< Yeremia 41 >

1 Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
But in the seuenth moneth came Ishmael the sonne of Nethaniah, the sonne of Elishama of the seede royall, and the princes of the King, and tenne men with him, vnto Gedaliah the sonne of Ahikam to Mizpah, and there they did eate bread together in Mizpah.
2 Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
Then arose Ishmael the sonne of Nethaniah with these tenne men that were with him, and smote Gedaliah the sonne of Ahikam the sonne of Shaphan with the sword, and slewe him, whom the King of Babel had made gouernour ouer the lande.
3 Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
Ishmael also slewe all the Iewes that were with Gedaliah at Mizpah, and all the Caldeans that were found there, and the men of warre.
4 Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
Now the second day that he had slaine Gedaliah, and no man knewe it,
5 watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
There came men from Shechem, from Shiloh, and from Samaria, euen fourescore men, hauing their beardes shauen, and their clothes rent and cut, with offerings and incense in their hands to offer in the house of the Lord.
6 Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
And Ishmael the sonne of Nethaniah went forth from Mizpah to meete them, weeping as he went: and when he met them, he said vnto them, Come to Gedaliah the sonne of Ahikam.
7 Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
And when they came into the middes of the citie, Ishmael the sonne of Nethaniah slewe them, and cast them into the middes of the pit, he and the men that were with him.
8 Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
But tenne men were founde among them, that saide vnto Ishmael, Slay vs not: for we haue treasures in the fielde, of wheate, and of barley, and of oyle, and of honie: so he stayed, and slew them not among their brethren.
9 Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
Now the pit wherein Ishmael had cast the dead bodies of the men (whom he had slayne because of Gedaliah) is it, which Asa the King had made because of Basha King of Israel, and Ishmael the sonne of Nethaniah filled it with them that were slaine.
10 Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
Then Ishmael caryed away captiue all the residue of the people that were in Mizpah, euen the Kings daughters, and all the people that remained in Mizpah, whom Nebuzar-adan the chiefe steward had committed to Gedaliah the sonne of Ahikam, and Ishmael the sonne of Nethaniah caried them away captiue, and departed to goe ouer to the Ammonites.
11 Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
But when Iohanan the sonne of Kareah, and all the captaines of the hoste that were with him, heard of all the euill that Ishmael the sonne of Nethaniah had done,
12 waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
Then they all tooke their men, and went to fight with Ishmael the sonne of Nethaniah, and founde him by ye great waters that are in Gibeon.
13 Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
Nowe when all the people whom Ishmael caryed away captiue, sawe Iohanan the sonne of Kareah, and all the captaines of the hoste, that were with him, they were glad.
14 Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
So all the people, that Ishmael had caryed away captiue from Mizpah, returned and came againe, and went vnto Iohanan the sonne of Kareah.
15 Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
But Ishmael the sonne of Nethaniah, escaped from Iohanan with eight men, and went to the Ammonites.
16 Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
Then tooke Iohanan the sonne of Kareah, and all the captaines of the hoste that were with him, all the remnant of the people, whom Ishmael the sonne of Nethaniah had caried away captiue from Mizpah, (after that he had slaine Gedaliah the sonne of Ahikam) euen the strong men of warre, and the women, and the children, and the eunuches, whom hee had brought againe from Gibeon:
17 Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
And they departed and dwelt in Geruth Chimham, which is by Beth-lehem, to goe and to enter into Egypt,
18 ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.
Because of the Caldeans: for they feared them, because Ishmael ye sonne of Nethaniah had slaine Gedaliah the sonne of Ahikam, whom the King of Babel made gouernour in the land.

< Yeremia 41 >