifalme la Farao huko Tahpanhesi.
Take in hand your stones large and you will hide them in the mortar in the brick-terrace which [is] at [the] entrance of [the] house of Pharaoh in Tahpanhes to [the] eyes of [the] people Jews.
10 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Nitamtumania mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, nami nitakiweka kiti chake cha enzi juu ya haya mawe niliyoyazika hapa, naye atatandaza hema yake ya ufalme juu yake.
And you will say to them thus he says Yahweh of hosts [the] God of Israel here I [am] about to send and I will fetch Nebuchadnezzar [the] king of Babylon servant my and I will set throne his from above the stones these which I have hidden and he will spread out (state tent his *Q(K)*) over them.
11 Atakuja na kuishambulia Misri, akiwaua wale waliokusudiwa kuuawa, awateke mateka wale waliokusudiwa kutekwa, na upanga kwa wale waliokusudiwa upanga.
(And he will come *Q(K)*) and he will attack [the] land of Egypt [those] who [are] for death to death and [those] who [are] for captivity to captivity and [those] who [are] for the sword to the sword.
12 Atachoma moto mahekalu yao ya miungu ya Misri, atachoma mahekalu yao na kuteka miungu yao. Kama vile mchungaji ajizungushiavyo vazi lake ndivyo atakavyojizungushia Misri na kuondoka mahali hapo bila kudhurika.
And I will kindle fire in [the] houses of [the] gods of Egypt and he will burn them and he will take captive them and he will delouse [the] land of Egypt just as he delouses the shepherd garment his and he will go out from there in peace.
13 Humo ndani ya hekalu la jua nchini ya Misri atabomoa nguzo za ibada, na kuteketeza kwa moto mahekalu ya miungu wa Misri.’”
And he will break [the] sacred pillars of Beth Shemesh which [is] in [the] land of Egypt and [the] houses of [the] gods of Egypt he will burn with fire.

< Yeremia 43 >