< Yeremia 39 >

1 Hivi ndivyo Yerusalemu ilivyotwaliwa: Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Mfalme Sedekia wa Yuda, katika mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu na akauzunguka mji.
Efter at Jerusalem var indtaget — i Kong Zedekias af Judas niende Regeringsaar i den tiende Maaned, kom Kong Nebukadrezar af Babel med hele sin Hær til Jerusalem og belejrede det;
2 Katika siku ya tisa ya mwezi wa nne wa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia, ukuta wa mji ulibomolewa.
i Zedekias's ellevte Aar paa den niende Dag i den fjerde Maaned blev Byen stormet —
3 Kisha maafisa wote wa mfalme wa Babeli wakaja na kuketi kwenye Lango la Kati, nao ni: Nergal-Shareza wa Samgari, Nebo-Sarsekimu afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa mwenye cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli.
da kom alle Babels Konges Fyrster og satte sig i Midterporten: Overhofmanden Nebusjazban, Magernes Øverste Nergal-Sar'ezer og alle Babels Konges andre Fyrster.
4 Mfalme Sedekia wa Yuda na askari wote walipowaona, wakakimbia na kuondoka mjini usiku kwa njia ya bustani ya mfalme, kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili, wakaelekea Araba.
Da Kong Zedekias af Juda og alle hans Krigsmænd saa dem, flygtede de om Natten fra Byen ad Vejen til Kongens Have gennem Porten mellem de to Mure og tog Vejen ad Araba til.
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia na kumpata Sedekia katika sehemu tambarare za Yeriko. Wakamkamata na kumpeleka kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu.
Men Kaldæernes Hær satte efter dem og indhentede Zedekias paa Jerikos Lavslette; og de tog ham med og bragte ham op til Kong Nebukadnezar af Babel i Ribla i Hamats Land; og han fældede hans Dom.
6 Huko Ribla, mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake, na pia akawaua wakuu wote wa Yuda.
Babels Konge lod i Ribla Zedekias's Sønner dræbe i hans Paasyn; ogsaa alle de ypperste i Juda lod Babels Konge dræbe;
7 Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia na kumfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
derpaa lod han Øjnene stikke ud paa Zedekias og lod ham lægge i Kobberlænker for at føre ham til Babel.
8 Jeshi la Wakaldayo likachoma moto jumba la kifalme na nyumba za watu, na kuzibomoa kuta za Yerusalemu.
Kaldæerne satte Ild paa Kongens Palads og Folkets Huse og nedbrød Jerusalems Mure.
9 Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akawachukua na kuwapeleka uhamishoni Babeli watu waliokuwa wamebaki ndani ya mji, pamoja na wale waliokuwa wamejisalimisha kwake, na watu wengine wote.
Resten af Folket, der var levnet i Byen, Overløberne, der var løbet over til ham, og Resten af Haandværkerne førte Livvagtsøversten Nebuzar'adan som Fanger til Babel,
10 Lakini Nebuzaradani kiongozi wa walinzi aliwabakiza baadhi ya watu maskini katika nchi ya Yuda, ambao hawakuwa na kitu. Naye wakati huo akawapa mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.
og kun nogle af den fattigste Befolkning, der intet ejede, lod Livvagtsøversten Nebuzar'adan blive tilbage i Judas Land, idet han samtidig gav dem Vingaarde og Agre.
11 Basi, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa ametoa maagizo kuhusu Yeremia kupitia Nebuzaradani kiongozi wa walinzi wa mfalme akisema:
Men om Jeremias bød Kong Nebukadrezar af Babel Livvagtsøversten Nebuzar'adan:
12 “Mchukue umtunze. Usimdhuru, lakini umfanyie chochote anachotaka.”
»Tag ham og hav Øje med ham og gør ham ingen Men; gør med ham, som han selv ønsker!«
13 Basi Nebuzaradani kiongozi wa walinzi, Nebushazbani afisa mkuu, Nergal-Shareza afisa wa cheo cha juu, na maafisa wengine wote wa mfalme wa Babeli
Saa sendte Livvagtsøversten Nebuzar'adan, Overhofmanden Nebusjazban og Magernes Øverste Nergal-Sar'ezer og alle Babels Konges andre Stormænd
14 wakatuma watu kumwondoa Yeremia kutoka ua wa walinzi. Wakamkabidhi kwa Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani, ili amrudishe nyumbani kwake. Kwa hiyo akabaki miongoni mwa watu wake mwenyewe.
Bud og lod Jeremias hente i Vagtforgaarden og overgav ham til Gedalja, en Søn af Sjafans Søn Ahikam, for at han skulde føre ham til hans Hjem; og han boede iblandt Folket.
15 Wakati Yeremia alipokuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia kusema:
Medens Jeremias sad fængslet i Vagtforgaarden, kom HERRENS Ord til ham saaledes:
16 “Nenda ukamwambie Ebed-Meleki Mkushi, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Ninakaribia kutimiza maneno yangu dhidi ya mji huu kwa njia ya maafa, wala si kwa kuwafanikisha. Wakati huo hayo yatatimizwa mbele ya macho yako.
Gaa hen og sig til Ætioperen Ebed-Melek: Saa siger Hærskarers HERRE, Israels Gud: Se, jeg lader mine Ord gaa i Opfyldelse paa denne By til Ulykke og ikke til Lykke, og du skal have dem i Tankerne paa hin Dag.
17 Lakini siku hiyo nitakuokoa, asema Bwana; hutatiwa mikononi mwa wale unaowaogopa.
Men paa hin Dag redder jeg dig, lyder det fra HERREN, og du skal ikke gives i de Mænds Haand, for hvem du frygter;
18 Nitakuokoa; hutaanguka kwa upanga, lakini maisha yako yatakuwa salama, kwa sababu unanitumaini, asema Bwana.’”
thi jeg vil frelse dig, saa du ikke falder for Sværdet, og du skal vinde dit Liv som Bytte, fordi du stolede paa mig, lyder det fra HERREN.

< Yeremia 39 >