< Yeremia 34 >

1 Wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli na jeshi lake lote, pamoja na falme zote na mataifa katika himaya aliyotawala walipokuwa wakipigana dhidi ya Yerusalemu pamoja na miji yote inayoizunguka, neno hili lilimjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word that was maad of the Lord to Jeremye, whanne Nabugodonosor, kyng of Babiloyne, and al his oost, and alle the rewmes of erthe, that weren vndur the power of his hond, and alle puplis fouyten ayens Jerusalem, and ayens alle citees therof; and he seide,
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli, kusema: Nenda kwa Sedekia mfalme wa Yuda umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteketeza kwa moto.
The Lord God of Israel seith these thingis, Go thou, and speke to Sedechie, kyng of Juda; and thou schalt seie to hym, The Lord seith these thingis, Lo! Y schal bitake this citee in to the hond of the kyng of Babiloyne, and he schal brenne it bi fier.
3 Hutaweza kuepuka mkono wake, bali hakika utatekwa na kukabidhiwa kwake. Utamwona mfalme wa Babeli kwa macho yako mwenyewe, naye atazungumza nawe ana kwa ana. Nawe utakwenda Babeli.
And thou schalt not ascape fro his hond, but thou schalt be takun bi takyng, and thou schalt be bitakun in to his hond; and thin iyen schulen se the iyen of the kyng of Babiloyne, and his mouth schal speke with thi mouth, and thou schalt entre in to Babiloyne.
4 “‘Lakini sikia ahadi ya Bwana, ee Sedekia mfalme wa Yuda. Hili ndilo asemalo Bwana kukuhusu: Hutakufa kwa upanga,
Netheles Sedechie, the kyng of Juda, here thou the word of the Lord; the Lord seith these thingis to thee, Thou schalt not die bi swerd,
5 utakufa kwa amani. Kama vile watu walivyowasha moto wa maziko kwa heshima ya baba zako, wafalme waliokutangulia, ndivyo watu watakavyowasha moto kwa heshima yako na kuomboleza, wakisema: “Ole, Ee Bwana!” Mimi mwenyewe ninaweka ahadi hii, asema Bwana.’”
but thou schalt die in pees, and bi the brennyngis of thi fadris, the formere kyngis that weren bifore thee, so thei schulen brenne thee, and thei schulen biweile thee, Wo! lord; for Y spak a word, seith the Lord.
6 Ndipo nabii Yeremia akamwambia Sedekia mfalme wa Yuda mambo haya yote huko Yerusalemu,
And Jeremye, the profete, spak to Sedechie, kyng of Juda, alle these wordis in Jerusalem.
7 wakati jeshi la mfalme wa Babeli lilipokuwa likipigana dhidi ya Yerusalemu na miji mingine ya Yuda ambayo bado ilikuwa imara, yaani Lakishi na Azeka. Hii ilikuwa miji pekee yenye ngome iliyobaki katika Yuda.
And the oost of the kyng of Babiloyne fauyt ayens Jerusalem, and ayens alle the citees of Juda, that weren left; ayens Lachis, and ayens Azecha; for whi these strong citees weren left of the citees of Juda.
8 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, baada ya Mfalme Sedekia kufanya agano na watu wote huko Yerusalemu ili kutangaza uhuru kwa watumwa.
The word that was maad of the Lord to Jeremye, aftir that kyng Sedechie smoot boond of pees with al the puple in Jerusalem,
9 Kila mmoja alipaswa kuwaacha huru watumwa wake wa Kiebrania, wanawake na wanaume. Hakuna yeyote aliyeruhusiwa kumshikilia Myahudi mwenzake kama mtumwa.
and prechide, that ech man schulde delyuere his seruaunt, and ech man his handmaide, an Ebreu man and an Ebru womman fre, and that thei schulden not be lordis of hem, that is, in a Jew, and her brothir.
10 Kwa hiyo maafisa wote na watu walioingia katika agano hili wakakubali kwamba watawaacha huru watumwa wao wa kiume na wa kike, na hawatawashikilia tena kama watumwa. Wakakubali na wakawaacha huru.
Therfor alle the princes and al the puple herden, whiche maden couenaunt, that thei schulden delyuere ech man his seruaunt, and ech man his handmaide fre, and schulde no more be lordis of hem; therfor thei herden, and delyueriden;
11 Lakini baadaye wakabadili mawazo yao, na kuwarudisha wale watumwa waliokuwa wamewaacha huru, wakawafanya tena watumwa.
and thei weren turned aftirward, and drowen ayen her seruauntis, and handmaidis, whiche thei hadden left fre, and thei maden suget in to seruauntis, and in to seruauntessis.
