< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
Et la parole du Seigneur fut adressée à Jérémie une seconde fois, lorsqu’il était encore enfermé dans le vestibule de la prison, disant:
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
Voici ce que dit le Seigneur, qui doit faire, et disposer, et préparer cela; le Seigneur est son nom.
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
Crie vers moi, et je t’exaucerai, et je t’annoncerai des choses grandes et certaines que tu ne sais pas.
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
Parce que voici ce que dit le Seigneur, Dieu d’Israël, aux maisons de cette ville et aux maisons du roi de Juda qui ont été détruites, et aux fortifications et au glaive
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
De ceux qui viennent, afin de combattre contre les Chaldéens, et afin de les remplir des cadavres des hommes que j’ai frappés dans ma fureur et dans mon indignation, détournant ma face de cette cité à cause de toute leur malice:
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
Voici que moi, je refermerai leur cicatrice, je leur donnerai la santé et je les soignerai; et je leur montrerai la paix et la vérité qu’ils demandent.
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
Et je ferai retourner certainement Juda et Jérusalem; et je les établirai comme dès le commencement.
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
Et je les purifierai de toute leur iniquité par laquelle ils ont péché contre moi, et je leur pardonnerai toutes leurs iniquités par lesquelles ils se sont rendus coupables envers moi, et m’ont méprisé.
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
Ce sera pour moi un renom, et une joie, et une louange, et une exultation parmi toutes les nations de la terre, qui apprendront tous les biens que moi je dois leur faire; et elles auront peur et elles seront troublées à cause de tous les biens et de toute la paix que moi je leur accorderai.
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
Voici ce que dit le Seigneur: On entendra encore dans ce lieu (que vous dites être un désert, parce qu’il n’y a pas d’homme ni de bête, dans les cités de Juda et au dehors de Jérusalem, cités qui sont désolées, sans homme et sans habitant, et sans troupeau)
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
La voix de la joie et la voix de l’allégresse, la voix de l’époux et la voix de l’épouse, la voix de ceux qui diront: Louez le Seigneur des armées parce que bon est le Seigneur, parce qu’éternelle est sa miséricorde, et la voix de ceux qui portent des vœux dans la maison du Seigneur; car je ramènerai les captifs de cette terre, et je les rétablirai comme dès le commencement, dit le Seigneur.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
Voici ce que dit le Seigneur des armées: Il y aura encore dans ce lieu désert, sans homme et sans bête, et dans toutes ses cités, une demeure de pasteurs qui feront reposer des troupeaux.
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
Dans les cités des montagnes, et dans les cités de la plaine, et dans les cités qui sont au midi, et dans la terre de Benjamin, et dans les environs de Jérusalem, et dans les cités de Juda, les troupeaux passeront encore sous la main de celui qui les compte, dit le Seigneur.
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
Voilà que des jours viennent, dit le Seigneur, et je réaliserai la bonne parole que j’ai dite à la maison d’Israël et à la maison de Juda.
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
En ces jours-là et en ce temps-là, je ferai germer dans David un germe de justice; et il rendra le jugement et la justice sur la terre.
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
En ces jours-là, Juda sera sauvé, et Jérusalem habitera en assurance; et voici le nom dont ils l’appelleront: Le Seigneur notre juste.
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
Car voici ce que dit le Seigneur: Il ne manquera pas dans la race de David, d’homme qui s’asseye sur le trône de la maison d’Israël.
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
Et d’entre les prêtres et d’entre les Lévites, il ne manquera pas un homme devant ma face qui offre des holocaustes, allume le sacrifice, et tue des victimes, tous les jours.
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Et la parole du Seigneur fut adressée à Jérémie, disant:
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
Voici ce que dit le Seigneur: Si mon alliance avec le jour et mon alliance avec la nuit peuvent être rendues vaines, en sorte qu’il n’y ait pas de jour et de nuit en leurs temps,
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
Mon alliance avec David, mon serviteur, pourra aussi être vaine, en sorte qu’il n’y ait pas de lui un fils qui règne sur son trône, ni de Lévites et de prêtres qui soient mes ministres.
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
Comme les étoiles du ciel ne peuvent être comptées, ni le sable de la mer être mesuré, ainsi je multiplierai la race de David, mon serviteur, et les Lévites, mes ministres.
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Et la parole du Seigneur fut adressée à Jérémie, disant:
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
Est-ce que tu n’as pas vu comment a parlé ce peuple, disant: Les deux familles qu’avait choisies le Seigneur ont été rejetées; et ils ont méprisé mon peuple, parce qu’il n’est plus une nation devant eux?
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
Voici ce que dit le Seigneur: Si je n’ai pas établi mon alliance entre le jour et la nuit, et des lois pour le ciel et pour la terre,
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
Certainement, je rejetterai aussi la race de Jacob et de David, mes serviteurs, afin de ne pas prendre de leur race des princes de la race d’Abraham, d’Isaac et de Jacob; car je ramènerai leurs captifs, et j’aurai pitié d’eux.

< Yeremia 33 >