< Yeremia 41 >
1 Katika mwezi wa saba Ishmaeli mwana wa Nethania mwana wa Elishama, aliyekuwa wa uzao wa mfalme na pia alikuwa mmoja wa maafisa wa mfalme, akaja pamoja na watu kumi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu huko Mispa. Walipokuwa wakila pamoja huko,
Chuche kum, lha sagi lhin in, leng insungmi khat, Nethaniah chapa Ishmael, leng inpia jong vaihom pipu khat chu, pasal misomtoh Mizpah khoa Gedaliah toh kimuto ding in acheuvin ahi. Abonchauva an anehkhom laitah un,
2 Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na wale watu kumi waliokuwa pamoja naye waliinuka na kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani kwa upanga, wakamuua yule ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua awe mtawala wa nchi.
Ishmael leh alhonpi pasal misom hochun, chemjam asatdoh un, Babylon lengpan gamvaipoa apansah Gedaliah chu, athattauve.
3 Ishmaeli akawaua pia Wayahudi wote waliokuwa na Gedalia huko Mispa, pamoja na askari wa Kikaldayo waliokuwa huko.
Ishmael in Gedaliah toh umkhom Judah miho leh Babylon sepaite jouse, abonchauvin athatgam heltai.
4 Siku moja baada ya kuuawa kwa siri kwa Gedalia, kabla mtu yeyote hajafahamu jambo hilo,
Ajing nikhon, Gedaliah kitha thu, mi koimachan ahetdoh masang in,
5 watu themanini waliokuwa wamenyoa ndevu zao, waliorarua nguo zao na kujikatakata walikuja kutoka Shekemu, Shilo na Samaria wakileta sadaka za nafaka na uvumba katika nyumba ya Bwana.
Shechem khoa kon, Shiloh khoa chule Samaria khoa kon in, pasal somget hochu, Pakai Houin a, thilto bolding in ahungtauve. Amaho chun anemul akihet tol uvin, aponsil u abottel uvin, chule atahsa chungu aki-atpop un, Houin a toding Chang le gimnamtwi ahinchoi uvin ahi.
6 Ishmaeli mwana wa Nethania akaondoka Mispa ili kwenda kuwalaki, huku akilia alipokuwa akienda. Alipokutana nao, akasema, “Karibuni kwa Gedalia mwana wa Ahikamu.”
Hichun, amaho chutoh gakimuto dimg in, Ishmael in Mizpah akon in akipat doh in, kappum pum in achei. Amaho kom alhunphat in, aman ajah uva, “Hungun, Ahikam chapa Gedaliah khu, ipin alhunden hitam, Hung veuvin,” ati.
7 Walipoingia mjini, Ishmaeli mwana wa Nethania na wale watu waliokuwa pamoja naye wakawachinja na kuwatupa ndani ya kisima.
Amaho chu khopi sung ahunglut phat un, Ismael leh alhonpi ho chun, hiche miho chu, misom tilou adangse abonchauvin athatgam’un, twikul a alehlut tauvin ahi.
8 Lakini watu kumi miongoni mwao wakamwambia Ishmaeli, “Sisi usituue! Tuna ngano na shayiri, mafuta na asali, vilivyofichwa katika shamba.” Kwa hiyo akawaacha na hakuwaua pamoja na wale wengine.
Adang misom hochun, Ismael jah’a, “Neithat hih un, keihon loujaova suhlou chang tampi, sakol chang tampi, Olive thao leh Khoiju tampi kasel uve, nangdin nahin choipeh nauving’e,” atiuvin ahi. Hijeh chun amaho chu ahinghoiyin ahi.
9 Basi kile kisima ambacho alitupa zile maiti za watu aliowaua pamoja na Gedalia kilikuwa ni kile kisima ambacho Mfalme Asa alikifanya sehemu ya ulinzi wake dhidi ya Baasha mfalme wa Israeli. Ishmaeli mwana wa Nethania akakijaza kisima hicho kwa maiti.
