< Yeremia 34 >

1 Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
La parole qui vint à Jérémie de par l’Éternel, lorsque Nebucadnetsar, roi de Babylone, et toute son armée, et tous les royaumes de la terre sur lesquels dominait sa main, et tous les peuples, combattaient contre Jérusalem et contre toutes ses villes, disant:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
Ainsi dit l’Éternel, le Dieu d’Israël: Va, et tu parleras à Sédécias, roi de Juda, et tu lui diras: Ainsi dit l’Éternel: Voici, je livre cette ville en la main du roi de Babylone, et il la brûlera par le feu;
3 Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
et toi, tu n’échapperas pas à sa main, car certainement tu seras pris, et tu seras livré en sa main, et tes yeux verront les yeux du roi de Babylone, et sa bouche parlera à ta bouche, et tu iras à Babylone.
4 “‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
Seulement, écoute la parole de l’Éternel, Sédécias, roi de Juda! Ainsi dit l’Éternel sur toi: Tu ne mourras pas par l’épée;
5 utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
tu mourras en paix, et, comme on a brûlé [des aromates] pour tes pères, les rois précédents qui ont été avant toi, ainsi on en brûlera pour toi, et on se lamentera sur toi, [disant]: Hélas, seigneur! Car j’ai dit cette parole, dit l’Éternel.
6 Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
Et Jérémie le prophète dit à Sédécias, roi de Juda, toutes ces paroles, dans Jérusalem.
7 wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
Et l’armée du roi de Babylone combattit contre Jérusalem, et contre toutes les villes de Juda qui restaient, contre Lakis et contre Azéka; car c’étaient, d’entre les villes de Juda, les villes fortes qui restaient.
8 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
La parole qui vint à Jérémie de par l’Éternel, après que le roi Sédécias eut fait un pacte avec tout le peuple qui était à Jérusalem, pour leur proclamer la liberté:
9 Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
pour que chacun renvoie libre son serviteur, et chacun sa servante, hébreu ou hébreue, pour que personne ne fasse plus servir son frère, un Juif.
10 Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
Et tous les princes et tout le peuple qui étaient entrés dans ce pacte écoutèrent pour renvoyer libres chacun son serviteur et chacun sa servante, pour ne plus les obliger à servir: ils écoutèrent et les renvoyèrent.
11 Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
Mais ensuite ils revinrent en arrière, et firent revenir les serviteurs et les servantes qu’ils avaient renvoyés libres, et les assujettirent pour être serviteurs et servantes.
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Et la parole de l’Éternel vint à Jérémie de par l’Éternel, disant:
13 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
Ainsi dit l’Éternel, le Dieu d’Israël: J’ai fait une alliance avec vos pères, au jour où je les ai fait sortir du pays d’Égypte, de la maison de servitude, disant:
14 ‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
Au bout de sept ans vous renverrez chacun votre frère, l’hébreu qui se sera vendu à toi; il te servira six ans, et tu le renverras libre de chez toi. Mais vos pères ne m’ont point écouté, et n’ont pas incliné leur oreille.
15 Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
Et vous, vous en étiez revenus aujourd’hui, et vous aviez fait ce qui est droit à mes yeux, en proclamant la liberté chacun à son prochain, et vous aviez fait une alliance devant moi, dans la maison qui est appelée de mon nom;
16 Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
mais vous êtes revenus en arrière, et vous avez profané mon nom; et vous avez fait revenir chacun son serviteur, et chacun sa servante, que vous aviez renvoyés libres [pour agir] à leur gré, et vous les avez assujettis pour vous être serviteurs et servantes.
17 “Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
C’est pourquoi, ainsi dit l’Éternel: Vous ne m’avez point écouté pour proclamer la liberté chacun à son frère, et chacun à son prochain; voici, je proclame, dit l’Éternel, la liberté contre vous à l’épée, à la peste, et à la famine; et je vous livrerai pour être chassés çà et là par tous les royaumes de la terre.
18 Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
Et je livrerai les hommes qui ont transgressé mon alliance, qui n’ont point accompli les paroles de l’alliance qu’ils avaient faite devant moi (le veau qu’ils ont coupé en deux et entre les pièces duquel ils ont passé),
19 Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
les princes de Juda, et les princes de Jérusalem, les eunuques, et les sacrificateurs, et tout le peuple du pays, qui ont passé entre les pièces du veau;
20 nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
je les livrerai en la main de leurs ennemis, et en la main de ceux qui cherchent leur vie, et leurs cadavres seront en pâture aux oiseaux des cieux et aux bêtes de la terre.
21 “Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
Et je livrerai Sédécias, roi de Juda, et ses princes, en la main de leurs ennemis, et en la main de ceux qui cherchent leur vie, et en la main de l’armée du roi de Babylone, qui s’est retirée d’auprès de vous.
22 Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”
Voici, je commande, dit l’Éternel, et je les fais revenir contre cette ville; et ils combattront contre elle, et la prendront, et la brûleront par le feu; et des villes de Juda, j’en ferai une désolation, de sorte qu’il n’y aura pas d’habitant.

< Yeremia 34 >