< Yeremia 43 >

1 Yeremia alipomaliza kuwaambia watu maneno yote ya Bwana Mungu wao, yaani kila kitu Bwana alichokuwa amemtuma kuwaambia,
Nowe when Ieremiah had made an ende of speaking vnto ye whole people all the wordes of the Lord their God, for the which the Lord their God had sent him to them, euen all these wordes,
2 Azaria mwana wa Hoshaya, na Yohanani mwana wa Karea, na watu wote wenye kiburi wakamwambia Yeremia, “Wewe unasema uongo! Bwana Mungu wetu hajakutuma kusema, ‘Kamwe msiende Misri kukaa huko.’
Then spake Azariah the sonne of Hoshaiah, and Iohanan the sonne of Kareah, and all the proude men, saying vnto Ieremiah, Thou speakest falsely: the Lord our God hath not sent thee to say, Goe not into Egypt to dwell there,
3 Lakini Baruku mwana wa Neria anakuchochea dhidi yetu ili ututie mikononi mwa Wakaldayo, ili watuue au watuchukue uhamishoni Babeli.”
But Baruch ye sonne of Neriah prouoketh thee against vs, for to deliuer vs into the hand of the Caldeans, that they might slay vs, and cary vs away captiues into Babel.
4 Basi Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi, na watu wote wakakataa kutii amri ya Bwana ya kukaa katika nchi ya Yuda.
So Iohanan the sonne of Kareah, and all the captaines of the hoste, and all the people obeied not the voyce of the Lord, to dwell in the lande of Iudah.
5 Badala yake, Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi wakawaongoza mabaki yote ya Yuda waliokuwa wamerudi kuishi katika nchi ya Yuda kutoka mataifa yote ambayo walikuwa wametawanywa.
But Iohanan the sonne of Kareah, and all the captaines of the hoste tooke all the remnant of Iudah, that were returned from al nations, whither they had bene driuen, to dwel in ye land of Iudah:
6 Pia wakawaongoza wanaume wote, wanawake na watoto, na binti za mfalme ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha na Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, na nabii Yeremia, na Baruku mwana wa Neria.
Euen men and women, and children, and the Kinges daughters, and euery person, that Nebuzar-adan the chiefe steward had left with Gedaliah the sonne of Ahikam, ye sonne of Shaphan, and Ieremiah the Prophet, and Baruch the sonne of Neriah.
7 Kwa hiyo wakaingia Misri kwa kutokumtii Bwana, wakaenda mpaka Tahpanhesi.
So they came into the lande of Egypt: for they obeied not the voice of the Lord: thus came they to Tahpanhes.
8 Huko Tahpanhesi neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Then came the worde of the Lord vnto Ieremiah in Tahpanhes, saying,
9 “Wayahudi wakiwa wanaona, chukua baadhi ya mawe makubwa na kuyazika katika udongo wa mfinyanzi katika njia iliyojengwa kwa matofali katika ingilio la jumba la kifalme la Farao huko Tahpanhesi.
Take great stones in thine hand, and hide them in the claie in the bricke kill, which is at the entrie of Pharaohs house in Tanpanhes in ye sight of the men of Iudah,
10 Kisha uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Nitamtumania mtumishi wangu Nebukadneza mfalme wa Babeli, nami nitakiweka kiti chake cha enzi juu ya haya mawe niliyoyazika hapa, naye atatandaza hema yake ya ufalme juu yake.
And say vnto them, Thus sayeth the Lord of hostes the God of Israel, Beholde, I will sende and bring Nebuchad-nezzar the King of Babel my seruant, and will set his throne vpon these stones that I haue hid, and he shall spread his pauilion ouer them.
11 Atakuja na kuishambulia Misri, akiwaua wale waliokusudiwa kuuawa, awateke mateka wale waliokusudiwa kutekwa, na upanga kwa wale waliokusudiwa upanga.
And when he shall come, he shall smite the land of Egypt: such as are appoynted for death, to death, and such as are for captiuitie, to captiuitie, and such as are for the sword to the sword.
12 Atachoma moto mahekalu yao ya miungu ya Misri, atachoma mahekalu yao na kuteka miungu yao. Kama vile mchungaji ajizungushiavyo vazi lake ndivyo atakavyojizungushia Misri na kuondoka mahali hapo bila kudhurika.
And I wil kindle a fire in the houses of the gods of Egypt, and he shall burne them and carie them away captiues, and he shall aray himself with the land of Egypt, as a shepheard putteth on his garment, and shall depart from thence in peace.
13 Humo ndani ya hekalu la jua nchini ya Misri atabomoa nguzo za ibada, na kuteketeza kwa moto mahekalu ya miungu wa Misri.’”
He shall breake also ye images of Beth-shemesh, that is in the lande of Egypt, and the houses of the gods of the Egyptians shall he burne with fire.

< Yeremia 43 >