< Yeremia 36 >

1 Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, neno hili lilimjia nabii Yeremia kutoka kwa Bwana, kusema:
Now it came about in the fourth year of Jehoiakim, the son of Josiah, king of Judah, that this word came to Jeremiah from the Lord, saying,
2 “Chukua kitabu uandike ndani yake maneno yote niliyonena nawe kuhusu Israeli, Yuda na mataifa mengine yote, tangu nilipoanza kunena nawe wakati wa utawala wa Yosia hadi sasa.
Take a book and put down in it all the words I have said to you against Israel and against Judah and against all the nations, from the day when my word came to you in the days of Josiah till this day.
3 Labda watu wa Yuda watakaposikia juu ya kila maafa ninayokusudia kuwapiga nayo, kila mmoja wao atageuka kutoka njia zake mbaya, kisha nitasamehe uovu wao na dhambi yao.”
It may be that the people of Judah, hearing of all the evil which it is my purpose to do to them, will be turned, every man from his evil ways; so that they may have my forgiveness for their evil-doing and their sin.
4 Hivyo Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria, naye Yeremia alipokuwa akiyakariri maneno yote aliyoyasema Bwana, Baruku akayaandika katika kitabu.
Then Jeremiah sent for Baruch, the son of Neriah; and Baruch took down from the mouth of Jeremiah all the words of the Lord which he had said to him, writing them in a book.
5 Kisha Yeremia akamwambia Baruku, “Nimezuiliwa, mimi siwezi kuingia katika Hekalu la Bwana.
And Jeremiah gave orders to Baruch, saying, I am shut up, and am not able to go into the house of the Lord:
6 Basi wewe nenda katika nyumba ya Bwana siku ya kufunga, uwasomee watu maneno ya Bwana kutoka kitabu hiki yale uliyoyaandika kutoka kinywani mwangu. Wasomee watu wote wa Yuda waliofika kutoka miji yao.
So you are to go, reading there from the book, which you have taken down from my mouth, the words of the Lord, in the hearing of the people in the Lord's house, on a day when they go without food, and in the hearing of all the men of Judah who have come out from their towns.
7 Labda wataomba na kusihi mbele za Bwana na kila mmoja akageuka kutoka njia zake mbaya, kwa sababu hasira na ghadhabu zilizotamkwa dhidi ya watu hawa na Bwana ni kubwa.”
It may be that their prayer for grace will go up to the Lord, and that every man will be turned from his evil ways: for great is the wrath and the passion made clear by the Lord against this people.
8 Baruku mwana wa Neria akafanya kila kitu nabii Yeremia alichomwambia kufanya. Alisoma maneno ya Bwana katika Hekalu la Bwana kutoka kile kitabu.
And Baruch, the son of Neriah, did as Jeremiah the prophet gave him orders to do, reading from the book the words of the Lord in the Lord's house.
9 Katika mwezi wa tisa, mnamo mwaka wa tano wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda, wakati wa kufunga mbele za Bwana, ilitangazwa kwa watu wote walioko Yerusalemu, na wale wote waliokuwa wamekuja kutoka miji ya Yuda.
Now it came about in the fifth year of Jehoiakim, the son of Josiah, king of Judah, in the ninth month, that it was given out publicly that all the people in Jerusalem, and all the people who came from the towns of Judah to Jerusalem, were to keep from food before the Lord.
10 Kutoka chumba cha Gemaria mwana wa Shafani mwandishi, kilichokuwa katika ua wa juu kwenye ingilio la Lango Jipya la Hekalu, Baruku akawasomea watu wote waliokuwa katika Hekalu la Bwana maneno ya Yeremia kutoka kwenye kile kitabu.
Then Baruch gave a public reading of the words of Jeremiah from the book, in the house of the Lord, in the room of Gemariah, the son of Shaphan the scribe, in the higher square, as one goes in by the new doorway of the Lord's house, in the hearing of all the people.
