< Yeremia 37 >

1 Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini mwana wa Yehoyakimu.
Le roi Sédécias, fils de Josias, régna à la place de Jéchonias, fils de Joakim, — Nabuchodonosor, roi de Babylone, l'avait établi roi sur le pays de Juda. —
2 Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.
Et il n'écouta point, ni lui, ni ses serviteurs, ni le peuple du pays, les paroles que Yahweh avait prononcées par l'intermédiaire de Jérémie, le prophète.
3 Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”
Le roi Sédécias envoya Juchal, fils de Sélémias, et Sophonie, fils de Maasias, le prêtre, vers Jérémie le prophète, pour lui dire: " Intercède donc pour nous auprès de Yahweh, notre Dieu. "
4 Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani.
Jérémie allait et venait au milieu du peuple, et on ne l'avait pas encore mis en prison.
5 Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.
Or l'armée de Pharaon était sortie d'Egypte, et les Chaldéens qui assiégeaient Jérusalem, en ayant appris la nouvelle, s'étaient éloignés de Jérusalem.
6 Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema:
Alors la parole de Yahweh fut adressée à Jérémie le prophète en ces termes:
7 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri.
Ainsi parle Yahweh, Dieu d'Israël: Vous parlerez ainsi au roi de Juda qui vous a envoyés pour m'interroger: Voici, l’armée de Pharaon qui est sortie pour vous secourir va retourner en son pays, en Egypte.
8 Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’
Et les Chaldéens reviendront, et ils combattront contre cette ville; ils la prendront et la brûleront.
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha!
Ainsi parle Yahweh: Ne vous faites pas illusion en disant: Les Chaldéens s'en iront sûrement loin de nous. Car ils ne s'en iront pas.
10 Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”
Et même quand vous auriez battu toute l'armée des Chaldéens qui combattent contre vous, et qu'il ne resterait d'eux que des blessés, ils se lèveraient chacun dans sa tente et brûleraient cette ville par le feu.
11 Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao,
Pendant que l'armée des Chaldéens s'était éloignée de Jérusalem, à cause de l'armée de Pharaon,
12 Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko.
Jérémie sortit de Jérusalem pour aller au pays de Benjamin, afin de retirer de là sa portion au milieu du peuple.
13 Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”
Mais pendant qu'il était à la porte de Benjamin, le capitaine de la garde, nommé Jérias, fils de Sélémias, fils de Hananias, arrêta Jérémie le prophète, en disant: " Tu passes aux Chaldéens! "
14 Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa.
Jérémie répondit: " C'est, faux, je ne passe pas aux Chaldéens! " Mais Jérias ne l'écouta point; il arrêta Jérémie et l'amena aux chefs.
15 Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.
Et les chefs s'emportèrent contre Jérémie; ils le battirent et le mirent en prison, dans la maison de Jonathan, le secrétaire; car ils en avaient fait une prison.
16 Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu.
Lorsque Jérémie eut pénétré dans la basse-fosse, sous les voûtes, et que Jérémie y fut resté bien des jours,
17 Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?” Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”
Sédécias l'envoya tirer de là. Il l'interrogea secrètement dans sa maison, et lui dit: " Y a-t-il une parole de la part de Yahweh? " Et Jérémie répondit: " Oui! " et il ajouta: " Tu seras livré entre les mains du roi de Babylone. "
18 Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani?
Jérémie dit encore au roi Sédécias: " Quelle offense ai-je commise contre toi, contre tes serviteurs et contre ce peuple, que vous m’ayez mis en prison?
19 Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’
Et où sont vos prophètes qui vous prophétisaient en disant: Le roi de Babylone ne viendra pas contre vous, ni contre ce pays?
20 Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”
Et maintenant écoute, je te prie, ô roi, mon seigneur! Que ma supplication arrive devant toi: Ne me renvoie pas dans la maison de Jonathan, le secrétaire, pour y mourir. "
21 Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.
Le roi Sédécias donna l’ordre de garder Jérémie dans la cour de la prison et de lui donner chaque jour une miche de pain, de la rue des boulangers, jusqu’à ce que tout le pain fût consommé dans la ville. Ainsi Jérémie demeura dans la cour de la prison.

< Yeremia 37 >