< Yeremia 37 >

1 Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini mwana wa Yehoyakimu.
Now king Sedecias the son of Josias reigned instead of Jechonias the son of Joakim: whom Nabuchodonosor king of Babylon made king in the land of Juda.
2 Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.
But neither he, nor his servants, nor the people of the land did obey the words of the Lord, that he spoke in the hand of Jeremias the prophet.
3 Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”
And king Sedecias sent Juchal the son of Selemias, and Sophonias the son of Maasias the priest to Jeremias the prophet, saying: Pray to the Lord our God for us.
4 Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani.
Now Jeremias walked freely in the midst of the people: for they had not as yet cast him into prison.
5 Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.
And the army of Pharao was come out of Egypt: and the Chaldeans that besieged Jerusalem, hearing these tidings, departed from Jerusalem.
6 Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema:
And the word of the Lord came to Jeremias the prophet, saying:
7 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri.
Thus saith the Lord the God of Israel: Thus shall you say to the king of Juda, who sent you to inquire of me: Behold the army of Pharao, which is come forth to help you, shall return into their own land, into Egypt.
8 Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’
And the Chaldeans shall come again, and fight against this city, and take it, and burn it with fire.
9 “Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha!
Thus saith the Lord: Deceive not your souls, saying: The Chaldeans shall surely depart and go away from us: for they shall not go away;
10 Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”
But if you should even beat all the army of the Chaldeans that fight against you, and there should be left of them some wounded men: they shall rise up, every man from his tent, and burn this city with Are.
11 Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao,
Now when the army of the Chaldeans was gone away from Jerusalem, because of Pharao’s army,
12 Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko.
Jeremias went forth out of Jerusalem to go into the land of Benjamin: and to divide a possession there in the presence of the citizens.
13 Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”
And when he was come to the gate of Benjamin, the captain of the gate, who I was there in his turn, was one named Jerias, the son of Selemias, the son of Hananias: and he took hold of Jeremias the prophet, saying: Thou art fleeing to the Chaldeans.
14 Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa.
And Jeremias answered: It is not so, I am not fleeing to the Chaldeans. But he hearkened not to him: so Jerias took Jeremias and brought him to the princes.
15 Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.
Wherefore the princes were angry with Jeremias, and they beat him, and cast him into the prison that was in the house of Jonathan the scribe: for he was chief over the prison.
16 Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu.
So Jeremias went into the house of the prison, and into the dungeon: and Jeremias remained there many days.
17 Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?” Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”
Then Sedecias the king, sending, took him: and asked him secretly in his house, and said: Is there, thinkest thou, any word from the Lord? And Jeremias said: There is. And he said: Thou shalt be delivered into the hands of the king of Babylon.
18 Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani?
And Jeremias said to king Sedecias: In what have I offended against thee, or thy servants, or thy people, that thou hast cast me into prison?
19 Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’
Where are your prophets that prophesied to you, and said: The king of Babylon shall not come against you, and against this land?
20 Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”
Now therefore hear, I beseech thee, my lord the king: let my petition be accepted in thy sight: and send me not back into the house of Jonathan the scribe, lest I die there.
21 Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.
Then king Sedecias commanded that Jeremias should be committed into the entry of the prison: and that they should give him daily a piece of bread, beside broth, till all the bread in the city were spent: and Jeremias remained in the entry of the prison.

< Yeremia 37 >