< Yeremia 4 >
1 “Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
Israël, si tu reviens, si tu reviens à moi, dit l'Éternel, si tu ôtes tes abominations de devant moi, tu ne seras plus errant.
2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
Et tu jureras: L'Éternel est vivant! en vérité, en équité et en justice. Alors les nations seront bénies en lui, et se glorifieront en lui.
3 Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
Car ainsi a dit l'Éternel aux hommes de Juda et de Jérusalem
4 Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
Soyez circoncis à l'Éternel, et circoncisez vos cœurs, hommes de Juda, habitants de Jérusalem! De peur que ma fureur ne sorte comme un feu, et qu'elle ne s'enflamme, sans que personne ne l'éteigne, à cause de la méchanceté de vos actions.
5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
Annoncez en Juda, et publiez à Jérusalem, et dites: Sonnez de la trompette dans le pays. Criez à pleine voix, dites: Assemblez-vous, et allons aux villes fortes!
6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
Élevez l'étendard vers Sion! Fuyez et ne vous arrêtez pas! Car j'amène du Nord le mal, une grande ruine.
7 Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
Le lion monte hors de son fourré; le destructeur des nations est en marche; il est sorti de son lieu pour faire de ton pays une désolation, pour que tes villes soient ruinées, et qu'il n'y ait plus d'habitants.
8 Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
C'est pourquoi ceignez-vous de sacs, lamentez-vous et gémissez; car l'ardeur de la colère de l'Éternel ne s'est point détournée de vous.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
Et en ce jour-là, dit l'Éternel, le cœur du roi et le cœur des chefs seront éperdus; les sacrificateurs seront troublés, et les prophètes seront stupéfaits.
10 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
Et je dis: Ah! Seigneur Éternel! Tu as donc véritablement abusé ce peuple et Jérusalem, en disant: Vous aurez la paix! et l'épée a pénétré jusqu'à l'âme.
11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
En ce temps-là, il sera dit à ce peuple et à Jérusalem: Un vent brûlant souffle des lieux élevés du désert, sur le chemin de la fille de mon peuple; non pour vanner, ni pour nettoyer.
12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
Plus impétueux est le vent qui viendra de ma part. Maintenant je prononcerai mes jugements sur eux.
13 Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
Voici, il monte comme des nuées, et ses chars sont comme un tourbillon. Ses chevaux sont plus légers que les aigles. Malheur à nous, car nous sommes détruits!
14 Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
Jérusalem, purifie ton cœur du mal, afin que tu sois délivrée. Jusqu'à quand entretiendras-tu des pensées mauvaises au-dedans de toi?
15 Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
Car une voix apporte des nouvelles de Dan; elle annonce l'affliction depuis la montagne d'Éphraïm.
16 “Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
Rappelez-le aux nations! Voici, publiez-le contre Jérusalem! Les assiégeants viennent d'un pays éloigné, et ils ont jeté leur cri contre les villes de Juda.
17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
Ils se sont mis tout autour d'elle, comme ceux qui gardent un champ; car elle m'a été rebelle, dit l'Éternel.
18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
Ta conduite, tes actions t'ont préparé ces choses; c'est là le fruit de ta méchanceté; oui, cela est amer, cela pénètre jusqu'à ton cœur.
19 Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
Mes entrailles! mes entrailles! Je sens de la douleur; le dedans de mon cœur, le cœur me bat. Je ne puis me taire! Car, ô mon âme! tu as entendu le son de la trompette, le cri du combat.
20 Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
Ruine sur ruine est annoncée; car tout le pays est détruit; mes tentes sont détruites tout d'un coup, mes pavillons en un moment!
21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
Jusqu'à quand verrai-je l'étendard, entendrai-je le bruit de la trompette?
22 “Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
C'est que mon peuple est insensé. Ils ne me connaissent pas. Ce sont des enfants insensés, dépourvus d'intelligence. Ils sont habiles pour faire le mal; mais ils ne savent pas faire le bien.
23 Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
Je regarde la terre, et voici elle est informe et vide; et les cieux, et leur lumière n'est plus.
24 Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
Je regarde les montagnes, et voici, elles chancellent, et toutes les collines sont ébranlées.
25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
Je regarde, et voici, il n'y a pas un seul homme, et tous les oiseaux des cieux ont fui.
26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
Je regarde, et voici, le Carmel est un désert, et toutes ses villes sont détruites, devant l'Éternel, devant l'ardeur de sa colère.
27 Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
Car ainsi a dit l'Éternel: Tout le pays sera dévasté; quoique je ne fasse pas une destruction entière.
28 Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
A cause de cela, la terre sera dans le deuil, et les cieux en haut seront noirs, parce que je l'ai dit, je l'ai résolu; je n'en reviendrai pas; je ne m'en repentirai point.
29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
Au bruit des cavaliers et des tireurs d'arc toutes les villes prennent la fuite; ils entrent dans les bois, montent sur les rochers; toutes les villes sont abandonnées, il n'y reste plus d'habitants.
30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
Et toi, dévastée, que fais-tu? Quoique tu te revêtes de pourpre, que tu te pares d'ornements d'or, et que tu bordes tes yeux de fard, tu t'embellis en vain: tes amants t'ont méprisée; c'est ta vie qu'ils cherchent.
31 Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”
Car j'entends comme le cri d'une femme en travail, comme l'angoisse d'une femme à son premier enfantement; c'est le cri de la fille de Sion qui soupire, étendant les mains: “Ah! malheur à moi! car mon âme succombe sous les meurtriers! “