< Yeremia 41 >
1 Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
But it happened that in the seventh month Ishmael son of Nethaniah son of Elishama, from the royal family, and some officers of the king, came—ten men were with him—to Gedaliah son of Ahikam, at Mizpah. They ate food together there in Mizpah.
2 Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
But Ishmael son of Nethaniah, and the ten men who were with him rose up and attacked Gedaliah son of Ahikam son of Shaphan, with the sword. Ishmael killed Gedaliah, whom the king of Babylon had put in charge of the land.
3 Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
Then Ishmael killed all the Judeans who were with Gedaliah in Mizpah and the Chaldean fighting men found there.
4 Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
Then it was the second day after the killing of Gedaliah, but no one knew.
5 watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
Some men came from Shechem, from Shiloh, and from Samaria—eighty men who had shaved their beard, torn their clothes, and cut themselves—with food offerings and frankincense in their hands to go to Yahweh's house.
6 Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
So Ishmael son of Nethaniah went out from Mizpah to meet them as they went, walking and weeping. Then it happened that as he encountered them, he said to them, “Come to Gedaliah son of Ahikam!”
7 Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
It came about that when they came into the city, Ishmael son of Nethaniah slaughtered them and threw them into a pit, he and the men who were with him.
8 Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
But there were ten men among them who said to Ishmael, “Do not kill us, for there are provisions of ours in a field: Wheat and barley, oil and honey.” So he did not kill them with their other companions.
9 Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
The cistern where Ishmael threw all the dead bodies that he had killed, was a large cistern that King Asa dug to make a defense against King Baasha of Israel. Ishmael son of Nethaniah filled it in with the dead.
10 Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
Next Ishmael captured all the other people who were in Mizpah, the king's daughters and all the people who were left in Mizpah whom Nebuzaradan the chief guard had assigned to Gedaliah son of Ahikam. So Ishmael son of Nethaniah captured them and went to cross over to the people of Ammon.
11 Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
But Johanan son of Kareah and all the army commanders with him heard of all the harm that Ishmael son of Nethaniah had done.
12 waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
So they took all their men and went to fight against Ishmael son of Nethaniah. They found him at the great pool of Gibeon.
13 Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
Then it happened that when all the people who were with Ishmael saw Johanan son of Kareah and all the army commanders who were with him, they were very happy.
14 Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
So all the people whom Ishmael had captured at Mizpah turned around and went to Johanan son of Kareah.
15 Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
But Ishmael son of Nethaniah fled with eight men from Johanan. He went to the people of Ammon.
16 Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
Johanan son of Kareah and all the army commanders with him took from Mizpah all the people who had been rescued from Ishmael son of Nethaniah. This was after Ishmael had killed Gedaliah son of Ahikam. Johanan and his companions took the strong men, the fighting men, the women and children, and the eunuchs who had been rescued at Gibeon.
17 Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
Then they went and stayed for a while in Geruth Kimham, which is near Bethlehem. They were going to go to Egypt
18 ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.
because of the Chaldeans. They were afraid of them since Ishmael son of Nethaniah had killed Gedaliah son of Ahikam, whom the king of Babylon had put in charge of the land.