< Yeremia 36 >
1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
and to be in/on/with year [the] fourth to/for Jehoiakim son: child Josiah king Judah to be [the] word [the] this to(wards) Jeremiah from with LORD to/for to say
2 “Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
to take: take to/for you scroll scroll: document and to write to(wards) her [obj] all [the] word which to speak: speak to(wards) you upon Israel and upon Judah and upon all [the] nation from day to speak: speak to(wards) you from day Josiah and till [the] day [the] this
3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
perhaps to hear: hear house: household Judah [obj] all [the] distress: harm which I to devise: devise to/for to make: do to/for them because to return: repent man: anyone from way: conduct his [the] bad: evil and to forgive to/for iniquity: crime their and to/for sin their
4 Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
and to call: call to Jeremiah [obj] Baruch son: child Neriah and to write Baruch from lip: word Jeremiah [obj] all word LORD which to speak: speak to(wards) him upon scroll scroll: document
5 Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
and to command Jeremiah [obj] Baruch to/for to say I to restrain not be able to/for to come (in): come house: temple LORD
6 Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
and to come (in): come you(m. s.) and to call: read out in/on/with scroll which to write from lip: word my [obj] word LORD in/on/with ear: hearing [the] people house: temple LORD in/on/with day fast and also in/on/with ear: hearing all Judah [the] to come (in): come from city their to call: read out them
7 Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
perhaps to fall: fall supplication their to/for face: before LORD and to return: repent man: anyone from way: conduct his [the] bad: evil for great: large [the] face: anger and [the] rage which to speak: promise LORD to(wards) [the] people [the] this
8 Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
and to make: do Baruch son: child Neriah like/as all which to command him Jeremiah [the] prophet to/for to call: read out in/on/with scroll: document word LORD house: temple LORD
9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
and to be in/on/with year [the] fifth to/for Jehoiakim son: child Josiah king Judah in/on/with month [the] ninth to call: call out fast to/for face: before LORD all [the] people in/on/with Jerusalem and all [the] people [the] to come (in): come from city Judah in/on/with Jerusalem
10 Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
and to call: read out Baruch in/on/with scroll: document [obj] word Jeremiah house: temple LORD in/on/with chamber Gemariah son: child Shaphan [the] secretary in/on/with court [the] high entrance gate house: temple LORD [the] New (Gate) in/on/with ear: hearing all [the] people
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
and to hear: hear Micaiah son: child Gemariah son: child Shaphan [obj] all word LORD from upon [the] scroll: document
12 alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
and to go down house: palace [the] king upon chamber [the] secretary and behold there all [the] ruler to dwell Elishama [the] secretary and Delaiah son: child Shemaiah and Elnathan son: child Achbor and Gemariah son: child Shaphan and Zedekiah son: child Hananiah and all [the] ruler
13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
and to tell to/for them Micaiah [obj] all [the] word which to hear: hear in/on/with to call: read out Baruch in/on/with scroll: document in/on/with ear: hearing [the] people
14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
and to send: depart all [the] ruler to(wards) Baruch [obj] Jehudi son: child Nethaniah son: child Shelemiah son: child Cushi to/for to say [the] scroll which to call: read out in/on/with her in/on/with ear: hearing [the] people to take: take her in/on/with hand your and to go: come and to take: take Baruch son: child Neriah [obj] [the] scroll in/on/with hand his and to come (in): come to(wards) them
15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
and to say to(wards) him to dwell please and to call: read out her in/on/with ear: to ears our and to call: read out Baruch in/on/with ear: to ears their
16 Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
and to be like/as to hear: hear they [obj] all [the] word to dread man: anyone to(wards) neighbor his and to say to(wards) Baruch to tell to tell to/for king [obj] all [the] word [the] these
17 Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
and [obj] Baruch to ask to/for to say to tell please to/for us how? to write [obj] all [the] word [the] these from lip: word his
18 Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
and to say to/for them Baruch from lip his to call: read out to(wards) me [obj] all [the] word [the] these and I to write upon [the] scroll: document in/on/with ink
19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
and to say [the] ruler to(wards) Baruch to go: went to hide you(m. s.) and Jeremiah and man: anyone not to know where? you(m. p.)
20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
and to come (in): come to(wards) [the] king court [to] and [obj] [the] scroll to reckon: put in/on/with chamber Elishama [the] secretary and to tell in/on/with ear: to ears [the] king [obj] all [the] word
21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
and to send: depart [the] king [obj] Jehudi to/for to take: take [obj] [the] scroll and to take: take her from chamber Elishama [the] secretary and to call: read out her Jehudi in/on/with ear: to ears [the] king and in/on/with ear: to ears all [the] ruler [the] to stand: stand from upon [the] king
22 Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
and [the] king to dwell house: palace [the] autumn in/on/with month [the] ninth and [obj] [the] hearth to/for face: before his to burn: burn
23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
and to be like/as to call: read out Jehudi three door and four to tear her in/on/with razor [the] secretary and to throw to(wards) [the] fire which to(wards) [the] hearth till to finish all [the] scroll upon [the] fire which upon [the] hearth
24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
and not to dread and not to tear [obj] garment their [the] king and all servant/slave his [the] to hear: hear [obj] all [the] word [the] these
25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
and also Elnathan and Delaiah and Gemariah to fall on in/on/with king to/for lest to burn [obj] [the] scroll and not to hear: hear to(wards) them
26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
and to command [the] `the king` [obj] Jerahmeel son: child [the] `the king` and [obj] Seraiah son: child Azriel and [obj] Shelemiah son: child Abdeel to/for to take: take [obj] Baruch [the] secretary and [obj] Jeremiah [the] prophet and to hide them LORD
27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
and to be word LORD to(wards) Jeremiah after to burn [the] king [obj] [the] scroll and [obj] [the] word which to write Baruch from lip: word Jeremiah to/for to say
28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
to return: again to take: take to/for you scroll another and to write upon her [obj] all [the] word [the] first: previous which to be upon [the] scroll [the] first which to burn Jehoiakim king Judah
29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
and upon Jehoiakim king Judah (to say *LA(bh)*) thus to say LORD you(m. s.) to burn [obj] [the] scroll [the] this to/for to say why? to write upon her to/for to say to come (in): come to come (in): come king Babylon and to ruin [obj] [the] land: country/planet [the] this and to cease from her man and animal
30 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
to/for so thus to say LORD upon Jehoiakim king Judah not to be to/for him to dwell upon throne David and carcass his to be to throw to/for drought in/on/with day and to/for ice in/on/with night
31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
and to reckon: punish upon him and upon seed: children his and upon servant/slave his [obj] iniquity: crime their and to come (in): bring upon them and upon to dwell Jerusalem and to(wards) man: anyone Judah [obj] all [the] distress: harm which to speak: promise to(wards) them and not to hear: hear
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
and Jeremiah to take: take scroll another and to give: give her to(wards) Baruch son: child Neriah [the] secretary and to write upon her from lip: word Jeremiah [obj] all word [the] scroll: document which to burn Jehoiakim king Judah in/on/with fire and still to add upon them word many like/as them