< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
Poleg tega je beseda od Gospoda drugič prišla Jeremiju, medtem ko je bil še zaprt na dvorišču ječe, rekoč:
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
»Tako govori Gospod, ki to dela, Gospod, ki je to oblikoval, da to osnuje, Gospod je njegovo ime.
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
›Kliči k meni in ti bom odgovoril in ti pokazal velike in mogočne stvari, ki jih ne poznaš.‹
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
Kajti tako govori Gospod, Izraelov Bog, glede hiš tega mesta in glede hiš Judovih kraljev, ki so zrušene z okopi in z mečem:
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
›Prišli so, da se borijo s Kaldejci, toda to je, da jih napolnijo s trupli mož, ki sem jih umoril v svoji jezi in v svoji razjarjenosti in svoj obraz sem zaradi vse zlobnosti skril pred tem mestom.
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
Glej, privedel bom zdravje in zdravilo, jih ozdravil in jim razodel obilje miru in resnice.
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
Povzročil bom Judovemu ujetništvu in Izraelovemu ujetništvu, da se vrnejo in jih bom zgradil kakor poprej.
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
Očistil jih bom pred vso njihovo krivičnostjo, s katero so grešili zoper mene, in oprostil jim bom vse njihove krivičnosti, s katerimi so grešili in s katerimi so se pregrešili zoper mene.
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
To mi bo ime radosti, hvala in čast pred vsemi narodi zemlje, ki bodo slišali vse dobro, ki jim ga storim. Bali se bodo in trepetali zaradi vse dobrote in zaradi vsega uspevanja, ki sem ga priskrbel.‹
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
Tako govori Gospod: ›Ponovno se bo na tem kraju, za katerega pravite, [da] bo zapuščen, brez človeka in brez živali, torej v Judovih mestih in na ulicah Jeruzalema, ki so zapuščene, brez človeka in brez naseljenca in brez živali, slišal
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
glas radosti in glas veselja, glas ženina in glas neveste, glas tistih, ki bodo rekli: ›Hvalite Gospoda nad bojevniki, kajti Gospod je dober, kajti njegovo usmiljenje vztraja na veke, ‹ in od teh, ki bodo prinašali žrtev hvale v Gospodovo hišo. Kajti povzročil bom vrnitev ujetništva dežele, kakor na začetku, ‹ govori Gospod.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
Tako govori Gospod nad bojevniki: ›Ponovno bo na tem kraju, ki je zapuščen, brez človeka in brez živali in v vseh njegovih mestih, prebivališče pastirjev, ki bodo svojim tropom povzročali, da se uležejo.
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
V gorskih mestih, v dolinskih mestih, v mestih na jugu, v Benjaminovi deželi, v krajih okoli Jeruzalema in v Judovih mestih bodo tropi ponovno prehajali pod rokama tistega, ki jih prešteva, ‹ govori Gospod.
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
›Glej, prihajajo dnevi, ‹ govori Gospod, ›da bom izpolnil to dobro stvar, ki sem jo obljubil Izraelovi hiši in Judovi hiši.
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
V tistih dneh in v tistem času, bom povzročil, da Davidu zraste Mladika pravičnosti, in on bo izvršil sodbo in pravičnost v deželi.
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
V tistih dneh bo Juda rešen in [prestolnica] Jeruzalem bo varno prebivala, in to je ime, s katerim bo imenovana: › Gospod, naša pravičnost.‹
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
Kajti tako govori Gospod: ›Davidu nikoli ne bo manjkalo moža, da sedi na prestolu Izraelove hiše,
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
niti ne bo duhovnikom Lévijevcem manjkal mož pred menoj, da daruje žgalne daritve in da vžiga jedilne daritve in da opravlja nenehno klavno daritev.‹«
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Gospodova beseda je prišla Jeremiju, rekoč:
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
»Tako govori Gospod: ›Če lahko prelomite mojo zavezo dneva in mojo zavezo noči in da ne bo več dneva in noči v njunem obdobju,
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
potem bo lahko tudi moja zaveza z Davidom, mojim služabnikom, prelomljena, da ne bi imel sina, da kraljuje na njegovem prestolu, in z duhovniki Lévijevci, mojimi služabniki.
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
Kakor vojska neba ne more biti prešteta niti morski pesek izmerjen, tako bom pomnožil seme Davida, svojega služabnika in Lévijevce, ki mi služijo.‹«
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Poleg tega je Gospodova beseda prišla Jeremiju, rekoč:
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
»Mar ne preudarjaš tega, kar je to ljudstvo govorilo, rekoč: ›Dve družini, ki ju je Gospod izbral, je celó zavrgel?‹ Tako so prezirali moje ljudstvo, da ne bi bilo več narod pred njimi.‹
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
Tako govori Gospod: ›Če ne bi bilo moje zaveze z dnevom in nočjo in če ne bi določil odredb o nebu in zemlji,
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
potem bom zavrgel Jakobovo seme in Davida, svojega služabnika, tako da ne bom vzel nobenega iz njegovega semena, da bi bili vladarji nad semenom Abrahama, Izaka in Jakoba, kajti njihovemu ujetništvu bom povzročil, da se vrnejo in se jih bom usmilil.‹«

< Yeremia 33 >