< Yeremia 4 >

1 “Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli, nirudie mimi,” asema Bwana. “Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu na usiendelee kutangatanga,
Budeš-li se míti navrátiti, Izraeli, dí Hospodin, ke mně se navrať. Nebo odejmeš-li ohavnosti své od tváři mé a nebudeš-li se toulati,
2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa, ‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’ ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye na katika yeye watajitukuza.”
A budeš-li přisahati právě, náležitě a spravedlivě, říkaje: Živť jest Hospodin, tedy požehnání dávati sobě v něm budou národové, a v něm se chlubiti.
3 Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu: “Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu, wala msipande katikati ya miiba.
Nebo takto praví Hospodin mužům Judským a Jeruzalémským: Zořte sobě ouhor, a nerozsívejte do trní.
4 Jitahirini katika Bwana, tahirini mioyo yenu, enyi wanaume wa Yuda na watu wa Yerusalemu, la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu na kuwaka kama moto kwa sababu ya uovu mliotenda, ikiwaka pasipo wa kuizima.
Obřežte se Hospodinu, a odejměte neobřízky srdce vašeho, muži Judští a obyvatelé Jeruzalémští, aby nevyšla jako oheň prchlivost má, a nehořela, tak že by nebyl kdo uhasiti, pro nešlechetnost předsevzetí vašich.
5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema: ‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’ Piga kelele na kusema: ‘Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie katika miji yenye maboma!’
Oznamte v Judstvu, a v Jeruzalémě ohlaste, a rcete: Trubte trubou v zemi, svolejte a sbeřte lid, a rcete: Shromažďte se, a vejděme do měst hrazených.
6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni! Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa! Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini, maangamizi ya kutisha.”
Vyzdvihněte korouhev na Sionu, zmužile se mějte, nepostávejte; nebo já zlé věci uvedu od půlnoci, a potření veliké.
7 Simba ametoka nje ya pango lake, mharabu wa mataifa amejipanga. Ametoka mahali pake ili aangamize nchi yenu. Miji yenu itakuwa magofu pasipo mtu wa kuishi humo.
Vychází lev z houště své, a ten, kterýž hubí národy, vyšed z místa svého, táhne, aby obrátil zemi tvou v pustinu, a města tvá aby zbořena byla, tak aby nebylo žádného obyvatele.
8 Hivyo vaeni nguo za magunia, ombolezeni na kulia kwa huzuni, kwa kuwa hasira kali ya Bwana haijaondolewa kwetu.
Protož přepašte se žíněmi, kvělte a naříkejte; nebo není odvrácen hněv prchlivosti Hospodinovy od nás.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana “mfalme na maafisa watakata tamaa, makuhani watafadhaika, na manabii watashangazwa mno.”
Stane se zajisté v ten den, dí Hospodin, že zhyne srdce královo a srdce knížat, užasnou se i kněží, a proroci diviti se budou.
10 Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”
I řekl jsem: Ach, Panovníče Hospodine, jistě že jsi velice podvedl lid tento, i Jeruzalém, říkaje: Pokoj míti budete, a však pronikl meč až k duši.
11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,
V ten čas řečeno bude lidu tomuto i Jeruzalému: Vítr tuhý z míst vysokých na poušti jde upřímo na lid můj, ne aby převíval, ani přečišťoval.
12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”
Vítr silnější než oni přijde mi, nyní já také vypovím jim úsudky.
13 Tazama! Anakuja kama mawingu, magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli, farasi wake wana mbio kuliko tai. Ole wetu! Tunaangamia!
Aj, jako oblakové vystupuje, a jako vicher vozové jeho, rychlejší jsou nežli orlice koni jeho. Běda nám, nebo popléněni jsme.
14 Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe. Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?
Obmej od nešlechetnosti srdce své, Jeruzaléme, abys vysvobozen byl. Dokudž zůstávati budou u prostřed tebe myšlení marnosti tvé?
15 Sauti inatangaza kutoka Dani, ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.
Nebo hlas oznamujícího přichází od Dan, a toho, kterýž ohlašuje nepravost, s hory Efraim.
16 “Waambie mataifa jambo hili, piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu: ‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali, likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.
Připomínejte těmto národům, aj, ohlašujte Jeruzalémským, že strážní táhnou z země daleké, a vydávají proti městům Judským hlas svůj.