11 Basi Mikaya mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana kutoka kwenye kile kitabu,
And Micaiah, the son of Gemariah, the son of Shaphan, after hearing all the words of the Lord from the book,
12 alishuka hadi kwenye chumba cha mwandishi kwenye jumba la kifalme, mahali walipokuwa wameketi maafisa wote: yaani Elishama mwandishi, Delaya mwana wa Shemaya, Elnathani mwana wa Akbori, Gemaria mwana wa Shafani, Sedekia mwana wa Hanania, na maafisa wengine wote.
Went down to the king's house, to the scribe's room: and all the rulers were seated there, Elishama the scribe and Delaiah, the son of Shemaiah, and Elnathan, the son of Achbor, and Gemariah, the son of Shaphan, and Zedekiah, the son of Hananiah, and all the rulers.
13 Baada ya Mikaya kuwaambia kila kitu ambacho alikuwa amesikia Baruku akiwasomea watu kutoka kwenye kile kitabu,
Then Micaiah gave them an account of all the words which had come to his ears when Baruch was reading the book to the people.
14 maafisa wote wakamtuma Yehudi mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, kumwambia Baruku, “Leta hicho kitabu ambacho umewasomea watu, nawe mwenyewe uje.” Ndipo Baruku mwana wa Neria akawaendea akiwa na hicho kitabu mkononi mwake.
So all the rulers sent Jehudi, the son of Nethaniah, the son of Shelemiah, the son of Cushi, to Baruch, saying, Take in your hand the book from which you have been reading to the people and come. So Baruch, the son of Neriah, took the book in his hand and came down to them.
15 Wakamwambia, “Tafadhali, keti na utusomee hicho kitabu.” Ndipo Baruku akawasomea kile kitabu.
Then they said to him, Be seated now, and give us a reading from it. So Baruch did so, reading it to them.
16 Walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana wao kwa wao kwa woga na kumwambia Baruku, “Lazima tutoe taarifa ya maneno haya yote kwa mfalme.”
Now it came about that, after hearing all the words, they said to one another in fear, We will certainly give the king an account of all these words.
17 Kisha wakamuuliza Baruku, “Tuambie, uliandikaje haya yote? Je, yalitoka kinywani mwa Yeremia?”
And questioning Baruch, they said, Say now, how did you put all these words down in writing from his mouth?
18 Baruku akajibu, “Ndiyo, maneno haya yote yalitoka kinywani mwa Yeremia, nami nikayaandika kwa wino katika hiki kitabu.”
Then Baruch, answering, said, He said all these things to me by word of mouth, and I put them down with ink in the book.
19 Ndipo wale maafisa wakamwambia Baruku, “Wewe na Yeremia nendeni mkajifiche. Mtu yeyote asijue mahali mlipo.”
Then the rulers said to Baruch, Go and put yourself in a safe place, you and Jeremiah, and let no man have knowledge of where you are.
20 Baada ya kuhifadhi kile kitabu ndani ya chumba cha Elishama mwandishi, wakamwendea mfalme katika ua wa nje na kumwarifu kila kitu.
Then they went into the open square to the king; but the book they put away in the room of Elishama the scribe; and they gave the king an account of all the words.
21 Mfalme akamtuma Yehudi akachukue kile kitabu. Yehudi akakileta hicho kitabu kutoka kwenye chumba cha Elishama mwandishi, na akakisoma mbele ya mfalme na maafisa wakiwa wamesimama kando ya mfalme.
So the king sent Jehudi to get the book, and he took it from the room of Elishama the scribe. And Jehudi gave a reading of it in the hearing of the king and all the rulers who were by the king's side.
22 Ulikuwa mwezi wa tisa, na mfalme alikuwa ameketi chumba cha wakati wa baridi akiota moto.
Now the king was seated in the winter house, and a fire was burning in the fireplace in front of him.
