< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
And the word of the Lord was maad to Jeremye, in the secounde tyme, whanne he was closid yit in the porche of the prisoun, and seide,
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
The Lord seith these thingis, The Lord is name of hym, that schal do, and fourme, and make redi that thing;
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
Crye thou to me, and Y schal here thee, and Y schal telle to thee grete thingis, and stidfast, whiche thou knowist not.
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
For the Lord God of Israel seith these thingis to the housis of this citee, and to the housis of the kyng of Juda, that ben distried, and to the strengthingis,
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
and to the swerd of men comynge to fiyte with Caldeis, and to fille tho housis with careyns of men, which Y smoot in my strong veniaunce, and in myn indignacioun; and Y hidde my face fro this citee, for al the malice of hem.
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
Lo! Y schal close togidere to hem a wounde and helthe, and Y schal make hem hool, and Y schal schewe to hem the bisechyng of pees and of treuthe;
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
and Y schal conuerte the conuersioun of Juda, and Y schal conuerte the conuersioun of Jerusalem, and Y schal bilde hem, as at the bigynnyng.
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
And Y schal clense hem fro al her wickidnesse, in which thei synneden to me, and Y schal be merciful to alle the wickidnessis of hem, in which thei trespassiden to me, and forsoken me.
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
And thei schulen be to me in to a name, and in to ioye, and in to heriyng, and in to ful out ioiyng to alle folkis of erthe, that herden alle the goodis whiche Y schal do to hem; and thei schulen drede, and schulen be disturblid in alle goodis, and in al the pees, which Y schal do to hem.
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
The Lord seith these thingis, Yit in this place, which ye seien to be forsakun, for no man is nether beeste in the citees of Juda, and in the yatis of Jerusalem, that ben desolat, without man, and with out dwellere,
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
and with out beeste, the vois of ioye schal be herd, and the vois of gladnesse, the vois of spouse, and the vois of spousesse, the vois of men, seiynge, Knowleche ye to the Lord of oostis, for the Lord is good, for his merci is with outen ende, and of men berynge vowis in to the hous of the Lord; for Y schal brynge ayen the conuersioun of the lond, as at the bigynnyng, seith the Lord.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
The Lord of oostis seith these thingis, Yit in this forsakun place, with out man, and with out beeste, and in alle citees therof, schal be a dwellyng place of scheepherdis, of flockis ligynge.
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
And in the citees in hilli places, and in the citees in feeldi places, and in the citees that ben at the south, and in the lond of Beniamyn, and in the cumpas of Jerusalem, and in the citees of Juda, yit flockis schulen passe, at the hond of the noumbrere, seith the Lord.
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
Lo! daies comen, seith the Lord, and Y schal reise the good word, which Y spak to the hous of Israel, and to the hous of Juda.
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
In tho daies, and in that tyme, Y schal make the seed of riytfulnesse to buriowne to Dauid, and he schal make doom and riytfulnesse in erthe.
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
In tho daies Juda schal be sauyd, and Israel schal dwelle tristili; and this is the name which thei schulen clepe hym, Oure riytful Lord.
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
For the Lord seith these thingis, A man of Dauid schal not perische, that shal sitte on the trone of the hous of Israel;
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
and of preestis and dekenes a man schal not perische fro my face, that schal offre brent sacrifices, and brenne sacrifice, and sle sacrifice, in alle daies.
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And the word of the Lord was maad to Jeremye,
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
and seide, The Lord seith these thingis, If my couenaunt with the dai and my couenaunt with the niyt mai be maad voide, that the dai and the niyt be not in his tyme;
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
and my couenaunt with Dauid, my seruaunt, mai be voide, that of hym be no sone, that schal regne in his trone, and no dekenes, and preestis, my mynistris;
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
as the sterris of heuene moun not be noumbrid, and the grauel of the see mai not be metun, so Y schal multiplie the seed of Dauid, my seruaunt, and dekenes, my mynystris.
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And the word of the Lord was maad to Jeremye, and seide, Whether thou hast not seyn,
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
that this puple spak, seiynge, Twei kynredis whiche the Lord chees, ben cast awei, and thei dispisiden my puple, for it is no more a folc bifore hem.
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
The Lord seith these thingis, If Y settide not my couenaunt bitwixe dai and niyt, and if Y settide not lawis to heuene and erthe;
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
sotheli and Y schal caste awei the seed of Jacob, and of Dauid, my seruaunt, that Y take not of the seed of hym princes, of the seed of Abraham, of Isaac, and of Jacob; for Y schal brynge ayen the conuersioun of hem, and Y schal haue merci on hem.

< Yeremia 33 >