< Yeremia 39 >

1 Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
Devete godine Sedekije cara Judina mjeseca desetoga doðe Navuhodonosor car Vavilonski sa svom vojskom svojom na Jerusalim i stade ga biti.
2 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
Jedanaeste godine Sedekijine mjeseca èetvrtoga, devetoga dana toga mjeseca provališe u grad.
3 Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
I uðoše svi knezovi cara Vavilonskoga, i stadoše kod srednjih vrata Nergal-sareser, Samgar-nevon, Sarsehim, starješina nad dvoranima, Nergal-sareser, starješina nad vraèima, i svi drugi knezovi cara Vavilonskoga.
4 Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
A kad ih vidje Sedekija car Judin i svi vojnici, pobjegoše i izidoše noæu iz grada pokraj vrta carskoga na vrata meðu dva zida; i iðahu preko polja.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
A vojska Haldejska gonjaše ih, i stiže Sedekiju u polju Jerihonskom, i uhvativši ga dovedoše ga k Navuhodonosoru caru Vavilonskom u Rivlu u zemlji Ematskoj, te mu sudi.
6 Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
I zakla car Vavilonski sinove Sedekijine u Rivli na njegove oèi, i sve znatne ljude od Jude pokla car Vavilonski.
7 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
Iza toga Sedekiji iskopa oèi, i sveza ga u dvoje verige mjedene, da ga odvede u Vavilon.
8 Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
A dom carev i domove narodne popališe Haldejci ognjem, i zidove Jerusalimske raskopaše.
9 Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
A ostatak naroda što osta u gradu i prebjege koji prebjegoše k njemu, ostatak naroda što bješe ostao, odvede Nevuzardan zapovjednik stražarski u Vavilon.
10 Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
Samo najsiromašnije iz naroda, koji ništa nemahu, ostavi Nevuzardan zapovjednik stražarski u zemlji Judinoj, i dade im tada vinograde i njive.
11 Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
A Navuhodonosor car Vavilonski zapovjedi za Jeremiju Nevuzardanu zapovjedniku stražarskom govoreæi:
12 “Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
Uzmi ga i gledaj ga dobro, i ne èini mu zla, nego mu èini što ti god kaže.
13 Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
I poslaše Nevuzardan zapovjednik stražarski i Nevusazvan, starješina nad dvoranima, i Nergal-sareser, starješina nad vraèima, i svi knezovi cara Vavilonskoga,
14 wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
Poslaše, te uzeše Jeremiju iz trijema od tamnice, i predaše ga Godoliji sinu Ahikama sina Safanova da ga odvede kuæi; tako osta meðu narodom.
15 Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
A Jeremiji doðe rijeè Gospodnja kad bješe zatvoren u trijemu od tamnice govoreæi:
16 “Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
Idi i reci Avdemelehu Etiopljaninu govoreæi: ovako veli Gospod nad vojskama Bog Izrailjev: evo ja æu uèiniti da se zbudu rijeèi moje tome gradu na zlo a ne na dobro, i navršiæe se pred tobom u onaj dan.
17 Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
Ali æu tebe izbaviti u onaj dan, govori Gospod, i neæeš biti predan u ruke ljudima kojih se bojiš.
18 Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”
Jer æu te doista saèuvati, te neæeš pasti od maèa, i biæe ti duša tvoja mjesto plijena zato što si se pouzdao u me, govori Gospod.

< Yeremia 39 >