Ishmael in amitha ho alelutna twikul chu, Asa lengpan Israel lengpa Baasha douna-a, chule ama kivenne ding’a, Mizpah khoa kulpi asem laiya, anasemdoh twikul lentah ahi. Hiche twikul chu Ishmael in amitha ho adipsettan ahi.
10 Ishmaeli akawafanya mateka watu wote ambao Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme alikuwa amewaacha huko Mispa na kumweka Gedalia mwana wa Ahikamu juu yao: walikuwa binti za mfalme pamoja na watu wote aliokuwa amewaacha huko. Ishmaeli mwana wa Nethania akawachukua mateka na kuondoka nao, akavuka kwenda kwa Waamoni.
Hichun Ishmael in Mizpah khoa umden ho, lengpa Chanute ahiuvin chule midang akidalha amoh chengse ahiuvin, in-ngah lamkaipa Nebuzaradan vettup na noiya umjouse chu, abonchauvin aman in ahentai. Ismael in amaho chu, Ammon mite gamlang’a sohchang ding in akaiyin, akipatdoh tai.
11 Yohanani mwana wa Karea na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye waliposikia juu ya uhalifu wote ambao Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa ameufanya,
Kareah chapa Johanan leh aumpi gal lamkai danghon, Ishmael thilse bolchu ajadoh tauve.
12 waliwachukua watu wao wote kwenda kupigana na Ishmaeli mwana wa Nethania. Wakakutana naye karibu na bwawa kubwa huko Gibeoni.
Hijeh chun, amahon amiteu akipuiyun, Nethaniah chapa Ishmael sat ding in adel tauvin ahi. Amahon Ishmael chu Gebion mun’a twikul-len umna-a chun aphapan tauvin ahi.
13 Ikawa watu wote waliokuwa na Ishmaeli walipomwona Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wa jeshi waliokuwa pamoja naye, wakafurahi.
Hichun Ishmael in sohchanga akaiho chun, Johanan leh alhonpi gal lamkai ho amuphat un, akipah behseh un a eojah tauve.
14 Watu wote ambao Ishmaeli alikuwa amewachukua mateka huko Mispa wakageuka na kumfuata Yohanani mwana wa Karea.
Sohchanga akaiho jouse chu, Johanan lang’a ahung lheilut soh keiyun, apangkhom tauvin ahi.
15 Lakini Ishmaeli mwana wa Nethania pamoja na watu wake wanane wakamtoroka Yohanani na kukimbilia kwa Waamoni.
Hichun Ishmael leh aloi mi get chu Johanan khut’a kon in ajamdoh man’un, Ammon gamsung’a ajamlut tauve.
16 Ndipo Yohanani mwana wa Karea pamoja na maafisa wote wa jeshi waliokuwa pamoja naye wakawaongoza wote walionusurika kutoka Mispa, ambao walipona kutoka mikononi mwa Ishmaeli mwana wa Nethania baada yake kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu: walikuwa askari, wanawake, watoto na matowashi aliowaleta kutoka Gibeoni.
Chuin Kareah chapa Johanan leh alhonpi gal lamkai hochun, Ishmael in Gedaliah atha jouva sohchang’a akaimangho: Sepai ho, numei ho, chapangho, chule nu-kiso ho, Gibeon mun’a ahuhdoh chengseu chu abonchauvin apui tauve.
17 Kisha wakaenda mbele na kutua Geruth-Kimhamu karibu na Bethlehemu wakiwa njiani kwenda Misri
Amahon ami huhdoh chengseu chu, Bethlehem kom’a Geruth Kimham kho’a chun apuiyun, Egypt gam jonpai ding in akigouvin ahi.
18 ili kuwatoroka Wakaldayo. Waliwaogopa kwa sababu Ishmaeli mwana wa Nethania alikuwa amemuua Gedalia mwana wa Ahikamu, ambaye alikuwa amewekwa na mfalme wa Babeli kuwa mtawala wa nchi.
Ajeh chu, Babylon miten Ahikam chapa Gedaliah, Babylon lengpan Judah gamvaipo a apansah pachu, Ishmael in athattai tithu ahin jahdoh ding chu, kicha ahiuve.