< Yeremia 4 >
1 “Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
Si tu revenais, ô Israël, dit le Seigneur, revenais à moi, si tu écartais tes abominations loin de ma face, sans plus errer de côté et d’autre,
2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
et si tu jurais "par l’Eternel vivant", en vérité, en droiture et justice mais les peuples par lui se diraient heureux, et par lui se diraient glorieux!
3 Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
Car c’est ainsi que parle l’Eternel aux gens de Juda et de Jérusalem: "Creusez-vous des sillons, et ne jetez pas vos semences parmi les épines.
4 Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
Tâchez de vous circoncire en l’honneur de l’Eternel et d’enlever les excroissances de votre coeur; sans cela ma colère éclatera comme le feu, et brûlera sans qu’on puisse l’éteindre, à cause de la perversité de vos actes."
5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
Annoncez en Juda, proclamez à Jérusalem et dites: "Qu’on fasse retentir la trompette dans le pays! Criez à plein gosier et dites: "Rassemblez-vous, afin de nous retirer dans les villes fortes!"
6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
Dressez une bannière dans la direction de Sion, fuyez, ne vous arrêtez pas! Car je fais venir du Nord une calamité, une terrible catastrophe.
7 Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
Un lion s’est élancé de son hallier, un destructeur de nations s’est mis en route, quittant sa résidence, pour réduire ton pays en ruine; tes villes deviendront des solitudes inhabitées.
8 Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
C’Est pourquoi ceignez-vous de cilices, exhalez votre douleur, lamentez-vous, puisque le feu de la colère divine ne se détourne pas de nous.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
En ce jour, il arrivera, dit l’Eternel, que le coeur du roi et le coeur des chefs seront éperdus; atterrés seront les prêtres et stupéfaits les prophètes.
10 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
Et je m’écriai: "Eh quoi! Eternel Dieu! Ainsi donc tu aurais complètement leurré ce peuple et Jérusalem, quand tu disais: "Vous obtiendrez la paix!—Et le glaive pénètre jusqu’à l’âme!
11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
En ce temps-là, on dira à ce peuple et à Jérusalem: "II y a un vent embrasé sur les hauteurs dans le désert, venant dans la direction de la fille de mon peuple, mais ne servant ni à vanner ni à épurer le grain.
12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
Un souffle violent m’arrive de là; maintenant je vais, moi aussi, prononcer l’arrêt contre eux.
13 Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
Voici, il s’élance comme les nuages; ses chars ressemblent à l’ouragan, ses chevaux sont plus rapides que les aigles. Malheur à nous! Car nous sommes, saccagés.
14 Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
O Jérusalem, lave ton coeur de toute perversité pour être sauvée: jusqu’à quand logeras-tu dans ton sein tes pensées criminelles?
15 Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
Car une voix se fait entendre de Dan et annonce la calamité depuis la montagne d’Ephraïm.
16 “Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
"Faites-le savoir aux nations, allons, apprenez-le à Jérusalem, que des assiégeants arrivent d’un pays lointain et poussent des clameurs contre les villes de Juda!"
17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
Comme les gardiens des champs, ils l’enserrent de tous côtés, parce qu’elle s’est révoltée contre moi, dit l’Eternel.
18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
C’Est ta conduite, ce sont tes actes qui t’ont valu cela; de là ton malheur, qui est si amer, car il t’atteint jusqu’au coeur.
19 Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
O mes entrailles, mes entrailles! Je frémis jusqu’au fond de mon coeur! Tout mon coeur est en émoi, je ne puis le calmer; car tu entends, ô mon âme, le son de la trompette. Les fanfares belliqueuses.
20 Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
On annonce désastres sur désastres, que tout le pays est saccagé; mes tentes ont été saccagées soudainement, mes pavillons en un clin d’oeil.
21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
Jusqu’à quand verrai-je des bannières? Entendrai-je les trompettes retentissantes?
22 “Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
Certes, mon peuple est dénué de raison, ils ne me connaissent pas; ce sont des enfants insensés, sans aucun discernement, intelligents seulement pour mal faire, incapables de faire le bien.
23 Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
J’Ai regardé la terre, et voici tout y était chaos informe; et vers les cieuxleur lumière avait disparu.
24 Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
J’Ai regardé les montagnes, elles étaient tremblantes; toutes les collineselles étaient violemment agitées.
25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
J’Ai regardé et voici, il n’y avait plus d’hommes, et tous les oiseaux du ciel avaient pris leur vol.
26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
J’Ai regardé et voici, la campagne fertile était devenue un désert, et toutes ses villes étaient renversées par l’action de l’Eternel, par le feu de sa colère.
27 Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
Oui, ainsi parle l’Eternel: "Tout le pays deviendra une solitude, bien que je ne consomme pas la ruine."
28 Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
C’Est pour cette raison que la terre est en deuil, et les cieux là-haut sont ténébreux, parce que j’ai annoncé ce que j’ai résolu et que je n’entends ni me raviser ni me rétracter.
29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
Devant la clameur des cavaliers et des archers, toute la ville est en fuite; on pénètre dans les fourrés, on escalade les rochers; toute ville est abandonnée, pas un homme n’y reste.
30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
Et toi, si complètement ruinée, que vas-tu faire? Tu aurais beau te vêtir de pourpre, te parer de tes bijoux d’or, allonger tes yeux au moyen du fard: vainement tu te ferais belle, les amoureux te dédaignent, c’est à ta vie qu’ils en veulent.
31 Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”
Car j’entends des plaintes comme celles d’une femme en travail, des cris d’angoisse comme ceux d’une mère mettant au monde son premier-né: c’est la voix de Sion qui exhale des soupirs, qui se tord les bras: "Malheur à moi, mon âme est à bout de force devant les meurtriers!"