< Yeremia 38 >
1 Shefatia mwana wa Matani, na Gedalia mwana wa Pashuri, na Yehukali mwana wa Shelemia, na Pashuri mwana wa Malkiya wakasikia kile Yeremia alichokuwa akiwaambia watu wote wakati aliposema,
and to hear: hear Shephatiah son: child Mattan and Gedaliah son: child Pashhur and Jucal son: child Shelemiah and Pashhur son: child Malchiah [obj] [the] word which Jeremiah to speak: speak to(wards) all [the] people to/for to say
2 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Yeyote akaaye ndani ya mji huu atakufa kwa upanga, njaa au tauni, lakini yeyote atakayejisalimisha kwa Wakaldayo ataishi. Atakayeyatoa maisha yake kama nyara, ataishi.’
thus to say LORD [the] to dwell in/on/with city [the] this to die in/on/with sword in/on/with famine and in/on/with pestilence and [the] to come out: come to(wards) [the] Chaldea (and to live *Q(K)*) and to be to/for him soul: life his to/for spoil and to live
3 Tena hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mji huu kwa hakika utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli, ambaye atauteka.’”
thus to say LORD to give: give to give: give [the] city [the] this in/on/with hand: power strength: soldiers king Babylon and to capture her
4 Ndipo maafisa wakamwambia mfalme, “Mtu huyu imempasa kuuawa. Anawakatisha tamaa askari waliobaki katika mji huu, vivyo hivyo na watu wote pia, kwa ajili ya mambo anayowaambia. Mtu huyu hawatakii mema watu hawa, bali maangamizi yao.”
and to say [the] ruler to(wards) [the] king to die please [obj] [the] man [the] this for as that: since as as he/she/it to slacken [obj] hand human [the] battle [the] to remain in/on/with city [the] this and [obj] hand all [the] people to/for to speak: speak to(wards) them like/as word [the] these for [the] man [the] this nothing he to seek to/for peace: well-being to/for people [the] this that if: except if: except to/for distress: harm
5 Mfalme Sedekia akajibu, “Yeye yuko mikononi mwenu! Mfalme hawezi kufanya lolote kuwapinga ninyi.”
and to say [the] king Zedekiah behold he/she/it in/on/with hand your for nothing [the] king be able [obj] you word: thing
6 Basi wakamchukua Yeremia na kumtia kwenye kisima cha Malkiya, mwana wa mfalme, kilichokuwa katika ua wa walinzi. Wakamteremsha Yeremia kwa kamba ndani ya kisima. Hakikuwa na maji ndani yake, ila tope tu, naye Yeremia akazama ndani ya matope.
and to take: take [obj] Jeremiah and to throw [obj] him to(wards) [the] pit Malchiah son: child [the] `the king` which in/on/with court [the] guardhouse and to send: depart [obj] Jeremiah in/on/with cord and in/on/with pit nothing water that if: except if: except mud and to sink Jeremiah in/on/with mud
7 Lakini Ebed-Meleki Mkushi, aliyekuwa afisa katika jumba la kifalme, akasikia kuwa walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya kisima. Wakati mfalme alipokuwa ameketi katika Lango la Benyamini,
and to hear: hear Ebed-melech Ebed-melech [the] Ethiopian man eunuch and he/she/it in/on/with house: palace [the] king for to give: put [obj] Jeremiah to(wards) [the] pit and [the] king to dwell in/on/with gate Benjamin (Gate)
8 Ebed-Meleki akatoka nje ya jumba la kifalme na kumwambia,
and to come out: come Ebed-melech Ebed-melech from house: palace [the] king and to speak: speak to(wards) [the] king to/for to say
9 “Mfalme bwana wangu, watu hawa wamefanya uovu kwa yote waliomtendea nabii Yeremia. Wamemtupa ndani ya kisima, mahali ambapo atakufa kwa njaa wakati ambapo hakuna chakula popote katika mji.”
