< Yeremia 41 >
1 Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
Ngem napasamak nga iti maika-pito a bulan, ni Ismael a putot ni Netanias a putot ni Elisama, a nagtaud iti pamilia dagiti ari, ken sumagmamano nga opisial ti ari-kaduana iti sangapulo a lallaki-ket napanda kenni Gedalias a putot ni Ahikam, idiay Mizpa. Nagsasangoda a nangan idiay Mizpa.
2 Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
Ngem timmakder ni Ismael a putot ni Netanias, ken dagiti sangapulo a lallaki a kaduana ket dinarupda ni Gedalias a putot ni Ahikam a putot ni Safan, babaen iti kampilan. Pinatay ni Ismael ni Gedalias, a dinutokan ti ari ti Babilonia a mangimaton iti daga.
3 Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
Ket pinapatay ni Ismael dagiti amin a Judio a kadua ni Gedalias idiay Mizpa ken dagiti mannakigubat a Caldeo a nasarakanda sadiay.
4 Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
Ket daytoy ti maikadua nga aldaw kalapasan ti panangpapatayda kenni Gedalias, ngem awan ti siasinoman a nakaammo.
5 watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
Adda lallaki nga immay manipud Sikem, Silo, ken Samaria-walopulo a lallaki a nangahit kadagiti barbasda, nangrayab-da kadagiti kawesda, ken nangsugat kadagiti bagbagida-adda iggemda a taraon a maisagut ken insenso nga ipanda iti balay ni Yahweh.
6 Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
Isu a rimmuar ni Ismael a putot ni Netanias manipud Mizpa tapno sabtenna ida bayat ti ipapanda, a magmagna ken agsangsangitda. Ket napasamak nga idi masabatna ida, kinunana kadakuada, “Umaykayo kenni Gedalias a putot ni Ahikam!”
7 Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
Ket napasamak nga idi simrekda iti siudad, pinapatay ida ni Ismael a putot ni Netanias ken intappuakna ida iti abot, isuna ken dagiti lallaki a kakaduana.
8 Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
Ngem adda sangapulo a lallaki a kadakuada a nagkuna kenni Ismael, “Saannakami a papatayen, ta adda taraonmi kadagiti taltalonmi: trigo ken sebada, lana ken diro.” Isu a saanna ida a pinapatay agraman dagiti dadduma a kakaduada.
9 Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
Ti abot a nangibellengan ni Ismael kadagiti bangkay dagiti lallaki a pinapatayda agraman ni Gedalias-daytoy a dakkel nga abot ket kinali ni Ari Asa idi rinaut ida ni Ari Baasa nga ari ti Israel. Pinunno daytoy ni Ismael a putot ni Netanias kadagiti pinapatayna.
10 Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
Ti simmaruno ket tiniliw amin ni Ismael dagiti tattao nga adda idiay Mizpa, dagiti babbai a putot ti ari ken amin dagiti tattao a nabatbati idiay Mizpa nga impaaywan ni Nebuzaradan, a pangulo dagiti agbanbantay, kenni Gedalias a putot ni Ahikam. Tiniliw ngarud ida ni Ismael a putot ni Netanias ket kalpasanna, pimmanaw tapno bumallasiw iti ayan dagiti tattao ti Ammon.
11 Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
Ngem nadamag ni Johanan a putot ni Karea ken dagiti amin a mangidadaulo a kaduana dagiti amin a dakes nga inaramid ni Ismael a putot ni Netanias.
12 waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
Isu nga inummongda amin dagiti tattaoda ket napanda nakiranget kenni Ismael a putot ni Netanias. Nasarakanda isuna iti nalawa a pagdigusan idiay Gabaon.
13 Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
Ket napasamak nga idi nakita dagiti amin a tattao a kadua ni Ismael ni Johanan a putot ni Karea ken dagiti amin a mangidadaulo ti armada a kakaduana, naragsakanda unay.
14 Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
Isu nga amin dagiti tattao a tiniliw ni Ismael idiay Mizpa ket nagsubli ket napanda kenni Johanan a putot ni Karea.
15 Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
Ngem naglibas ni Ismael a putot ni Netanias a kaduana dagiti walo a lallaki manipud kenni Johanan. Napan isuna kadagiti tattao ti Ammon.
16 Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
Inkuyog ni Johanan, a putot ni Karea ken dagiti amin a mangidadaulo kadagiti armada, dagiti amin a tattao manipud Mizpa a naispal manipud kenni Ismael a putot ni Netanias. Daytoy ket kalpasan iti panangpapapatay ni Ismael kenni Gedalias a putot ni Ahikam. Innala ni Johanan ken dagiti kakaduana dagiti napipigsa a lallaki, dagiti mannakigubat a lallaki, dagiti babbai ken ubbing, ken dagiti eunoko a naispal idiay Gabaon.
17 Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
Ket napanda naggian iti apagbiit idiay Gerut Kimham, nga asideg iti Betlehem. Mapanda koma idiay Egipto
18 ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.
gapu kadagiti Caldeo. Mabutengda kadakuada agsipud ta pinapatay ni Ismael a putot ni Netanias ni Gedalias a putot ni Ahikam, a dinutokan ti ari ti Babilonia a mangituray iti daga.