< Yeremia 34 >
1 Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
La parole qui fut adressée en ces mots à Jérémie, de la part de l'Éternel, lorsque Nébucadnetsar, roi de Babylone, et toute son armée, tous les royaumes de la terre gouvernés par sa main, et tous les peuples, combattaient contre Jérusalem et contre toutes ses villes:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
Ainsi a dit l'Éternel, le Dieu d'Israël: Va, et parle à Sédécias, roi de Juda, et dis-lui: Ainsi a dit l'Éternel: Voici, je vais livrer cette ville dans la main du roi de Babylone, et il la brûlera.
3 Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
Et toi, tu n'échapperas pas à sa main; car certainement tu seras pris, et tu seras livré entre ses mains; et tes yeux verront les yeux du roi de Babylone, et il te parlera bouche à bouche, et tu iras à Babylone.
4 “‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
Toutefois, écoute la parole de l'Éternel, Sédécias, roi de Juda! Ainsi a dit l'Éternel: Tu ne mourras point par l'épée.
5 utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
Tu mourras en paix, et comme on a brûlé des parfums pour tes pères, les rois précédents qui ont été avant toi, on en brûlera pour toi et on te pleurera, en disant: Hélas, Seigneur! Car j'ai prononcé cette parole, dit l'Éternel.
6 Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
Jérémie, le prophète, prononça toutes ces paroles à Sédécias, roi de Juda, à Jérusalem.
7 wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
Et l'armée du roi de Babylone combattait contre Jérusalem et contre toutes les villes de Juda qui restaient, contre Lakis et contre Azéka; car c'étaient les villes fortes qui restaient d'entre les villes de Juda.
8 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
La parole qui fut adressée par l'Éternel à Jérémie, après que le roi Sédécias eut fait une alliance avec tout le peuple de Jérusalem, pour proclamer la liberté parmi eux,
9 Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
Afin que chacun renvoyât libre son serviteur israélite et chacun sa servante israélite, et que personne ne rendît esclave le Juif, son frère.
10 Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
Tous les chefs et tout le peuple qui étaient entrés dans cette alliance, s'engagèrent à renvoyer libres chacun son serviteur et chacun sa servante, sans plus les tenir dans l'esclavage. Ils obéirent et les renvoyèrent.
11 Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
Mais ensuite ils changèrent d'avis, et firent revenir leurs serviteurs et leurs servantes, qu'ils avaient renvoyés libres, et se les assujettirent comme serviteurs et comme servantes.
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Alors la parole de l'Éternel fut adressée à Jérémie, en ces mots:
13 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
Ainsi a dit l'Éternel le Dieu d'Israël: J'ai fait alliance avec vos pères au jour où je les tirai hors du pays d'Égypte, de la maison de servitude, et je leur ai dit:
14 ‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
Au bout de sept ans, vous renverrez chacun votre frère hébreu qui vous aura été vendu. Il te servira six ans: puis tu le renverras libre de chez toi. Mais vos pères ne m'ont point écouté et n'ont point prêté l'oreille.
15 Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
Cependant vous étiez revenus aujourd'hui; vous aviez fait ce qui est droit à mes yeux, en publiant chacun la liberté de son prochain; et vous aviez traité l'alliance en ma présence, dans la maison sur laquelle mon nom est invoqué.
16 Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
Mais vous avez changé d'avis, et vous avez profané mon nom, en faisant revenir chacun son serviteur et chacun sa servante, que vous aviez renvoyés libres et pour être à eux-mêmes; et vous les avez forcés à être vos serviteurs et vos servantes.
17 “Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Éternel: Vous ne m'avez point obéi, pour publier la liberté, chacun à son frère, chacun à son prochain; voici, dit l'Éternel, je publie la liberté contre vous à l'épée, à la peste et à la famine, et je vous livrerai pour être agités par tous les royaumes de la terre.
18 Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
Et je livrerai les hommes qui ont transgressé mon alliance, qui n'ont pas exécuté les paroles de l'accord qu'ils avaient fait devant moi, en passant entre les deux moitiés du veau qu'ils avaient coupé en deux,
19 Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
Les chefs de Juda et les chefs de Jérusalem, les eunuques et les sacrificateurs, et tous les gens du pays qui ont passé entre les moitiés du veau,
20 nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
Je les livrerai entre les mains de leurs ennemis, entre les mains de ceux qui cherchent leur vie, et leurs cadavres seront la pâture des oiseaux du ciel et des bêtes de la terre.
21 “Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
Je livrerai aussi Sédécias, roi de Juda, avec ses princes, entre les mains de leurs ennemis et entre les mains de ceux qui cherchent leur vie, entre les mains de l'armée du roi de Babylone qui s'est éloigné de vous.
22 Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”
Voici, je vais donner ordre, dit l'Éternel, et je les ramènerai contre cette ville. Et ils combattront contre elle, et ils la prendront, et la brûleront; et je mettrai les villes de Juda en désolation, sans aucun habitant.