< Yeremia 39 >

1 Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
Yahuda Kralı Sidkiya'nın dokuzuncu yılının onuncu ayında Babil Kralı Nebukadnessar bütün ordusuyla Yeruşalim önlerine gelerek kenti kuşattı.
2 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
Sidkiya'nın krallığının on birinci yılında, dördüncü ayın dokuzuncu günü kent surlarında gedik açıldı.
3 Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
Yeruşalim ele geçirilince Babil Kralı'nın bütün komutanları –Samgarlı Nergal-Sareser, askeri danışman Nebo-Sarsekim, baş görevli Nergal-Sareser ve bütün öteki görevliler– içeri girip Orta Kapı'da oturdular.
4 Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
Yahuda Kralı Sidkiya'yla askerler onları görünce kaçtılar. Gece kral bahçesinin yolundan iki duvarın arasındaki kapıdan kaçarak Arava yoluna çıktılar.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
Ama artlarına düşen Kildani ordusu Eriha ovalarında Sidkiya'ya yetişti, onu yakalayıp Hama topraklarında, Rivla'da Babil Kralı Nebukadnessar'ın huzuruna çıkardılar. Nebukadnessar onun hakkında karar verdi:
6 Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
Rivla'da Sidkiya'nın gözü önünde oğullarını, sonra da bütün Yahuda ileri gelenlerini öldürttü.
7 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
Sidkiya'nın gözlerini oydu, zincire vurup Babil'e götürdü.
8 Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
Kildaniler sarayla halkın evlerini ateşe verdiler, Yeruşalim surlarını yıktılar.
9 Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
Komutan Nebuzaradan kentte sağ kalanları, kendi safına geçen kaçakları ve geri kalan halkı Babil'e sürgün etti.
10 Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
Ancak hiçbir şeyi olmayan bazı yoksulları Yahuda'da bıraktı, onlara bağ ve tarla verdi.
11 Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
Babil Kralı Nebukadnessar, muhafız birliği komutanı Nebuzaradan aracılığıyla Yeremya'yla ilgili şu buyruğu verdi:
12 “Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
“Onu sorumluluğun altına al, ona iyi bak, hiç zarar verme, senden ne dilerse yap.”
13 Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
Bunun üzerine muhafız birliği komutanı Nebuzaradan, askeri danışman Nebuşazban, baş görevli Nergal-Sareser ve Babil Kralı'nın öbür görevlileri
14 wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
adam gönderip Yeremya'yı muhafız avlusundan getirttiler. Evine geri götürmesi için Şafan oğlu Ahikam oğlu Gedalya'nın koruyuculuğuna verdiler. Böylece Yeremya halkı arasında yaşamını sürdürdü.
15 Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
Yeremya daha muhafız avlusunda tutukluyken RAB ona şöyle seslenmişti:
16 “Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
“Git, Kûşlu Ebet-Melek'e de ki, ‘İsrail'in Tanrısı, Her Şeye Egemen RAB şöyle diyor: Bu kent üzerine yarar değil, zarar verecek sözlerimi yerine getirmek üzereyim. O gün olanları sen de göreceksin.
17 Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
Ama o gün seni kurtaracağım diyor RAB. Korktuğun adamların eline teslim edilmeyeceksin.
18 Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”
Seni kesinlikle kurtaracağım, kılıçla öldürülmeyeceksin. Hiç değilse canını kurtarmış olacaksın. Çünkü bana güvendin, diyor RAB.’”

< Yeremia 39 >