< Yeremia 36 >

1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
La quatrième année de Joakim, fils de Josias, roi de Juda, cette parole fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh, en ces termes:
2 “Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
" Prends un volume, et tu y écriras toutes les paroles que je t'ai dites contre Israël, contre Juda et contre toutes les nations, depuis le jour où je t'ai parlé, depuis les jours de Josias, jusqu'aujourd'hui.
3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
Peut-être que la maison de Juda entendra tout le mal que j'ai dessein de leur faire, afin qu'ils se détournent chacun de sa mauvaise voie, et que je pardonne leur iniquité et leur péché. "
4 Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
Jérémie appela donc Baruch, fils de Néria; et Baruch écrivit dans le volume, sous la dictée de Jérémie, toutes les paroles que Yahweh avait dites à celui-ci.
5 Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
Et Jérémie donna cet ordre à Baruch, en disant: " Je suis empêché, et ne puis aller dans la maison de Yahweh.
6 Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
Tu iras donc, toi, et tu liras, dans le volume que tu as écrit sous ma dictée, les paroles de Yahweh aux oreilles du peuple, dans la maison de Yahweh, le jour du jeûne; tu les liras aussi aux oreilles de tous ceux de Juda qui seront venus de leurs villes.
7 Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
Peut-être que leur supplication arrivera devant Yahweh, et qu'ils se détourneront chacun de sa mauvaise voie; car grande est la colère et l'indignation que Yahweh a exprimées contre ce peuple. "
8 Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
Et Baruch, fils de Néria, fit tout ce que Jérémie le prophète lui avait commandé, lisant dans le livre les paroles de Yahweh, dans la maison de Yahweh.
9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
La cinquième année de Joakim, fils de Josias, roi de Juda, le neuvième mois, on publia un jeûne devant Yahweh, pour tout le peuple de Jérusalem et pour tout le peuple qui viendrait des villes de Juda à Jérusalem.
10 Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
Alors Baruch lut dans le livre les paroles de Yahweh, dans la maison de Yahweh, dans la chambre de Gamarias, fils de Saphan, le secrétaire, dans le parvis supérieur, à l'entrée de la porte Neuve de la maison de Yahweh, aux oreilles de tout le peuple.
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
Michée, fils de Gamarias, fils de Saphan, entendit toutes les paroles de Yahweh contenues dans le livre.
12 alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
Il descendit à la maison du roi, dans la chambre du secrétaire; et voici que là étaient assis tous les chefs, Elisama, le secrétaire, Dalaïas, fils de Séméïas, Elnathan, fils d'Achobor, Gamarias, fils de Saphan, Sédécias, fils de Hananias, et tous les chefs.
13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
Et Michée leur rapporta toutes les paroles qu'il avait entendues lorsque Baruch lisait dans le livre, aux oreilles du peuple.
14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
Alors tous les chefs envoyèrent vers Baruch Judi, fils de Nathanias, fils de Sélémias, fils de Chusi, pour lui dire: " Prends le volume dans lequel tu as lu aux oreilles du peuple, et viens! " Baruch, fils de Néria, prit le volume et se rendit auprès d'eux.
15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
Ils lui dirent: " Assieds-toi, et lis ce livre à nos oreilles! " Et Baruch le lut à leurs oreilles.
16 Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
Lorsqu'ils eurent entendu toutes ces paroles, ils se regardèrent avec effroi les uns les autres, et dirent à Baruch: " Il faut que nous rapportions au roi toutes ces paroles. "
17 Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
Puis ils interrogèrent Baruch en ces termes: " Déclare-nous comment tu as écrit toutes ces paroles sorties de sa bouche. "
18 Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
Baruch leur dit: " Il m'a dicté de sa bouche toutes ces paroles, et je les ai écrites sur le livre avec de l'encre. "
19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
Alors les chefs dirent à Baruch: " Va, cache-toi, ainsi que Jérémie, et que personne ne sache où vous êtes. "
20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
Ils entrèrent ensuite chez le roi dans la cour, laissant le volume dans la chambre d'Elisama, le secrétaire, et ils racontèrent aux oreilles du roi toute l'affaire.
21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
Le roi envoya Judi pour prendre le volume; et Judi le prit dans la chambre d'Elisama, le secrétaire, et il le lut aux oreilles du roi et aux oreilles de tous les chefs qui se tenaient debout devant le roi.
22 Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
Or le roi était assis dans l'appartement d'hiver, au neuvième mois, et le brasier était allumé devant lui.
23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
Dès que Judi avait lu trois ou quatre colonnes, le roi coupait le livre avec le canif du secrétaire, et le jetait dans le feu du brasier, jusqu'à ce que tout le volume fût consumé par le feu du brasier.
24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
Le roi et tous ses serviteurs qui entendirent toutes ces paroles, ne furent point effrayés et ne déchirèrent point leurs vêtements.
25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
Pourtant Elnathan, Dalaïas et Gamarias avaient fait des instances auprès du roi pour qu'il ne brûlât pas le volume; mais il ne les avait pas écoutés.
26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
Puis le roi ordonna à Jérémiel, fils du roi, et à Saraïas, fils d'Ezriel, et à Sélémias, fils d'Abdéel, de saisir Baruch, le secrétaire, et Jérémie, le prophète; mais Yahweh les cacha.
27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
Et la parole de Yahweh fut adressée à Jérémie, après que le roi eut brûlé le volume avec les paroles que Baruch avait écrites sous la dictée de Jérémie, en ces termes:
28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
Va prendre un autre volume, et tu y écriras toutes les premières paroles qui étaient dans le premier volume que Joakim, roi de Juda, a brûlé.
29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
Et tu diras à Joakim, roi de Juda: Ainsi parle Yahweh: Toi, tu as brûlé ce volume, en disant: " Pourquoi y as-tu écrit que le roi de Babylone viendra certainement, qu'il dévastera ce pays et qu’il en fera disparaître hommes et bêtes? "
30 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
C’est pourquoi ainsi parle Yahweh touchant Joakim, roi de Juda: Il n'aura pas un des siens assis sur le trône de David; et son cadavre sera jeté dehors, à la chaleur pendant le jour, et au froid pendant la nuit.
31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
Je punirai sur lui, sur sa race et sur ses serviteurs leur iniquité, et je ferai venir sur eux, sur les habitants de Jérusalem et sur les hommes de Juda, tous le mal que je leur ai annoncé sans qu'ils m'aient écouté.
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
Jérémie prit donc un autre volume et le donna à Baruch, fils de Nérias, le secrétaire; et Baruch y écrivit, sous la dictée de Jérémie, toutes les paroles du livre que Joakim, roi de Juda, avait brûlé au feu; et beaucoup d'autres paroles semblables y furent ajoutées.

< Yeremia 36 >