< Yeremia 41 >
1 Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
And it came to pass in the seventh month, that Ishmael, the son of Nethaniah, the son of Elishama, of the blood royal, and one of the great officers of the king, and ten men with him, came to Gedaliah, the son of Ahikam, to Mizpah; and they ate bread there together in Mizpah.
2 Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
Then Ishmael, the son of Nethaniah, arose, and the ten men that were with him, and smote Gedaliah, the son of Ahikam, the son of Shaphan, with the sword, and slew him whom the king of Babylon had made governor over the land.
3 Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
And all the Jews that were with him, with Gedaliah at Mizpah, and the Chaldaeans that were found there, the men of war, did Ishmael smite.
4 Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
And it came to pass, the second day after he had slain Gedaliah, and no man knew it,
5 watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
that there came certain men from Shechem, from Shiloh, and from Samaria, fourscore persons, having their beards shaven, and their clothes rent, and having cut themselves, with an oblation and incense in their hands, to bring to the house of Jehovah.
6 Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
And Ishmael, the son of Nethaniah, went forth from Mizpah to meet them, weeping all along as he went; and when he met them, he said to them, “Come ye to Gedaliah, the son of Ahikam.”
7 Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
And when they had come into the midst of the city, Ishmael, the son of Nethaniah, slew them, and cast them into the pit, he and the men that were with him.
8 Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
But ten men were found among them who said to Ishmael, “Slay us not, for we have hidden stores in the field, of wheat, and barley, and oil, and honey.” He forbore, therefore, and slew them not with their brethren.
9 Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
Now the pit into which Ishmael cast all the dead bodies of the men whom he slew, together with Gedaliah, is the same which King Asa made on account of Baasha, king of Israel; and Ishmael, the son of Nethaniah, filled it with them that were slain.
10 Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
And Ishmael took captive all the residue of the people that were in Mizpah, the king's daughters, and all the people that remained in Mizpah, whom Nebuzaradan, captain of the guard, had committed to the charge of Gedaliah, the son of Ahikam; even Ishmael, the son of Nethaniah, took them captive, and set forth to go over [[the Jordan]] to the children of Ammon.
11 Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
But when Johanan, the son of Kareah, and all the captains of the forces that were with him, heard of all the evil which Ishmael, the son of Nethaniah, had done,
12 waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
they took all the men, and went up to fight with Ishmael, the son of Nethaniah, and came up with him at the great waters that are in Gibeon.
13 Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
And when all the people which were with Ishmael saw Johanan, the son of Kareah, and all the captains of the forces that were with him, they were glad;
14 Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
and all the people that Ishmael had carried away captive from Mizpah faced about and returned, and went to Johanan, the son of Kareah.
15 Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
But Ishmael, the son of Nethaniah, escaped from Johanan with eight men, and went to the children of Ammon.
16 Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
Then took Johanan, the son of Kareah, and all the captains of the forces that were with him, all the remnant of the people whom he had recovered from Ishmael, the son of Nethaniah, from Mizpah, after he had slain Gedaliah, the son of Ahikam, strong men, men of war, and women, and children, and eunuchs, whom he had brought back from Gibeon;
17 Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
and they went, and tarried in the inn of Chimham, which is near Bethlehem, in order to flee into Egypt
18 ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.
from the Chaldaeans; for they were afraid of them, because Ishmael, the son of Nethaniah, had slain Gedaliah, the son of Ahikam, whom the king of Babylon had made governor over the land.