< Yeremia 36 >
1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
It came about in the fourth year of Jehoiakim son of Josiah king of Judah, that this word came to Jeremiah from Yahweh, and he said,
2 “Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
“Take a scroll for yourself and write on it all the words that I have told you concerning Israel and Judah, and every nation. Do this for everything I have told from the days of Josiah until this very day.
3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
Perhaps the people of Judah will listen to all the disasters that I intend to bring on them. Perhaps everyone will turn away from his wicked way, so I can forgive their iniquity and their sin.”
4 Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
Then Jeremiah called Baruch son of Neriah, and Baruch wrote in a scroll, at Jeremiah's dictation, all the words of Yahweh spoken to him.
5 Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
Next Jeremiah gave a command to Baruch. He said, “I am in prison and cannot go to Yahweh's house.
6 Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
So you must go and read from the scroll that you wrote at my dictation. On the day of the fast, you must read Yahweh's words in the hearing of the people in his house, and also in the hearing of all of Judah who have come from their cities. Proclaim these words to them.
7 Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
Perhaps their pleas for mercy will come before Yahweh. Perhaps each person will turn from his wicked way, since the wrath and fury that Yahweh has proclaimed against this people are severe.”
8 Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
So Baruch son of Neriah did everything that Jeremiah the prophet had commanded him to do. He read aloud the words of Yahweh in the house of Yahweh.
9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
It came about in the fifth year and ninth month of Jehoiakim son of Josiah, king of Judah, that all the people in Jerusalem and the people who came to Jerusalem from the cities of Judah proclaimed a fast before Yahweh.
10 Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
Baruch read aloud Jeremiah's words in the house of Yahweh, from the room of Gemariah son of Shaphan the scribe, in the upper courtyard, by the gate of the entrance to the house of Yahweh. He did this in the hearing of all the people.
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
Now Micaiah son of Gemariah son of Shaphan heard all of Yahweh's words in the scroll.
12 alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
He went down to the house of the king, to the secretary's room. Look, all the officials were sitting there: Elishama the secretary, Delaiah son of Shemaiah, Elnathan son of Akbor, Gemariah son of Shaphan, and Zedekiah son of Hananiah, and all the officials.
13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
Then Micaiah reported to them all the words that he had heard that Baruch read aloud in the hearing of the people.
14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
So all the officials sent Jehudi son of Nethaniah son of Shelemiah son of Cushi, to Baruch. Jehudi said to Baruch, “Take the scroll in your hand, the scroll from which you were reading in the hearing of the people, and come.” So Baruch son of Neriah took the scroll in his hand and went to the officials.
15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
Then they said to him, “Sit down and read this in our hearing.” So Baruch read the scroll.
16 Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
It happened that when they heard all these words, each man turned in fear to the one next to him and said to Baruch, “We must certainly report all of these words to the king.”
17 Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
Then they asked Baruch, “Tell us, how did you come to write all these words at Jeremiah's dictation?”
18 Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
Baruch said to them, “He dictated all these words to me, and I wrote them in ink on this scroll.”
19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
Then the officials said to Baruch, “Go, hide yourself, and Jeremiah, too. Do not let anyone know where you are.”
20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
So they put the scroll in the room of Elishama the secretary, and they went to the king in the courtyard and they reported everything in the hearing of the king.
21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
Then the king sent Jehudi to get the scroll. Jehudi took it from the room of Elishama the secretary. Then he read it in the hearing of the king and all the officials who were standing beside him.
22 Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
Now the king was staying in the winter house in the ninth month, and a brazier was burning in front of him.
23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
It happened that as Jehudi read three or four columns, the king would cut it off with a knife and throw it into the fire in the brazier until all of the scroll was destroyed.
24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
But neither the king nor any of his servants who heard all these words were frightened, nor did they tear their clothes.
25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
Elnathan, Delaiah, and Gemariah had even urged the king not to burn the scroll, but he did not listen to them.
26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
Then the king commanded Jerahmeel, a relative, Seraiah son of Azriel, and Shelemiah son of Abdeel to arrest Baruch the scribe and Jeremiah the prophet, but Yahweh had hidden them.
27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
Then the word of Yahweh came to Jeremiah after the king had burned the scroll and the words that Baruch had written at Jeremiah's dictation, saying,
28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
“Go back, take another scroll for yourself, and write in it all the words that were on the original scroll, the one that Jehoiakim king of Judah burned.
29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
Then you must say this to Jehoiakim king of Judah: 'You burned that scroll, saying, “Why have you written on it, 'The king of Babylon will certainly come and destroy this land, for he will destroy both man and beast in it'?”'”
30 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
Therefore Yahweh says this concerning you, Jehoiakim king of Judah: “No descendant of yours will ever sit on the throne of David. As for you, your corpse will be thrown out into the heat of day and the frost of night.
31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
For I will punish you, your descendants, and your servants for the iniquity of you all. I will bring on you, on all the inhabitants of Jerusalem, and on every person in Judah all the disasters with which I have threatened you with, but to which you paid no attention.”
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
So Jeremiah took another scroll and gave it to Baruch son of Neriah the scribe. Baruch wrote on it at Jeremiah's dictation all the words that had been in the scroll burned by Jehoiakim king of Judah. Furthermore, many other similar words were added to this scroll.