< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
And there is a word of YHWH to Jeremiah a second time—and he [is] yet detained in the court of the prison—saying:
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
“Thus said YHWH who has made it, YHWH who has formed it, to establish it, YHWH [is] His Name:
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
Call to Me, and I answer you, indeed, I declare to you great and inaccessible things—you have not known them.
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
For thus said YHWH, God of Israel, concerning the houses of this city, and concerning the houses of the kings of Judah that are broken down for the [siege] mounds, and for the tool;
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
they are coming to fight with the Chaldeans, and to fill them with the carcasses of men, whom I have struck in My anger, and in My fury, and [for] whom I have hidden My face from this city, because of all their evil:
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
Behold, I am increasing health and cure to it, And have healed them, and revealed to them The abundance of peace and truth.
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
And I have turned back the captivity of Judah, And the captivity of Israel, And I have built them as at the first,
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
And cleansed them from all their iniquity That they have sinned against Me, And I have pardoned all their iniquities That they have sinned against Me, And that they transgressed against Me.
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
And it has been for a name of joy to Me, For praise, and for beauty, to all nations of the earth, Who hear of all the good that I am doing them, And they have feared, And they have trembled for all the good, And for all the peace, that I am doing to it.”
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
Thus said YHWH: “Again is heard in this place—of which you are saying, It [is] dry, without man and without beast, In cities of Judah, and in streets of Jerusalem, That are desolated, without man, And without inhabitant, and without beast—
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
A voice of joy and a voice of gladness, Voice of bridegroom and voice of bride, The voice of those saying, Thank YHWH of Hosts, for YHWH [is] good, For His kindness [is] for all time, Who are bringing in thanksgiving to the house of YHWH, For I return the captivity of the land, As at the first,” said YHWH.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
Thus said YHWH of Hosts: “Again there is in this place—that is dry, Without man and beast, And in all its cities—a habitation of shepherds, Causing the flock to lie down.
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
In the cities of the hill-country, In the cities of the low country, And in the cities of the south, And in the land of Benjamin, And in the outskirts of Jerusalem, And in the cities of Judah, Again the flock passes by under the hands of the numberer,” said YHWH.
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
“Behold, days are coming,” a declaration of YHWH, “And I have established the good word That I spoke to the house of Israel, And concerning the house of Judah.
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
In those days, and at that time, I cause a Shoot of righteousness to shoot up to David, And He has done judgment and righteousness in the earth.
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
In those days Judah is saved, And Jerusalem dwells confidently, And this [is] what she is called: YHWH [is] Our Righteousness.”
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
For thus said YHWH: “A man sitting on the throne of the house of Israel [is] never cut off from David,
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
And to the priests—the Levites, A man is not cut off from before My face, Causing a burnt-offering to ascend, And perfuming a present, and making sacrifice—all the days.”
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And there is a word of YHWH to Jeremiah, saying,
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
“Thus said YHWH: If you can break My covenant with the day, And My covenant with the night, So that they are not daily and nightly in their season,
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
My covenant is also broken with My servant David, So that he does not have a son reigning on his throne, And with the Levites the priests, My ministers.
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
As the host of the heavens is not numbered, Nor the sand of the sea measured, So I multiply the seed of My servant David, And My ministers the Levites.”
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And there is a word of YHWH to Jeremiah, saying,
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
“Have you not considered what this people have spoken, saying, The two families on which YHWH fixed, He rejects them? And they despise My people, so that they are no longer a people before them!”
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
Thus said YHWH: “If My covenant [is] not with day and night, [And if] I have not appointed the statutes of the heavens and earth—
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
I also reject the seed of Jacob, and My servant David, From taking rulers from his seed For the seed of Abraham, Isaac, and Jacob, For I return their captivity, and have pitied them.”

< Yeremia 33 >