23 Hata ikawa kila wakati Yehudi alipomaliza kusoma kurasa tatu au nne za hicho kitabu, mfalme alizikata kwa kisu cha mwandishi na kuzitupia motoni, hadi kitabu chote kikateketea.
And it came about that whenever Jehudi, in his reading, had got through three or four divisions, the king, cutting them with his penknife, put them into the fire, till all the book was burned up in the fire which was burning in the fireplace.
24 Mfalme na watumishi wake wote waliosikia yote yaliyosomwa hawakuonyesha hofu yoyote, wala hawakuyararua mavazi yao.
But they had no fear and gave no signs of grief, not the king or any of his servants, after hearing all these words.
25 Hata ingawa Elnathani, Delaya na Gemaria walimsihi mfalme asikichome kile kitabu, yeye hakuwasikiliza.
And Elnathan and Delaiah and Gemariah had made a strong request to the king not to let the book be burned, but he would not give ear to them.
26 Badala yake, mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, Seraya mwana wa Azrieli, na Shelemia mwana wa Abdeeli kuwakamata mwandishi Baruku na nabii Yeremia. Lakini Bwana alikuwa amewaficha.
And the king gave orders to Jerahmeel, the king's son, and Seraiah, the son of Azriel, and Shelemiah, the son of Abdeel, to take Baruch the scribe and Jeremiah the prophet: but the Lord kept them safe.
27 Baada ya mfalme kuchoma kile kitabu kilichokuwa na yale maneno Baruku aliyokuwa ameyaandika kutoka kinywani mwa Yeremia, neno la Bwana lilimjia Yeremia likisema:
Then after the book, in which Baruch had put down the words of Jeremiah, had been burned by the king, the word of the Lord came to Jeremiah, saying,
28 “Chukua kitabu kingine na uandike juu yake maneno yote yaliyokuwa katika kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda amekiteketeza kwa moto.
Take another book and put down in it all the words which were in the first book, which Jehoiakim, king of Judah, put into the fire.
29 Mwambie pia Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ulikiteketeza kile kitabu ukasema, “Kwa nini uliandika kwenye kitabu kwamba kwa hakika mfalme wa Babeli angekuja na kuangamiza nchi hii, na kuwakatilia mbali watu na wanyama kutoka humo?”
And about Jehoiakim, king of Judah, you are to say, This is what the Lord has said: You have put this book into the fire, saying, Why have you put in it that the king of Babylon will certainly come, causing the destruction of this land and putting an end to every man and beast in it?
30 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana kuhusu Yehoyakimu mfalme wa Yuda: Hatakuwa na mtu yeyote atakayekalia kiti cha enzi cha Daudi; maiti yake itatupwa nje kwenye joto wakati wa mchana na kupigwa na baridi wakati wa usiku.
For this reason the Lord has said of Jehoiakim, king of Judah, He will have no son to take his place on the seat of David: his dead body will be put out to undergo the heat of the day and the cold of the night.
31 Nitamwadhibu yeye, watoto wake na watumishi wake kwa ajili ya uovu wao. Nitaleta juu yao na wote waishio Yerusalemu na watu wa Yuda kila maafa niliyoyasema dhidi yao, kwa sababu hawajasikiliza.’”
And I will send punishment on him and on his seed and on his servants for their evil-doing; I will send on them and on the people of Jerusalem and the men of Judah, all the evil which I said against them, but they did not give ear.
32 Kisha Yeremia akachukua kitabu kingine na kumpa mwandishi Baruku mwana wa Neria, naye kama Yeremia alivyosema, Baruku akaandika juu yake maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa amekichoma moto, na maneno mengine mengi yaliyofanana na hayo yaliyoongezewa humo.
Then Jeremiah took another book, and gave it to Baruch the scribe, the son of Neriah, who put down in it, from the mouth of Jeremiah, all the words of the book which had been burned in the fire by Jehoiakim, king of Judah: and in addition a number of other words of the same sort.

< Yeremia 36 >