< Yeremia 41 >
1 Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
Now it came about in the seventh month that Ishmael, the son of Nethaniah, the son of Elishama, of the king's seed, having with him ten men, came to Gedaliah, the son of Ahikam, in Mizpah; and they had a meal together in Mizpah.
2 Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
Then Ishmael, the son of Nethaniah, and the ten men who were with him, got up, and attacking Gedaliah, the son of Ahikam, the son of Shaphan, with the sword, put to death him whom the king of Babylon had made ruler over the land.
3 Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
And Ishmael put to death all the Jews who were with him, even with Gedaliah, at Mizpah, and the Chaldaean men of war.
4 Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
Now on the second day after he had put Gedaliah to death, when no one had knowledge of it,
5 watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
Some people came from Shechem, from Shiloh and Samaria, eighty men, with the hair of their faces cut off and their clothing out of order, and with cuts on their bodies, and in their hands meal offerings and perfumes which they were taking to the house of the Lord.
6 Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
And Ishmael, the son of Nethaniah, went out from Mizpah with the purpose of meeting them, weeping on his way: and it came about that when he was face to face with them he said, Come to Gedaliah, the son of Ahikam.
7 Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
And when they came inside the town, Ishmael, the son of Nethaniah, and the men who were with him, put them to death and put their bodies into a deep hole.
8 Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
But there were ten men among them who said to Ishmael, Do not put us to death, for we have secret stores, in the country, of grain and oil and honey. So he did not put them to death with their countrymen.
9 Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
Now the hole into which Ishmael had put the dead bodies of the men whom he had put to death, was the great hole which Asa the king had made for fear of Baasha, king of Israel: and Ishmael, the son of Nethaniah, made it full of the bodies of those who had been put to death.
10 Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
Then Ishmael took away as prisoners all the rest of the people who were in Mizpah, the king's daughters and all the people still in Mizpah, whom Nebuzaradan, the captain of the armed men, had put under the care of Gedaliah, the son of Ahikam: Ishmael, the son of Nethaniah, took them away prisoners with the purpose of going over to the children of Ammon.
11 Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
But when Johanan, the son of Kareah, and all the captains of the armed forces who were with him, had news of all the evil which Ishmael, the son of Nethaniah, had done,
12 waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
They took their men and went out to make war on Ishmael, the son of Nethaniah, and they came face to face with him by the great waters in Gibeon.
13 Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
Now when all the people who were with Ishmael saw Johanan, the son of Kareah, and all the captains of the forces with him, then they were glad.
14 Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
And all the people whom Ishmael had taken away prisoners from Mizpah, turning round, came back and went to Johanan, the son of Kareah.
15 Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
But Ishmael, the son of Nethaniah, got away from Johanan, with eight men, and went to the children of Ammon.
16 Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
Then Johanan, the son of Kareah, and all the captains of the forces who were with him, took all the rest of the people whom Ishmael, the son of Nethaniah, had made prisoners, after he had put to death Gedaliah, the son of Ahikam, the people from Mizpah, that is, the men of war and the women and the children and the unsexed servants, whom he had taken back with him from Gibeon:
17 Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
And they went and were living in the resting-place of Chimham, which is near Beth-lehem on the way into Egypt,
18 ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.
Because of the Chaldaeans: for they were in fear of them because Ishmael, the son of Nethaniah, had put to death Gedaliah, the son of Ahikam, whom the king of Babylon had made ruler over the land.