< Yeremia 34 >

1 Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
Слово, еже бысть ко Иеремии от Господа, егда Навуходоносор царь Вавилонский и вси вои его, и вся земля власти его и вси людие воеваху на Иерусалим и на вся грады Иудины, глаголя:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
тако рече Господь Бог Израилев: иди ко Седекии царю Иудину и речеши ему: тако рече Господь: преданием предастся сей град в руце царя Вавилонска, и возмет его и пожжет его огнем:
3 Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
и ты не уцелееши от руку его, и ят будеши, и в руце его предасися: и очи твои очи его узрят, и уста его со усты твоими соглаголют, и в Вавилон внидеши.
4 “‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
Но обаче слыши слово Господне, Седекие, царю Иудин! Тако глаголет Господь к тебе: не умреши от меча, но в мире умреши:
5 utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
и якоже плакаша отцев твоих царствовавших прежде тебе, восплачутся и тебе: увы, господи, и: увы, господи! Восплачутся и тебе, яко слово Аз соглаголах, рече Господь.
6 Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
И глагола Иеремиа пророк ко Седекии царю Иудину вся словеса сия во Иерусалиме.
7 wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
И сила царя Вавилонска воева на Иерусалим и на грады Иудины оставшыяся: на Лахис и на Азику, яко тии осташася во градех Иудиных грады тверды.
8 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
Слово бывшее ко Иеремии от Господа, повнегда скончати царю Седекии завет к людем, иже во Иерусалиме, еже нарещи им отпущение,
9 Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
еже отпустити комуждо раба своего и комуждо рабыню свою, Евреанина и Евреаныню, свободны, да не работает муж от Израиля.
10 Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
И обратишася вси вельможи и вси людие вступившии в завет еже отпустити комуждо раба своего и комуждо рабу свою свободны и ктому не владети ими. Слышаша убо и отпустиша.
11 Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
И обратишася по сих вспять и удержаша паки рабы и рабыни своя, ихже отпустиша свободных, и взяша в рабы и рабыни.
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
И бысть слово Господне ко Иеремии от Господа глаголя:
13 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
тако рече Господь Бог Израилев: Аз завещах завет ко отцем вашым в день, в оньже избавих я от земли Египетския, из дому работы, глаголя:
14 ‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
егда скончаются шесть лет, да отпустиши брата своего Евреанина, иже продан есть тебе: и да делает ти шесть лет, и да отпустиши его свободна от себе. И не послушаша Мене отцы ваши, ни приклониша уха своего.
15 Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
И обратистеся вы днесь сотворити правая пред очима Моима, еже нарещи комуждо отпущение ближняго своего: и совершисте завет пред лицем Моим в дому, идеже наречеся имя Мое в нем:
16 Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
и отвратистеся, и осквернисте завет Мой, еже возвратити комуждо раба своего и комуждо рабу свою, ихже отпустисте свободны душею их: и покористе их, якоже быти у вас в рабы и в рабыни.
17 “Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
Того ради сице рече Господь: вы не послушасте Мене, нарещи отпущения кийждо брату своему и кийждо ближнему своему: се, Аз нарицаю отпущение вам на мечь и на смерть и на глад, и дам вы на разсыпание всем царствам земным:
18 Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
и дам мужы преступившыя завет Мой и не хранящыя словес завета Моего, емуже соизволиша пред лицем Моим: телца егоже разсекоша на две части и ходиша между разделенными частьми его:
19 Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
князи Иудины и князи Иерусалимли, и вельможы и жерцы и вся люди земли ходящыя между разделеным телцем,
20 nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
и дам я в руки врагом их и в руки ищущих души их, и будут трупи их в ядь птицам небесным и зверем земным:
21 “Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
и Седекию царя Иудейска и князи его дам в руце врагов их и в руку ищущих души их и в руку воинства царя Вавилонска, отбегающих от них.
22 Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”
Се, Аз завещаю, рече Господь, и возвращу я в землю сию, и повоюют на ню, и возмут ю, и пожгут ю огнем и грады Иудины: и дам я в непроходны от живущих.

< Yeremia 34 >