< Yeremia 41 >

1 Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
Or, au septième mois, Ismaël, fils de Nethania, fils d'Elishama, de la race royale et l'un des principaux officiers du roi, et dix hommes avec lui, vinrent auprès de Guedalia, fils d'Ahikam, à Mitspa; et là ils mangèrent ensemble le pain à Mitspa.
2 Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
Alors Ismaël, fils de Nethania, se leva, avec les dix hommes qui étaient avec lui, et frappa avec l'épée Guedalia, fils d'Ahikam, fils de Shaphan, et le tua, lui que le roi de Babylone avait établi gouverneur du pays.
3 Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
Ismaël tua aussi tous les Juifs qui étaient avec Guedalia à Mitspa, et les hommes de guerre chaldéens qui s'y trouvaient.
4 Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
Le deuxième jour après qu'il eut tué Guedalia, et que personne ne l'eut su,
5 watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
des hommes vinrent de Sichem, de Silo et de Samarie, quatre-vingts hommes, la barbe rasée, les vêtements déchirés, et s'étant coupés, avec des offrandes et de l'encens à la main, pour les amener à la maison de Yahvé.
6 Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
Ismaël, fils de Nethania, sortit de Mitspa pour aller au-devant d'eux, en pleurant tout le long de son chemin; et, lorsqu'il les rencontra, il leur dit: « Venez vers Guedalia, fils d'Ahikam. »
7 Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
Lorsqu'ils arrivèrent au milieu de la ville, Ismaël, fils de Nethania, les tua et les jeta au milieu de la fosse, lui et les hommes qui étaient avec lui.
8 Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
Mais on trouva dix hommes parmi ceux qui dirent à Ismaël: « Ne nous tue pas, car nous avons des provisions cachées dans les champs, du blé et de l'orge, de l'huile et du miel. » Il s'arrêta donc, et ne les tua pas parmi leurs frères.
9 Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
Et la fosse dans laquelle Ismaël jeta tous les cadavres des hommes qu'il avait tués, près de Guedalia (c'était celle qu'avait faite le roi Asa par crainte de Baescha, roi d'Israël), Ismaël, fils de Nethania, la remplit de ceux qui avaient été tués.
10 Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
Et Ismaël emmena captif tout le peuple qui était resté à Mitspa, même les filles du roi, et tout le peuple qui était resté à Mitspa, que Nebuzaradan, chef des gardes, avait confié à Guedalia, fils d'Ahikam. Ismaël, fils de Nethania, les emmena captifs, et partit pour passer chez les enfants d'Ammon.
11 Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
Mais lorsque Johanan, fils de Karéa, et tous les chefs des troupes qui étaient avec lui, apprirent tout le mal qu'avait fait Ismaël, fils de Nethania,
12 waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
ils prirent tous les hommes et allèrent combattre Ismaël, fils de Nethania, et ils le trouvèrent près des grandes eaux qui sont à Gabaon.
13 Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
Et quand tout le peuple qui était avec Ismaël vit Johanan, fils de Karéah, et tous les chefs des troupes qui étaient avec lui, ils se réjouirent.
14 Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
Et tout le peuple qu'Ismaël avait emmené captif de Mitspa se retourna et revint, et alla vers Johanan, fils de Karéah.
15 Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
Mais Ismaël, fils de Nethania, échappa à Johanan avec huit hommes, et alla vers les fils d'Ammon.
16 Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
Alors Johanan, fils de Karéa, et tous les chefs des troupes qui étaient avec lui, prirent tout le reste du peuple qu'il avait récupéré d'Ismaël, fils de Nethania, à Mitspa, après qu'il eut tué Guedalia, fils d'Ahikam, les hommes de guerre, avec les femmes, les enfants et les eunuques, qu'il avait ramenés de Gabaon.
17 Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
Ils partirent et s'établirent à Geruth Chimham, qui est près de Bethléem, pour aller entrer en Égypte
18 ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.
à cause des Chaldéens; car ils avaient peur d'eux, parce qu'Ismaël, fils de Nethania, avait tué Guedalia, fils d'Ahikam, que le roi de Babylone avait établi gouverneur du pays.

< Yeremia 41 >