lord my [the] king be evil [the] human [the] these [obj] all which to make: do to/for Jeremiah [the] prophet [obj] which to throw to(wards) [the] pit and to die underneath: stand him from face: because [the] famine for nothing [the] food: bread still in/on/with city
10 Basi mfalme akamwamuru Ebed-Meleki Mkushi, akisema, “Chukua watu thelathini kutoka hapa pamoja nawe, mkamtoe nabii Yeremia huko kwenye kisima kabla hajafa.”
and to command [the] king [obj] Ebed-melech Ebed-melech [the] Ethiopian to/for to say to take: take in/on/with hand: themselves your from this thirty human and to ascend: establish [obj] Jeremiah [the] prophet from [the] pit in/on/with before to die
11 Basi Ebed-Meleki akawachukua watu pamoja naye, wakaenda mpaka kwenye chumba kilichoko chini ya hazina ndani ya jumba la kifalme. Akachukua matambaa makuukuu pamoja na nguo zilizochakaa kutoka huko, na kumshushia Yeremia kwa kamba ndani ya kisima.
and to take: take Ebed-melech Ebed-melech [obj] [the] human in/on/with hand: to his and to come (in): come house: palace [the] king to(wards) underneath: under [the] treasure and to take: take from there old (rag *Q(K)*) and old rag and to send: depart them to(wards) Jeremiah to(wards) [the] pit in/on/with cord
12 Ebed-Meleki Mkushi akamwambia Yeremia, “Weka haya matambaa makuukuu na hizo nguo zilizochakaa makwapani ili kuzuia kamba.” Yeremia akafanya hivyo,
and to say Ebed-melech Ebed-melech [the] Ethiopian to(wards) Jeremiah to set: make please old [the] rag and [the] rag underneath: under joint hand your from underneath: under to/for cord and to make: do Jeremiah so
13 nao wakamvuta juu kwa kamba na kumtoa katika kisima. Yeremia akakaa katika ua wa walinzi.
and to draw [obj] Jeremiah in/on/with cord and to ascend: establish [obj] him from [the] pit and to dwell Jeremiah in/on/with court [the] guardhouse
14 Ndipo Mfalme Sedekia akatuma watu wamwitie nabii Yeremia wamlete kwake kwenye ingilio la tatu la Hekalu la Bwana. Mfalme akamwambia Yeremia, “Ninataka kukuuliza jambo fulani, usinifiche kitu chochote.”
and to send: depart [the] king Zedekiah and to take: recieve [obj] Jeremiah [the] prophet to(wards) him to(wards) entrance [the] third which in/on/with house: temple LORD and to say [the] king to(wards) Jeremiah to ask I [obj] you word: speaking not to hide from me word
15 Yeremia akamwambia Sedekia, “Nikikupa jibu, je, hutaniua? Hata kama nikikupa shauri, wewe hutanisikiliza.”
and to say Jeremiah to(wards) Zedekiah for to tell to/for you not to die to die me and for to advise you not to hear: hear to(wards) me
16 Lakini Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia kiapo hiki kwa siri, akisema, “Hakika kama aishivyo Bwana, ambaye ametupa pumzi, sitakuua wala sitakutia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wako.”
and to swear [the] king Zedekiah to(wards) Jeremiah in/on/with secrecy to/for to say alive LORD ([obj] *Q(K)*) which to make to/for us [obj] [the] soul: life [the] this if: surely no to die you and if to give: give you in/on/with hand: power [the] human [the] these which to seek [obj] soul: life your
17 Kisha Yeremia akamwambia Sedekia, “Hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Ikiwa utajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, maisha yako yatasalimika, na mji huu hautateketezwa kwa moto. Pia wewe na jamaa yako mtaishi.
and to say Jeremiah to(wards) Zedekiah thus to say LORD God Hosts God Israel if to come out: surrender to come out: surrender to(wards) ruler king Babylon and to live soul: life your and [the] city [the] this not to burn in/on/with fire and to live you(m. s.) and house: household your
18 Lakini ikiwa hutajisalimisha kwa maafisa wa mfalme wa Babeli, mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo na watauteketeza kwa moto, nawe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao.’”
