< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
and to be word LORD to(wards) Jeremiah second and he/she/it still he to restrain in/on/with court [the] guardhouse to/for to say
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
thus to say LORD to make her LORD to form: formed [obj] her to/for to establish: establish her LORD name his
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
to call: call to to(wards) me and to answer you and to tell to/for you great: large and to gather/restrain/fortify not to know them
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
for thus to say LORD God Israel upon house: home [the] city [the] this and upon house: home king Judah [the] to tear to(wards) [the] mound and to(wards) [the] sword
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
to come (in): come to/for to fight with [the] Chaldea and to/for to fill them with corpse [the] man which to smite in/on/with face: anger my and in/on/with rage my and which to hide face my from [the] city [the] this upon all distress: evil their
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
look! I to ascend: establish to/for her health and healing and to heal them and to reveal: reveal to/for them abundance peace: well-being and truth: certain
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
and to return: rescue [obj] captivity Judah and [obj] captivity Israel and to build them like/as in/on/with first
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
and be pure them from all iniquity: guilt their which to sin to/for me and to forgive (to/for all *Q(K)*) iniquity: guilt their which to sin to/for me and which to transgress in/on/with me
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
and to be to/for me to/for name rejoicing to/for praise and to/for beauty to/for all nation [the] land: country/planet which to hear: hear [obj] all [the] welfare which I to make: do [obj] them and to dread and to tremble upon all [the] welfare and upon all [the] peace: well-being which I to make: offer to/for her
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
thus to say LORD still to hear: hear in/on/with place [the] this which you(m. p.) to say desolate he/she/it from nothing man and from nothing animal in/on/with city Judah and in/on/with outside Jerusalem [the] be desolate: destroyed from nothing man and from nothing to dwell and from nothing animal
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
voice rejoicing and voice joy voice son-in-law and voice daughter-in-law: bride voice to say to give thanks [obj] LORD Hosts for pleasant LORD for to/for forever: enduring kindness his to come (in): bring thanksgiving house: temple LORD for to return: rescue [obj] captivity [the] land: country/planet like/as in/on/with first to say LORD
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
thus to say LORD Hosts still to be in/on/with place [the] this [the] desolate from nothing man and till animal and in/on/with all city his pasture to pasture to stretch flock
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
in/on/with city [the] mountain: hill country in/on/with city [the] Shephelah and in/on/with city [the] Negeb and in/on/with land: country/planet Benjamin and in/on/with around Jerusalem and in/on/with city Judah still to pass [the] flock upon hand to count to say LORD
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
behold day to come (in): come utterance LORD and to arise: establish [obj] [the] word: promised [the] pleasant which to speak: promise to(wards) house: household Israel and upon house: household Judah
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
in/on/with day [the] they(masc.) and in/on/with time [the] he/she/it to spring to/for David branch righteousness and to make: do justice and righteousness in/on/with land: country/planet
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
in/on/with day [the] they(masc.) to save Judah and Jerusalem to dwell to/for security and this which to call: call by to/for her LORD Righteousness our
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
for thus to say LORD not to cut: lack to/for David man to dwell upon throne house: household Israel
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
and to/for priest [the] Levi not to cut: lack man from to/for face: before my to ascend: offer up burnt offering and to offer: burn offering and to make sacrifice all [the] day: always
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
and to be word LORD to(wards) Jeremiah to/for to say
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
thus to say LORD if to break [obj] covenant my [the] day and [obj] covenant my [the] night and to/for lest to be by day and night in/on/with time their
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
also covenant my to break with David servant/slave my from to be to/for him son: descendant/people to reign upon throne his and with [the] Levi [the] priest to minister me
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
which not to recount army [the] heaven and not to measure sand [the] sea so to multiply [obj] seed: children David servant/slave my and [obj] [the] Levi to minister [obj] me
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
and to be word LORD to(wards) Jeremiah to/for to say
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
not to see: see what? [the] people [the] this to speak: speak to/for to say two [the] family which to choose LORD in/on/with them and to reject them and [obj] people my to spurn [emph?] from to be still nation to/for face: before their
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
thus to say LORD if not covenant my by day and night statute heaven and land: country/planet not to set: make
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
also seed: children Jacob and David servant/slave my to reject from to take: take from seed: children his to rule to(wards) seed: children Abraham Isaac and Jacob for (to return: rescue *Q(K)*) [obj] captivity their and to have compassion them

< Yeremia 33 >