< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
And it came [the] word of Yahweh to Jeremiah a second [time] and he still he [was] shut up in [the] courtyard of the guard saying.
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
Thus he says Yahweh [who] made it Yahweh [who] formed it to establish it [is] Yahweh name his.
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
Call to me and I will answer you and I will tell to you great [things] and incomprehensible [things] [which] not you know them.
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
For thus he says Yahweh [the] God of Israel on [the] houses of the city this and on [the] houses of [the] kings of Judah which have been pulled down because of the mounds and because of the sword.
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
Going to fight with the Chaldeans and to fill them with [the] corpses of humankind which I struck down in anger my and in rage my and whom I have hidden face my from the city this on all evil their.
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
Here I [will] bring up for it healing and healing and I will heal them and I will uncover to them an abundance of well-being and faithfulness.
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
And I will turn back [the] captivity of Judah and [the] captivity of Israel and I will rebuild them as at the former [time].
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
And I will cleanse them from all iniquity their which they have sinned to me and I will forgive (all *Q(K)*) iniquities their which they have sinned to me and which they have rebelled against me.
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
And it will become to me a name of joy praise and honor to all [the] nations of the earth who they will hear all the good which I [will be] doing them and they will be in awe and they will tremble on all the good and on all the well-being which I [will be] doing for it.
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
Thus - he says Yahweh again it will be heard in the place this which you [are] saying [is] desolate it from not human being and from not animal in [the] cities of Judah and in [the] streets of Jerusalem which are made desolate from not human being and from not inhabitant and from not animal.
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
[the] sound of Joy and [the] sound of gladness [the] sound of a bridegroom and [the] sound of a bride [the] sound of [those who] say give thanks to Yahweh of hosts for [is] good Yahweh for [is] for ever covenant loyalty of his [those who] bring a thank-offering [the] house of Yahweh for I will turn back [the] captivity of the land as at the former [time] he says Yahweh.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
Thus he says Yahweh of hosts again it will be - in the place this desolate from not human being and unto an animal and in all cities its pasture of shepherds [who] make to lie down flock[s].
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
In [the] cities of the hill country in [the] cities of the Shephelah and in [the] cities of the Negev and in [the] land of Benjamin and in [the] surroundings of Jerusalem and in [the] cities of Judah again they will pass the flock on [the] hands of [one who] counts he says Yahweh.
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
Here! days [are] coming [the] utterance of Yahweh and I will carry out the word good which I have spoken to [the] house of Israel and to [the] house of Judah.
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
In the days those and at the time that I will cause to sprout for David a branch of righteousness and he will do justice and righteousness in the land.
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
In the days those it will be saved Judah and Jerusalem it will dwell to security and this [is that] which anyone will call it Yahweh - [is] righteousness our.
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
For thus he says Yahweh not it will be cut off to David a man [who] sits on [the] throne of [the] house of Israel.
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
And to the priests the Levites not it will be cut off a man from to before me [who] offers up a burnt offering and [who] makes smoke a grain offering and [who] makes a sacrifice all the days.
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to Jeremiah saying.
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
Thus he says Yahweh if you will break covenant of my the day and covenant of my the night and to not to be daytime and night at appropriate time their.
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
Also covenant my it will be broken with David servant my from belonging to him a son [who] reigns on throne his and with the Levites the priests servants my.
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
Which not it will be counted [the] host of the heavens and not it will be measured [the] sand of the sea so I will increase [the] offspring of David servant my and the Levites [the] servants of me.
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And it came [the] word of Yahweh to Jeremiah saying.
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
¿ Not have you seen what? the people this have they said saying [the] two the clans which he chose Yahweh them and he has rejected them and people my they spurn! from being again a nation before them.
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
Thus he says Yahweh if not covenant of my daytime and night [the] fixed order of heaven and earth not I have ordained.
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
Also [the] offspring of Jacob and David servant my I will reject from taking any of offspring his rulers to [the] offspring of Abraham Isaac and Jacob for (I will cause to turn back *Q(K)*) captivity their and I will have compassion on them.

< Yeremia 33 >