and if not to come out: surrender to(wards) ruler king Babylon and to give: give [the] city [the] this in/on/with hand: power [the] Chaldea and to burn her in/on/with fire and you(m. s.) not to escape from hand: power their
19 Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia, “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbilia kwa Wakaldayo, kwa kuwa Wakaldayo wanaweza kunitia mikononi mwao, nao wakanitenda vibaya.”
and to say [the] king Zedekiah to(wards) Jeremiah I be anxious [obj] [the] Jew which to fall: deserting to(wards) [the] Chaldea lest to give: give [obj] me in/on/with hand: to their and to abuse in/on/with me
20 Yeremia akajibu, “Hawatakutia mikononi mwao. Mtii Bwana kwa kufanya kile ninachokuambia. Kisha utafanikiwa na maisha yako yatakuwa salama.
and to say Jeremiah not to give: give to hear: obey please in/on/with voice LORD to/for which I to speak: speak to(wards) you and be good to/for you and to live soul: life your
21 Lakini ukikataa kujisalimisha, hili ndilo Bwana alilonifunulia:
and if refusing you(m. s.) to/for to come out: surrender this [the] word which to see: see me LORD
22 Wanawake wote walioachwa katika jumba la kifalme la mfalme wa Yuda wataletwa mbele ya maafisa wa mfalme wa Babeli. Wanawake hao watakuambia: “‘Walikupotosha na kukushinda, wale rafiki zako uliowaamini. Miguu yako imezama matopeni; rafiki zako wamekuacha.’
and behold all [the] woman which to remain in/on/with house: palace king Judah to come out: send to(wards) ruler king Babylon and they(fem.) to say to incite you and be able to/for you human peace: friendship your to sink in/on/with mire foot your to turn back
23 “Wake zako wote na watoto wataletwa na kutiwa mikononi mwa Wakaldayo. Wewe mwenyewe hutaweza kujiokoa mikononi mwao. Lakini utatekwa na mfalme wa Babeli, na mji huu utateketezwa kwa moto.”
and [obj] all woman: wife your and [obj] son: child your to come out: send to(wards) [the] Chaldea and you(m. s.) not to escape from hand: power their for in/on/with hand: power king Babylon to capture and [obj] [the] city [the] this to burn in/on/with fire
24 Kisha Sedekia akamwambia Yeremia, “Usiruhusu mtu yeyote ajue kuhusu haya mazungumzo, la sivyo utakufa.
and to say Zedekiah to(wards) Jeremiah man: anyone not to know in/on/with word [the] these and not to die
25 Maafisa wakisikia kwamba nimezungumza nawe, nao wakakujia na kusema, ‘Tuambie kile ulichozungumza na mfalme na kile mfalme alichokuambia, usitufiche au sivyo tutakuua,’
and for to hear: hear [the] ruler for to speak: speak with you and to come (in): come to(wards) you and to say to(wards) you to tell [emph?] please to/for us what? to speak: speak to(wards) [the] king not to hide from us and not to die you and what? to speak: speak to(wards) you [the] king
26 basi waambie, ‘Nilikuwa ninamsihi mfalme asinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani nisije nikafia humo.’”
and to say to(wards) them to fall: fall I supplication my to/for face: before [the] king to/for lest to return: return me house: household Jonathan to/for to die there
27 Maafisa wote wakamjia Yeremia na kumuuliza, naye Yeremia akawaambia kila kitu mfalme alichomwagiza kusema. Kisha hawakusema lolote zaidi na Yeremia kwa sababu hakuna yeyote aliyesikia mazungumzo yake na mfalme.
and to come (in): come all [the] ruler to(wards) Jeremiah and to ask [obj] him and to tell to/for them like/as all [the] word [the] these which to command [the] king and be quiet from him for not to hear: hear [the] word: speaking
28 Naye Yeremia akabaki katika ua wa walinzi hadi siku Yerusalemu ilipotekwa.
and to dwell Jeremiah in/on/with court [the] guardhouse till day which to capture Jerusalem and to be like/as as which to capture Jerusalem