17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba, kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’” asema Bwana.
Jako ti, kteříž hlídají polí, položí se proti němu vůkol; nebo jest mi odporný, dí Hospodin.
18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe yameleta haya juu yako. Hii ndiyo adhabu yako. Tazama jinsi ilivyo chungu! Tazama jinsi inavyochoma moyo!”
Cesta tvá a skutkové tvoji to způsobili tobě; toť nešlechetnost tvá, žeť to hořké jest, a že dosahá až do srdce tvého.
19 Ee mtima wangu, mtima wangu! Ninagaagaa kwa maumivu. Ee maumivu makuu ya moyo wangu! Moyo wangu umefadhaika ndani yangu, siwezi kunyamaza. Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta, nimesikia kelele ya vita.
Ó, střeva má, střeva má, bolest trpím, ó osrdí mé, kormoutí se ve mně srdce mé, nemohuť mlčeti. Nebo hlas trouby slyšíš, duše má, a prokřikování vojenské.
20 Maafa baada ya maafa, nchi yote imekuwa magofu. Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa, makazi yangu kwa muda mfupi.
Potření za potřením provolává se, popléněna zajisté bude všecka země, náhle popléněni budou stanové moji, v okamžení kortýny mé.
21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita na kusikia sauti za tarumbeta?
Až dokud vídati budu korouhev, slýchati hlas trouby?
22 “Watu wangu ni wapumbavu, hawanijui mimi. Ni watoto wasio na akili, hawana ufahamu. Ni hodari kutenda mabaya, hawajui kutenda yaliyo mema.”
Nebo bláznivý lid můj nezná mne, synové nemoudří a nerozumní jsou. Moudří jsou k činění zlého, ale činiti dobře neumějí.
23 Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
Hledím-li na zemi, a aj, nesličná jest a prázdná; pakli na nebe, není na něm žádného světla.
24 Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
Hledím-li na hory, a aj, třesou se, a všickni pahrbkové pohybují se.
25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
Hledím-li, a aj, není žádného člověka, a všeliké ptactvo nebeské zaletělo.
26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
Hledím-li, a aj, pole úrodné jest pouští, a všecka města jeho zbořena jsou od Hospodina a od hněvu prchlivosti jeho.
27 Hivi ndivyo Bwana asemavyo: “Nchi yote itaharibiwa, ingawa sitaiangamiza kabisa.
Nebo takto praví Hospodin: Spustne všecka země, a však konce ještě neučiním.
28 Kwa hiyo dunia itaomboleza na mbingu zilizo juu zitakuwa giza, kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma, nimeamua na wala sitageuka.”
Kvíliti bude nad tím země, a zasmuší se na hoře nebe, proto že jsem mluvil, co jsem myslil, a nelituji, aniž se odvrátím od toho.
29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde kila mji unakimbia. Baadhi wanakimbilia vichakani, baadhi wanapanda juu ya miamba. Miji yote imeachwa, hakuna aishiye ndani yake.
Před hřmotem jezdců a těch, kteříž střílejí z lučiště, uteče všecko město. Vejdou do hustých oblaků, a na skálí vylezou; všecka města opuštěna budou, a žádný nebude bydliti v nich.
30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa? Kwa nini unajivika vazi jekundu na kuvaa vito vya dhahabu? Kwa nini unapaka macho yako rangi? Unajipamba bure. Wapenzi wako wanakudharau, wanautafuta uhai wako.
Ty pak pohubena jsuc, což činiti budeš? Ačkoli obláčíš se v šarlat, ačkoli se ozdobuješ ozdobou zlatou, ačkoli líčíš tvář svou líčidlem, darmo se okrašluješ. Pohrdají tebou frejíři, bezživotí tvého hledají.
31 Nasikia kilio kama cha mwanamke katika utungu wa kuzaa, kilio cha uchungu kama cha anayemzaa mtoto wake wa kwanza: kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua, akiinua mikono yake, akisema, “Ole wangu! Ninazimia; maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”
Nebo slyším hlas jako rodičky, svírání jako té, kteráž po nejprvé ku porodu pracuje, hlas dcery Sionské, ustavičně vzdychající, a lomící rukama svýma, říkající: Běda mně nyní, nebo ustala duše má pro vrahy.

< Yeremia 4 >