< Yeremia 36 >

1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
И бысть в лето четвертое Иоакима, сына Иосиина, царя Иудина, бысть слово Господне ко Иеремии глаголя:
2 “Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
возми себе свиток книжный и напиши в нем вся словеса, яже соглаголах к тебе на Израиля и на Иуду и на вся языки, от негоже дне глаголах к тебе, от дне Иосии царя Иудина и до сего дне:
3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
негли услышит дом Иудин вся злая, яже Аз помышляю сотворити им, да отвратятся от пути своего злаго, и милостив буду неправдам их и грехом их.
4 Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
И призва Иеремиа Варуха, сына Нириина: и вписа Варух от уст Иеремииных вся словеса Господня, яже соглагола к нему, во свиток книжный.
5 Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
И заповеда Иеремиа Варуху глаголя: мене стрегут, и не могу внити в дом Господень,
6 Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
ты убо вниди и прочти во свитце сем, в немже написал еси от уст моих словеса Господня, во ушы людий в дому Господни в день поста и во ушы всему дому Иудину, приходящым от градов своих, да прочтеши им:
7 Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
негли падет молитва их пред лицем Господним, и отвратятся от пути своего злаго: яко велика ярость и гнев Господень, егоже соглагола на люди сия.
8 Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
И сотвори Варух сын Нириин но всему, елика заповеда ему Иеремиа пророк прочести во книзе словеса Господня в дому Господни.
9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
И бысть в пятое лето Иоакима царя Иудина, в девятый месяц, заповедаша пост пред лицем Господним всем людем во Иерусалиме и всему множеству, еже снидеся от градов Иудиных во Иерусалим.
10 Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
И прочте Варух во книзе словеса Иеремиина в дому Господни, в дому Гамариеве, сына Сафаня книгочия, во дворе вышнем, во преддверии врат дому Господня новых, во ушы всех людий.
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
И слыша Михей сын Гамариев, сына Сафаня, вся словеса Господня от книги.
12 alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
И сниде в дом царев, в дом книжника, и се, тамо вси князи седяху, Елисам книгочий и Далеа сын Селемиев, и Нафан сын Аховоров и Гамариа сын Сафань, и Седекиа сын Ананиин и вси князи,
13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
и возвести им Михей вся словеса, яже слыша чтуща Варуха во ушы людем.
14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
И послаша вси князи ко Варуху сыну Нириину, Иудину сыну Нафаниину, сына Селемиина, сына Хусиина, глаголюще: книгу, юже ты чтеши во ушы людем, возми ю в руку свою и прииди. И взя Варух сын Нириин книгу в руку свою и сниде к ним.
15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
И рекоша ему: паки прочти во ушы наши. И прочте Варух во ушы их.
16 Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
И бысть яко услышаша вся словеса, совещашася кийждо со ближним своим и реша Варуху: возвещающе возвестим царю вся словеса сия.
17 Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
И вопросиша Варуха, глаголюще: откуду еси вписал вся словеса сия?
18 Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
И рече Варух: от уст своих поведа ми Иеремиа вся словеса сия, аз же писах в книгу.
19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
И рекоша князи Варуху: иди и скрыйся ты и Иеремиа, и человек да не увесть, где вы.
20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
И внидоша ко царю во двор, книгу же вдаша хранити в дому Елисама книгочия, и возвестиша царю вся словеса сия.
21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
И посла царь Иудина взяти книгу. И взя ю от дому Елисамы книгочия, и прочте Иудин во ушы царевы и во ушы всех князей стоящих окрест царя.
22 Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
Царь же седяше во храмине зимней, в девятый месяц, и поставлено бе пред ним огнище со огнем.
23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
И бысть чтущу Иудину третий лист и четвертый, раздроби я бритвою книгочия и возметаше на огненное огнище, дондеже скончася весь свиток на огненнем огнищи.
24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
И не ужасошася и не растерзаша риз своих царь и вси отроцы его, слышавшии вся словеса сия.
25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
Елнафан же и Далеа, и Гамариа и Годолиа глаголаша царю, еже бы не сожещи свитка. И не послуша их.
26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
И повеле царь Иеремеилу сыну цареву и Сараеви сыну Езриилеву и Селемию сыну Авдеилеву, да изымают Варуха книгочия и Иеремию пророка. Но сокры я Господь.
27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
И бысть слово Господне ко Иеремии, егда сожже царь свиток, вся словеса, яже вписа Варух от уст Иеремииных, глаголя:
28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
паки возми ты свиток другий и впиши вся словеса бывшая во свитце, яже сожже царь Иоаким:
29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
и ко Иоакиму царю Иудину речеши: тако рече Господь: ты сожегл еси сию книгу, глаголя: почто вписал еси в ней, глаголя: входя внидет царь Вавилонский и потребит землю сию, и потребятся от нея человецы и скоти?
30 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
Того ради сице рече Господь на Иоакима царя Иудина: не будет ему седящаго на престоле Давидове, и будет тело его мертвое повержено на знои дневнем и на мразе нощнем:
31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
и посещу нань и на его род и на отроки его, и наведу нань и на живущыя во Иерусалиме и на землю Иудину вся злая, яже соглаголах на ня, и не послушаша.
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
И взя Варух свиток другий и вписа в нем от уст Иеремииных вся словеса книги, яже сожже Иоаким царь Иудин: и еще приложишася ему словеса множайша неже первая.

< Yeremia 36 >