< Yeremia 42 >
1 Ndipo maafisa wote wa jeshi, pamoja na Yohanani mwana wa Karea, na Yezania mwana wa Hoshaya, na watu wote kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana wakamjia
Then all the captaines of the hoste, and Iohanan the sonne of Kareah, and Iezaniah the sonne of Hoshaaiah, and all the people from the least vnto the most came,
2 Yeremia nabii na kumwambia, “Tafadhali sikia maombi yetu na umwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watu hawa wote waliosalia. Kwa kuwa kama unavyoona sasa, ingawa wakati fulani tulikuwa wengi, sasa tumesalia wachache tu.
And saide vnto Ieremiah the Prophete, Heare our prayer, we beseeche thee, and pray for vs vnto the Lord thy God, euen for all this remnant (for we are left, but a fewe of many, as thine eyes doe beholde)
3 Omba ili Bwana Mungu wako atuambie twende wapi na tufanye nini.”
That the Lord thy God may shewe vs the way wherein wee may walke, and the thing that we may doe.
4 Nabii Yeremia akajibu, “Nimewasikia. Kwa hakika nitamwomba Bwana Mungu wenu kama mlivyoomba. Nitawaambia kila kitu asemacho Bwana, wala sitawaficha chochote.”
Then Ieremiah the Prophet said vnto them, I haue heard you: behold, I will pray vnto ye Lord your God according to your wordes, and whatsoeuer thing the Lord shall answere you, I will declare it vnto you: I will keepe nothing backe from you.
5 Kisha wakamwambia Yeremia, “Bwana na awe shahidi wa kweli na mwaminifu kati yetu kama hatutafanya sawasawa na kila kitu Bwana Mungu wako atakachokutuma utuambie.
Then they said to Ieremiah, The Lord be a witnesse of trueth, and faith betweene vs, if we doe not, euen according to all things for ye which the Lord thy God shall send thee to vs.
6 Likiwa jema au likiwa baya, tutamtii Bwana Mungu wetu, ambaye tunakutuma kwake, ili mambo yote yawe mema kwetu, kwa maana tutamtii Bwana Mungu wetu.”
Whether it be good or euill, we will obey the voyce of the Lord God, to whom we sende thee that it may be well with vs, when wee obey the voyce of the Lord our God.
7 Baada ya siku kumi, neno la Bwana likamjia Yeremia.
And so after ten dayes came the word of the Lord vnto Ieremiah.
8 Kwa hiyo akawaita pamoja Yohanani mwana wa Karea, na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye na watu wote kuanzia mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana.
Then called he Iohanan the sonne of Kareah, and all the captaines of the hoste, which were with him, and all ye people from ye least to the most,
9 Akawaambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye mlinituma kuwasilisha maombi yenu:
And saide vnto them, Thus saith the Lord God of Israel, vnto whom ye sent me to present your prayers before him,
10 ‘Kama mkikaa katika nchi hii, nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa, kwani ninahuzunishwa na maafa niliyowapiga nayo.
If ye will dwell in this land, then I wil build you, and not destroy you, and I will plant you, and not roote you out: for I repent me of the euill that I haue done vnto you.
11 Msimwogope mfalme wa Babeli, ambaye sasa mnamwogopa. Msimwogope, asema Bwana, kwa kuwa niko pamoja nanyi, nami nitawaokoa na kuwaponya kutoka mikononi mwake.
Feare not for the King of Babel, of whom ye are afraide: be not afraid of him, saith the Lord: for I am with you, to saue you, and to deliuer you from his hand,
12 Nitawaonea huruma ili naye awe na huruma nanyi na kuwarudisha katika nchi yenu.’
And I will graunt you mercie that he may haue compassion vpon you, and he shall cause you to dwell in your owne land.
13 “Hata hivyo, kama mkisema, ‘Hatutakaa katika nchi hii,’ hivyo mkaacha kumtii Bwana Mungu wenu,
But if ye say, We will not dwell in this land, neither heare the voyce of the Lord your God,
14 nanyi kama mkisema, ‘Hapana, tutakwenda kuishi Misri, mahali ambapo hatutaona vita au kusikia sauti ya tarumbeta au kuwa na njaa ya chakula,’
Saying, Nay, but we will goe into the land of Egypt, where we shall see no warre, nor heare the sounde of the trumpet, nor haue hunger of bread, and there will we dwell,
15 basi sikieni neno la Bwana, enyi mabaki ya Yuda. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Ikiwa mmekusudia kwenda Misri na kufanya makazi huko,
(And nowe therefore heare the worde of the Lord, ye remnant of Iudah: thus sayeth the Lord of hostes the God of Israel, If ye set your faces to enter into Egypt, and goe to dwell there)
16 basi ule upanga mnaouogopa utawapata huko, na njaa mnayoihofia itawafuata huko Misri, nanyi mtafia huko.
Then the sworde that ye feared, shall take you there in the land of Egypt, and the famine, for the which ye care, shall there hang vpon you in Egypt, and there shall ye die.
17 Naam, wote waliokusudia kwenda kuishi Misri watakufa kwa upanga, njaa na tauni; hakuna hata mmoja wao atakayenusurika au kuokoka maafa nitakayoyaleta juu yao.’
And all the men that set their faces to enter into Egypt to dwell there, shall die by ye sword, by the famine and by the pestilence, and none of them shall remaine nor escape from the plague, that I will bring vpon them.
18 Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama vile hasira yangu na ghadhabu yangu ilivyomwagwa juu ya wale walioishi Yerusalemu, ndivyo ghadhabu yangu itakavyomwagwa juu yenu mtakapokwenda Misri. Mtakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha kulaumia na cha kushutumia, nanyi kamwe hamtaona mahali hapa tena.’
For thus saith the Lord of hostes the God of Israel, As mine anger and my wrath hath bene powred foorth vpon the inhabitants of Ierusalem: so shall my wrath be powred foorth vpon you, when ye shall enter into Egypt, and ye shall be a detestation, and an astonishment, and a curse and a reproche, and ye shall see this place no more.
19 “Enyi mabaki ya Yuda, Bwana amewaambia, ‘Msiende Misri.’ Hakikisheni jambo hili: Ninawaonya leo
O ye remnant of Iudah, the Lord hath said concerning you, Goe not into Egypt: knowe certeinely that I haue admonished you this day.
20 kwamba mmefanya kosa kubwa mioyoni mwenu mliponituma kwa Bwana Mungu wenu na kusema, ‘Mwombe Bwana Mungu wetu kwa ajili yetu, nawe utuambie kila kitu atakachosema, nasi tutafanya.’
Surely ye dissembled in your hearts When ye sent me vnto the Lord your God, saying, Pray for vs vnto the Lord our God, and declare vnto vs euen according vnto al that the Lord our God shall say, and we will doe it.
21 Nimewaambieni leo, lakini bado ninyi hamtaki kumtii Bwana Mungu wenu katika yote aliyonituma niwaambie.
Therefore I haue this day declared it you, but you haue not obeyed the voyce of the Lord your God, nor any thing for the which he hath sent me vnto you.
22 Basi sasa, hakikisheni jambo hili: Mtakufa kwa upanga, njaa na tauni mahali ambapo mnataka kwenda kuishi.”
Nowe therefore, knowe certeinely that ye shall die by the sworde, by the famine, and by the pestilence, in the place whither ye desire to goe and dwell.