< Yeremia 33 >

1 Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
And the word of the Lord came to Jeremias the second time, while he was yet shut up in the court of the prison, saying:
2 “Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
Thus saith the Lord, who will do, and will form it, and prepare it, the Lord is his name.
3 ‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
Cry to me and I will hear thee: and I will shew thee great things, and sure things which thou knowest not.
4 Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
For thus saith the Lord the God of Israel to the houses of this city, and to the houses of the king of Juda, which rue destroyed, and to the bulwarks, and to the sword.
5 katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
Of them that come to fight with the Chaldeans, and to fill them with the dead bodies of the men whom I have slain in my wrath, and in my indignation, hiding my face from this city because of all their wickedness.
6 “‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
Behold I will close their wounds and give them health, and I will cure them: and I will reveal to them the prayer of peace and truth.
7 Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
And I will bring back the captivity of Juda, and the captivity of Jerusalem: and I will build them as from the beginning.
8 Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
And I will cleanse them from all their iniquity, whereby they have sinned against me: and I will forgive all their iniquities, whereby they have sinned against me, and despised me.
9 Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
And it shall be to me a name, and a joy, and a praise, and a gladness before all the nations of the earth, that shall hear of all the good things which I will do to them: and they shall fear and be troubled for all the good things, and for all the peace that I will make for them.
10 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
Thus saith the Lord: There shall be heard again in this place (which you say is desolate, because there is neither man nor beast: in the cities of Juda, and without Jerusalem, which are desolate without man, and without inhabitant, and without beast)
11 sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
The voice of joy and the voice of gladness, the voice of the bridegroom and the voice of the bride, the voice of them that shall say: Give ye glory to the Lord of hosts, for the Lord is good, for his mercy endureth for ever: and of them that shall bring their vows into the house of the Lord: for I will bring back the captivity of the land as at the first, saith the Lord.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
Thus saith the Lord of hosts: There shall be again in this place that is desolate without man, and without beast, and in all the cities thereof, an habitation of shepherds causing their flocks to lie down.
13 Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
And in the cities on the mountains, and in the cities of the plains, and in the cities that are towards the south: and in the land of Benjamin, and round about Jerusalem, and in the cities of Juda shall the flocks pass again under the hand of him that numbereth them, saith the Lord.
14 “‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
Behold the days come, saith the Lord, that I will perform the good word that I have spoken to the house of Israel, and to the house of Juda.
15 “‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
In those days, and at that time, I will make the bud of justice to spring forth unto David, and he shall do judgment and justice in the earth.
16 Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
In those days shall Juda be saved, and Jerusalem shall dwell securely: and this is the name that they shall call him, The Lord our just one.
17 Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
For thus saith the Lord: There shall not be cut off from David a man to sit upon the throne of the house of Israel.
18 wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
Neither shall there be cut off from the priests and Levites a man before my face to offer holocausts, and to burn sacrifices, and to kill victims continually:
19 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And the word of the Lord came to Jeremias, saying:
20 “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
Thus saith the Lord: If my covenant with the day can be made void, and my covenant with the night, that there should not be day and night in their season:
21 basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
Also my covenant with David my servant may be made void, that he should not have a son to reign upon his throne, and with the Levites and priests my ministers.
22 Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
As the stars of heaven cannot be numbered, nor the sand of the sea be measured: so will I multiply the seed of David my servant, and the Levites my ministers.
23 Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
And the word of the Lord came to Jeremias, saying:
24 “Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
Hast thou not seen what this people hath spoken, saying: The two families which the Lord had chosen, are cast off: and they have despised my people, so that it is no more a nation before them?
25 Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
Thus saith the Lord: If I have not set my covenant between day and night, and laws to heaven and earth:
26 basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”
Surely I will also cast; off the seed of Jacob, and of David my servant, so as not to take any of his seed to be rulers of the seed of Abraham, Isaac, and Jacob: for I will bring back their captivity, and will have mercy on them.

< Yeremia 33 >