< Yeremia 4 >

1 “Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
if to return: return Israel utterance LORD to(wards) me to return: return and if to turn aside: remove abomination your from face my and not to wander
2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
and to swear alive LORD in/on/with truth: true in/on/with justice and in/on/with righteousness and to bless in/on/with him nation and in/on/with him to boast: boast
3 Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
for thus to say LORD to/for man Judah and to/for Jerusalem to break to/for you fallow ground and not to sow to(wards) thorn
4 Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
to circumcise to/for LORD and to turn aside: remove foreskin heart your man Judah and to dwell Jerusalem lest to come out: issue like/as fire rage my and to burn: burn and nothing to quench from face: because evil deed your
5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
to tell in/on/with Judah and in/on/with Jerusalem to hear: proclaim and to say (to blow *Q(K)*) trumpet in/on/with land: country/planet to call: call out to fill and to say to gather and to come (in): come to(wards) city [the] fortification
6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
to lift: raise ensign Zion [to] to seek refuge not to stand: stand for distress: harm I to come (in): bring from north and breaking great: large
7 Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
to ascend: rise lion from thicket his and to ruin nation to set out to come out: come from place his to/for to set: make land: country/planet your to/for horror: destroyed city your to desolate from nothing to dwell
8 Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
upon this to gird sackcloth to mourn and to wail for not to return: turn back burning anger face: anger LORD from us
9 “Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
and to be in/on/with day [the] he/she/it utterance LORD to perish heart [the] king and heart [the] ruler and be desolate: appalled [the] priest and [the] prophet to astounded
10 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
and to say alas! Lord YHWH/God surely to deceive to deceive to/for people [the] this and to/for Jerusalem to/for to say peace: well-being to be to/for you and to touch sword till [the] soul: life
11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
in/on/with time [the] he/she/it to say to/for people [the] this and to/for Jerusalem spirit: breath dazzling bareness in/on/with wilderness way: direction daughter people my not to/for to scatter and not to/for to purify
12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
spirit: breath full from these to come (in): come to/for me now also I to speak: speak justice: judgement with them
13 Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
behold like/as cloud to ascend: rise and like/as whirlwind chariot his to lighten from eagle horse his woe! to/for us for to ruin
14 Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
to wash from distress: evil heart your Jerusalem because to save till how to lodge in/on/with entrails: among your plot evil: wickedness your
15 Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
for voice to tell from Dan and to hear: proclaim evil: trouble from mountain: mount (Mount) Ephraim
16 “Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
to remember to/for nation behold to hear: proclaim upon Jerusalem to watch to come (in): come from land: country/planet [the] distance and to give: cry out upon city Judah voice their
17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
like/as to keep: guard field to be upon her from around for [obj] me to rebel utterance LORD
18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
way: conduct your and deed your to make: do these to/for you this distress: harm your for to provoke for to touch till heart your
19 Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
belly my belly my (to wait: wait *Q(K)*) wall heart my to roar to/for me heart my not be quiet for voice: sound trumpet (to hear: hear *Q(K)*) soul: myself my shout battle
20 Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
breaking upon breaking to call: call out for to ruin all [the] land: country/planet suddenly to ruin tent my moment curtain my
21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
till how to see: see ensign to hear: hear voice: sound trumpet
22 “Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
for fool(ish) people my [obj] me not to know son: child fool they(masc.) and not to understand they(masc.) wise they(masc.) to/for be evil and to/for be good not to know
23 Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
to see: see [obj] [the] land: country/planet and behold formlessness and void and to(wards) [the] heaven and nothing light their
24 Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
to see: see [the] mountain: mount and behold to shake and all [the] hill to lighten
25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
to see: see and behold nothing [the] man and all bird [the] heaven to wander
26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
to see: see and behold [the] plantation [the] wilderness and all city his to tear from face: before LORD from face: before burning anger face: anger his
27 Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
for thus to say LORD devastation to be all [the] land: country/planet and consumption not to make
28 Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
upon this to mourn [the] land: country/planet and be dark [the] heaven from above upon for to speak: speak to plan and not to be sorry: relent and not to return: repent from her
29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
from voice: sound horseman and to shoot bow to flee all [the] city to come (in): come in/on/with cloud and in/on/with rock to ascend: rise all [the] city to leave: forsake and nothing to dwell in/on/with them man: anyone
30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
(and you(f. s.) *Q(K)*) to ruin what? to make: do for to clothe scarlet for to adorn ornament gold for to tear in/on/with color eye your to/for vanity: vain be beautiful to reject in/on/with you to lust soul: life your to seek
31 Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”
for voice like/as be weak: grieved to hear: hear distress like/as to be/bear firstborn voice daughter Zion to breathe to spread palm her woe! please to/for me for be faint soul: myself my to/for to kill

< Yeremia 4 >