< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
The word of Jehovah came also to Jeremiah the second time, while he was shut up in the court of the prison, and said: —
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
Thus saith Jehovah, who doeth it, Jehovah who disposeth it, to establish it; Jehovah is his name.
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
Call to me, and I will answer thee, And I will show thee great things, And hidden things which thou knowest not.
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
For thus saith Jehovah, the God of Israel, Concerning the houses of this city, And concerning the houses of the kings of Judah, Which are thrown down toward the mounds and the sword,
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
To fight with the Chaldaeans, And to fill them with the dead bodies of men, Whom I have smitten in mine anger and in my wrath, And for all whose wickedness I have hid my face from this city:
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
Behold, I will bind up her wounds, and heal them, And I will reveal to them abundance of peace and stability.
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
And I will bring back the captives of Judah, And the captives of Israel, And I will build them, as at the first.
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
And I will cleanse them from all their iniquity, Whereby they have sinned against me; And I will forgive all their iniquities, Whereby they have sinned, And have rebelled against me.
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
And it [[the city]] shall be to me a name of joy, A praise and a glory among all the nations of the earth, Who shall hear of all the good which I do to them. And they shall fear and tremble because of all the good, And because of all the prosperity, which I bestow upon it.
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
Thus saith Jehovah: Yet again shall be heard in this place, Of which ye say, “It is desolate, without man and without beast,” In the cities of Judah, and in the streets of Jerusalem, Which are desolate, without man, Even without an inhabitant and without beast,
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
The voice of joy and the voice of gladness, The voice of the bridegroom and the voice of the bride, The voice of them that say, “Praise ye Jehovah of hosts, For Jehovah is good, For his mercy endureth forever!” And of them that bring an offering of praise to the house of Jehovah. For I will restore the captives of the land, As at the first, saith Jehovah.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
Thus saith Jehovah of hosts: Yet again shall there be in this place, Which is desolate, without man and without beast, And in all the cities thereof, A habitation of shepherds, who shall cause their flocks to rest;
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
In the cities of the hill-country, and in the cities of the plain, And in the cities of the south, and in the land of Benjamin, And in the places about Jerusalem, and in the cities of Judah, Shall the flocks pass yet again Under the hands of him that numbereth them, saith Jehovah.
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
Behold, the days come, saith Jehovah, That I will perform that good thing Which I have spoken concerning the house of Israel, And concerning the house of Judah.
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
In those days and at that time Will I cause to grow up from David a righteous branch, Who shall maintain justice and equity in the land.
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
In those days shall Judah be saved, And Jerusalem shall dwell securely; And this is the name which shall be given her, Jehovah-is-our-salvation.
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
For thus saith Jehovah: There shall never fail from David A man to sit upon the throne of the house of Israel;
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
Neither from the priests and the Levites Shall a man fail before me, To offer burnt-offerings, and to kindle meat-offerings, And to perform sacrifice continually.
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And the word of Jehovah came to Jeremiah and said,
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
Thus saith Jehovah: If ye can break my covenant concerning the day, And my covenant concerning the night, So that there shall no more be day and night in their season,
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
Then also may my covenant with David my servant be broken, So that he shall not have a son to reign upon his throne, And with the Levites, the priests, my servants.
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
As the host of heaven cannot be numbered, Nor the sand of the sea measured, So will I multiply the posterity of David my servant, And the Levites who minister to me.
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
The word of Jehovah came also to Jeremiah, saying:
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
Seest thou not what this people speaketh, saying, “The two families, which Jehovah chose, he hath cast off”? Therefore they despise my people, So that they are no more a people in their eyes.
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
Thus saith Jehovah: If my covenant concerning the day and the night be not maintained, And if I have not established the ordinances of the heaven and the earth,
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
Then will I cast away the posterity of Jacob, and of David, my servant, So as not to take of his posterity to be rulers Over the posterity of Abraham, Isaac, and Jacob; For I will bring them back from their captivity, And have mercy upon them.

< Yeremia 33 >