12 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And the word of the Lord was maad of the Lord to Jeremye, and seide,
13 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nilifanya agano na baba zenu nilipowatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Nilisema,
The Lord God of Israel seith these thingis, Y smoot a boond of pees with youre fadris, in the dai in which Y ledde hem out of the lond of Egipt, out of the hous of seruage; and Y seide, Whanne seuene yeeris ben fillid,
14 ‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
ech man delyuere his brother, an Ebreu man, which is seeld to hym, and he schal serue thee sixe yeer, and thou schalt delyuere hym fro thee; and youre fadris herden not me, nether bowiden her eere.
15 Hivi karibuni tu mlitubu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu: Kila mmoja wenu aliwatangazia uhuru Waebrania wake. Hata mlifanya agano mbele zangu ndani ya nyumba iitwayo kwa Jina langu.
And ye ben conuertid to dai, and ye diden that, that is riytful bifore myn iyen, that ye precheden ech man fredom to his frend, and ye maden couenaunt in my siyt, in the hous wherynne my name is clepid to help on that fredom.
16 Lakini sasa mmegeuka na kulinajisi jina langu. Kila mmoja wenu amemrudisha mtumwa wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaacha huru waende zao walikotaka. Mmewalazimisha kuwa watumwa wenu tena.
And ye turneden ayen, and defouliden my name, and ye brouyten ayen ech man his seruaunt, and ech man his handmaide, whiche ye delyueriden, that thei schulden be fre, and of her owne power; and ye maden hem suget, that thei be seruauntis and haundmaidis to you.
17 “Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Hamkunitii mimi. Hamkutangaza uhuru kwa ndugu zenu. Hivyo sasa, ninawatangazia ninyi ‘uhuru,’ asema Bwana: ‘uhuru’ ili kuanguka kwa upanga, tauni na njaa. Nitawafanya mwe chukizo kwa falme zote za dunia.
Therfor the Lord seith thes thingis, Ye herden not me, that ye prechiden fredom, ech man to his brothir, and ech man to his freend; lo! Y preeche to you fredom, seith the Lord, and to swerd, and to hungur, and to pestilence, and Y schal yyue you in to stiryng to alle rewmes of erthe.
18 Watu waliovunja agano langu, na ambao hawakutunza masharti ya agano walilofanya mbele zangu, nitawafanya kama ndama waliyemkata vipande viwili, kisha wakatembea kati ya vile vipande vya huyo ndama.
And Y schal yyue the men, that breken my boond of pees, and kepten not the wordis of boond of pees, to whiche thei assentiden in my siyt, and kepten not the calf, which thei kittiden in to twei partis; and the princes of Juda,
19 Viongozi wa Yuda na Yerusalemu, maafisa wa mahakama, makuhani na watu wote wa nchi waliopita kati ya vile vipande vya ndama,
and the princes of Jerusalem, and the onest seruauntis, and preestis yeden bytwixe the partyngis therof, and al the puple of the lond, that yeden bitwixe the departyngis of the calf;
20 nitawatia mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao. Maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
and Y schal yyue hem in to the hond of her enemyes, and in to the hond of hem that seken her lijf; and the deed careyn of hem schal be in to mete to the volatilis of the eir, and to the beestis of erthe.
21 “Nitamtia Sedekia mfalme wa Yuda na maafisa wake mikononi mwa adui zao wanaotafuta uhai wao, kwa jeshi la mfalme wa Babeli, lililokuwa limeondoka kwenu.
And Y schal yyue Sedechie, the kyng of Juda, and hise princes, in to the hond of her enemyes, and in to the hond of hem that seken her lijf, and in to the hond of the oostis of the kyng of Babiloyne, that yeden awei fro you.
22 Nitatoa amri, asema Bwana, nami nitawarudisha tena katika mji huu. Watapigana dhidi yake, wautwae na kuuteketeza kwa moto. Nami nitaiangamiza miji ya Yuda hivyo pasiwe na yeyote atakayeweza kuishi humo.”
Lo! Y comaunde, seith the Lord, and Y schal brynge hem ayen in to this citee, and thei schulen fiyte ayens it, and schulen take it, and schulen brenne it with fier; and Y schal yyue the citees of Juda in to wildirnesse, for ther is no dwellere.

< Yeremia 34 >