< Yeremia 4 >

1 “Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
Ja tu atgriezīsies, Israēl, saka Tas Kungs, pie Manis atgriezīsies, un ja tu savas negantības Manā priekšā atstāsi un neskraidīsi apkārt,
2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
Un ja tu zvērēsi: „tik tiešām kā Tas Kungs dzīvo!“Ar patiesību, ar tiesu un ar taisnību, tad tautas iekš viņa svētīsies un ar viņu lielīsies.
3 Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
Jo tā saka Tas Kungs uz Jūda un Jeruzālemes vīriem: ariet sev jaunu zemi un nesējat ērkšķos.
4 Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
Apgraizaties Tam Kungam un atņemat nost savas sirds priekšādu, Jūda vīri un Jeruzālemes iedzīvotāji, ka Mana bardzība neizšaujās kā uguns un nedeg, ka neviens nevar dzēst, jūsu nedarbu dēļ.
5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
Sludinājiet Jūdā un Jeruzālemē, liekat to dzirdēt un stāstiet, bazūnējat ar bazūni tai zemē, sauciet ar pilnu muti un sakāt: sapulcinājaties un iesim stiprās pilsētās.
6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
Paceļat karogu uz Ciānu, bēgat, nestāvat. Jo Es atvedu nelaimi no ziemeļa puses un lielu postu.
7 Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
Lauva ceļas no sava biezuma, un tautu maitātājs nāk; viņš ir izgājis no savas vietas, tavu zemi darīt tukšu, lai tavas pilsētas top izpostītas, ka neviens tur vairs nedzīvo.
8 Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
Tādēļ apjoziet maisus, žēlojaties un kauciet, jo Tā Kunga bardzības karstums no mums neatstājās.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
Tai dienā, saka Tas Kungs, iznīks ķēniņa sirds drošība un lielo kungu sirds drošība, un priesteri izbīsies, un pravieši iztrūcināsies.
10 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
Tad es sacīju: ak Kungs, Dievs! Patiesi, šiem ļaudīm un Jeruzālemei Tu esi ļāvis kļūt lielā viltū, ka sacīja: jums būs miers! Kur tomēr zobens sniedzās līdz pat dvēselei.
11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
Tanī laikā sacīs uz šiem ļaudīm un uz Jeruzālemi: sauss vējš nāk no augstiem tuksneša kalniem pret Manu tautu, ne vētīšanas, ne tīrīšanas pēc.
12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
Vējš Man nāks, kas stiprāks būs nekā viņi, tad arī Es nesīšu tiesu pret viņiem.
13 Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
Redzi, viņš cēlās kā debesis, un viņa rati ir kā viesulis, viņa zirgi ir čaklāki nekā ērgļi, - ak vai, mums, jo mēs esam postā!
14 Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
Mazgā savu sirdi no ļaunuma, Jeruzāleme, ka topi izglābta; cik ilgi tu savas nelietības domas glabāsi savā sirdī?
15 Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
Jo balss sludina no Dana un ziņo bēdas no Efraīma kalniem.
16 “Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
Dariet pagāniem zināmu, redzi, sludinājiet par Jeruzālemi: sargi nāk no tālas zemes, un tie paceļ savu balsi pret Jūda pilsētām.
17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
Kā sargi ap tīrumu, tā tie būs visapkārt pret viņu, tādēļ ka tā pret Mani cēlusies, saka Tas Kungs.
18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
Tavs ceļš un tavi nedarbi tev to padara; tā ir tava blēdība, kas tik rūgta, ka tā sniedzās līdz pat tavai sirdij.
19 Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
Ak manas iekšas, manas iekšas! Kā bērnu sāpes man spiežas caur manu sirdi, mana sirds lec iekš manis, es nevaru klusu ciest, jo mana dvēsele dzird bazūnes skaņu un kara troksni.
20 Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
Posts pār postu tiek daudzināts. Jo visa zeme ir postīta, piepeši ir postīti mani dzīvokļi, acumirklī manas teltis.
21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
Cik ilgi jel man būs redzēt karogu, dzirdēt bazūnes skaņu?
22 “Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
Tiešām, mani ļaudis ir traki un mani nepazīst; tie ir ģeķīgi bērni un neprātīgi. Tie gan ir gudri, ļaunu darīt, bet labu darīt tie nemāk.
23 Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
Es uzlūkoju zemi, un redzi, tā ir tumša un tukša, - un debesi, un viņai nav sava gaišuma.
24 Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
Es uzlūkoju kalnus, un redzi, tie dreb, un visi kalni trīc.
25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
Es lūkoju, un redzi, neviena cilvēka nav, un visi putni apakš debess ir aizskrējuši.
26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
Es lūkoju, un redzi, auglīgais lauks ir tuksnesis, un visas viņa pilsētas ir salauztas priekš Tā Kunga un priekš Viņa bardzības karstuma.
27 Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
Jo tā saka Tas Kungs: visa tā zeme būs postā, tomēr Es to neizpostīšu pavisam.
28 Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
Tādēļ zeme bēdāsies, un debess augšām aptumšosies, jo Es to esmu runājis un apņēmies, un tas Man nebūs žēl, un no tā Es neatkāpšos.
29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
Visas pilsētas bēgs no jātnieku un strēlnieku trokšņa, tie ies biezos mežos un kāps uz klints kalniem, visas pilsētas taps atstātas, un neviena nebūs, kas tur dzīvos.
30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
Ko tu tad darīsi, tu postītā? Jebšu tu apģērbsies ar purpuru, jebšu tu izgreznosies ar zelta glītumu, jebšu tu savas acis darīsi jaukas, tad tu tomēr velti izgreznosies. Tie drauģeļi tevi apsmies, tie meklēs tavu dvēseli.
31 Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”
Jo Es dzirdu kā dzemdētājas balsi, vaidēšanu, kā no tās, kas cieš pirmās bērnu sāpes, Ciānas meitas balsi; tā vaid un izpleš savas rokas: ak vai, man! Jo manu dvēseli nomāc slepkavas.

< Yeremia 4 >