< Yeremia 39 >

1 Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
La neuvième année de Sédécias, roi de Juda, au dixième mois, Nebucadnetsar, roi de Babylone, et toute son armée vinrent contre Jérusalem et l'assiégèrent.
2 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
La onzième année de Sédécias, le quatrième mois, le neuvième jour du mois, une brèche fut ouverte dans la ville.
3 Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
Tous les princes du roi de Babylone entrèrent et s'assirent à la porte du milieu: Nergal Sharezer, Samgarnebo, Sarsechim, le Rabsaris, Nergal Sharezer, le Rabmag, et tous les autres princes du roi de Babylone.
4 Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
Lorsque Sédécias, roi de Juda, et tous les hommes de guerre les virent, ils s'enfuirent et sortirent de nuit de la ville, par le chemin du jardin du roi, par la porte entre les deux murs.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
Mais l'armée des Chaldéens les poursuivit et rattrapa Sédécias dans les plaines de Jéricho. Après l'avoir pris, ils le firent monter devant Nebucadnetsar, roi de Babylone, à Ribla, dans le pays de Hamath, et il prononça un jugement contre lui.
6 Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
Alors le roi de Babylone tua sous ses yeux les fils de Sédécias à Ribla. Le roi de Babylone tua aussi tous les nobles de Juda.
7 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
Il fit crever les yeux à Sédécias et le lia avec des chaînes, pour le transporter à Babylone.
8 Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
Les Chaldéens incendièrent la maison du roi et les maisons du peuple et démolirent les murailles de Jérusalem.
9 Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
Alors Nebuzaradan, chef des gardes, emmena captifs à Babylone le reste du peuple qui était resté dans la ville, les déserteurs qui s'étaient ralliés à lui, et le reste du peuple qui était resté.
10 Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
Mais Nebuzaradan, chef des gardes, laissa dans le pays de Juda les pauvres du peuple, qui n'avaient rien, et leur donna en même temps des vignes et des champs.
11 Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
Nebucadnetsar, roi de Babylone, donna cet ordre à Nebuzaradan, chef des gardes, au sujet de Jérémie:
12 “Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
« Prends-le et occupe-toi de lui. Ne lui fais pas de mal, mais fais-lui ce qu'il te dira. »
13 Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
Alors Nebuzaradan, chef des gardes, Nebushazban, Rabsaris, Nergal Sharezer, Rabmag, et tous les officiers supérieurs du roi de Babylone
14 wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
envoyèrent chercher Jérémie dans la cour des gardes, et le confièrent à Guedalia, fils d'Ahikam, fils de Shaphan, pour qu'il le ramène chez lui. Il vécut ainsi parmi le peuple.
15 Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
La parole de Yahvé fut adressée à Jérémie, pendant qu'il était enfermé dans la cour des gardes, en ces termes:
16 “Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
Va, et dis à Ebed Melech, l'Éthiopien, que Yahvé des armées, le Dieu d'Israël, dit: « Voici, je ferai venir sur cette ville mes paroles en mal et non en bien, et elles s'accompliront devant toi en ce jour-là.
17 Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
Mais je te délivrerai en ce jour-là, dit l'Éternel, et tu ne seras pas livré entre les mains des hommes dont tu as peur.
18 Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”
Car je te sauverai. Tu ne tomberas pas par l'épée, mais tu t'échapperas avec ta vie, parce que tu as mis ta confiance en moi, dit Yahvé.'"

< Yeremia 39 >