< Yeremia 34 >

1 Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh, lorsque Nabuchodonosor, roi de Babylone, avec toute son armée, tous les royaumes de la terre soumis à sa domination et tous les peuples, combattaient contre Jérusalem et contre toutes les villes de sa dépendance — en ces termes:
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
Ainsi parle Yahweh, Dieu d'Israël: Va et parle à Sédécias, roi de Juda, et dis-lui: Ainsi parle Yahweh: Voici que je vais livrer cette ville au roi de Babylone et il la brûlera.
3 Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
Et toi, tu n'échapperas pas à sa main, car tu seras certainement pris et livré entre ses mains; tes yeux verront les yeux du roi de Babylone, il te parlera bouche à bouche, et tu iras à Babylone.
4 “‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
Toutefois écoute la parole de Yahweh, Sédécias, roi de Juda! Ainsi parle Yahweh à ton sujet: Tu ne mourras point par l'épée.
5 utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
Tu mourras en paix et, comme on a brûlé des parfums pour tes pères, les anciens rois qui t'ont précédé, ainsi on en brûlera pour toi, et on se lamentera sur toi en disant: Hélas! Seigneur! Car moi, j'ai prononcé cette parole, — oracle de Yahweh.
6 Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
Jérémie le prophète dit toutes ces paroles à Sédécias, roi de Juda, à Jérusalem.
7 wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
Or l'armée du roi de Babylone combattait contre Jérusalem et contre toutes les villes de Juda qui tenaient encore, contre Lachis et contre Azéca; car des villes de Juda, des villes fortes, il ne restait plus que celles-là.
8 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh, après que le roi Sédécias eut fait un accord avec tout le peuple de Jérusalem pour publier à leur adresse un affranchissement,
9 Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
afin que chacun renvoyât libre son esclave et chacun sa servante, hébreu ou hébreuse, et qu'il n'y eût personne qui retînt en servitude un Judéen son frère.
10 Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
Tous les chefs et tout le peuple, qui étaient entrés dans cet accord, consentirent à renvoyer libres chacun son esclave et chacun sa servante, pour ne plus les retenir en servitude; ils y consentirent et les renvoyèrent.
11 Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
Mais ensuite ils changèrent d'avis et firent revenir les esclaves, hommes et femmes, qu'ils avaient renvoyés libres, et les obligèrent à redevenir esclaves et servantes.
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Et la parole de Yahweh fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh en ces termes:
13 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
Ainsi parle Yahweh, Dieu d'Israël: Moi j'avais fait alliance avec vos pères au jour où je les fis sortir du pays d'Egypte, de la maison de servitude, en leur disant:
14 ‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
Au terme de sept ans, chacun de vous renverra libre son frère hébreu qui lui aura été vendu; il te servira six ans, puis tu le renverras libre de chez toi. Mais vos pères ne m'ont point écouté; ils n'ont point prêté l'oreille.
15 Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
Vous, aujourd'hui, vous étiez revenus, et aviez fait ce qui est droit à mes yeux, en proclamant la liberté, chacun pour son prochain; vous aviez conclu un accord en ma présence, dans la maison sur laquelle mon nom est invoqué.
16 Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
Mais vous avez changé d'avis, et vous avez profané mon nom, en faisant revenir chacun votre esclave et chacun votre servante, que vous aviez affranchis et rendus à eux-mêmes, et en les obligeant à redevenir vos esclaves et vos servantes.
17 “Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
C’est pourquoi ainsi parle Yahweh: Vous ne m'avez point obéi en publiant un affranchissement chacun pour son frère, chacun pour son prochain; voici que je publie pour vous un affranchissement — oracle de Yahweh; je vous renvoie à l'épée, à la peste et à la famine, et je ferai de vous un objet de terreur parmi tous les royaumes de la terre.
18 Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
Et les hommes qui ont transgressé mon accord, qui n'ont point exécuté les termes de l'accord qu'ils ont conclu en ma présence, je les rendrai tels que le jeune taureau qu'ils ont coupé en deux pour passer entre les morceaux:
19 Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
les chefs de Juda et les chefs de Jérusalem, les eunuques, les prêtres, et tous les gens du pays qui ont passé entre les morceaux du jeune taureau.
20 nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
Je les livrerai entre les mains de leurs ennemis et entre les mains de ceux qui en veulent à leur vie; et leurs cadavres seront la pâture des oiseaux du ciel et des bêtes de la terre.
21 “Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
Et Sédécias, roi de Juda, et ses princes, je les livrerai aux mains de leurs ennemis, aux mains de ceux qui en veulent à leur vie, aux mains de l'armée de Babylone, qui s'est éloignée de vous.
22 Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”
Voici que je donne des ordres, — oracle de Yahweh, — et je vais les ramener contre cette ville; ils combattront contre elle, ils la prendront et la brûleront; et je ferai des villes de Juda un désert sans habitants!

< Yeremia 34 >