< Yeremia 39 >

1 Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
in/on/with year [the] ninth to/for Zedekiah king Judah in/on/with month [the] tenth to come (in): come Nebuchadnezzar king Babylon and all strength: soldiers his to(wards) Jerusalem and to confine upon her
2 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
in/on/with eleven ten year to/for Zedekiah in/on/with month [the] fourth in/on/with nine to/for month to break up/open [the] city
3 Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
and to come (in): come all ruler king Babylon and to dwell in/on/with gate [the] midst Nergal-sar-ezer Nergal-sar-ezer Nergal-sar-ezer Samgar, Nebu-sar-sekim Samgar, Nebu-sar-sekim Samgar, Nebu-sar-sekim Samgar, Nebu-sar-sekim Rab-saris Rab-saris Nergal-sar-ezer Nergal-sar-ezer Nergal-sar-ezer Rab-mag Rab-mag and all remnant ruler king Babylon
4 Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
and to be like/as as which to see: see them Zedekiah king Judah and all human [the] battle and to flee and to come out: come night from [the] city way: road garden [the] king in/on/with gate between [the] wall and to come out: come way: road [the] Arabah
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
and to pursue strength: soldiers Chaldea after them and to overtake [obj] Zedekiah in/on/with plain Jericho and to take: take [obj] him and to ascend: establish him to(wards) Nebuchadnezzar king Babylon Riblah [to] in/on/with land: country/planet Hamath and to speak: promise with him justice: judgement
6 Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
and to slaughter king Babylon [obj] son: child Zedekiah in/on/with Riblah to/for eye his and [obj] all noble Judah to slaughter king Babylon
7 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
and [obj] eye Zedekiah to blind and to bind him in/on/with bronze to/for to come (in): bring [obj] him Babylon [to]
8 Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
and [obj] house: palace [the] king and [obj] house: home [the] people to burn [the] Chaldea in/on/with fire and [obj] wall Jerusalem to tear
9 Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
and [obj] remainder [the] people [the] to remain in/on/with city and [obj] [the] to fall: fall which to fall: deserting upon him and [obj] remainder [the] people [the] to remain to reveal: remove Nebuzaradan Nebuzaradan chief guard Babylon
10 Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
and from [the] people [the] poor which nothing to/for them anything to remain Nebuzaradan chief guard in/on/with land: country/planet Judah and to give: give to/for them vineyard and field in/on/with day [the] he/she/it
11 Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
and to command Nebuchadnezzar king Babylon upon Jeremiah in/on/with hand: by Nebuzaradan chief guard to/for to say
12 “Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
to take: take him and eye your to set: make upon him and not to make: do to/for him anything bad: evil for (if: except *Q(K)*) like/as as which to speak: speak to(wards) you so to make: do with him
13 Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
and to send: depart Nebuzaradan chief guard and Nebushazban Rab-saris Rab-saris and Nergal-sar-ezer Nergal-sar-ezer Nergal-sar-ezer Rab-mag Rab-mag and all chief king Babylon
14 wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
and to send: depart and to take: take [obj] Jeremiah from court [the] guardhouse and to give: give [obj] him to(wards) Gedaliah son: child Ahikam son: child Shaphan to/for to come out: send him to(wards) [the] house: home and to dwell in/on/with midst [the] people
15 Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
and to(wards) Jeremiah to be word LORD in/on/with to be he to restrain in/on/with court [the] guardhouse to/for to say
16 “Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
to go: went and to say to/for Ebed-melech Ebed-melech [the] Ethiopian to/for to say thus to say LORD Hosts God Israel look! I (to come (in): fulfill *Q(k)*) [obj] word my to(wards) [the] city [the] this to/for distress: harm and not to/for welfare and to be to/for face: before your in/on/with day [the] he/she/it
17 Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
and to rescue you in/on/with day [the] he/she/it utterance LORD and not to give: give in/on/with hand: power [the] human which you(m. s.) fearing from face of their
18 Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”
for to escape to escape you and in/on/with sword not to fall: kill and to be to/for you soul: life your to/for spoil for to trust in/on/with me utterance LORD

< Yeremia 39 >