< Yeremia 32 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Nebukadneza.
Parole qui fut adressée à Jérémie par le Seigneur en la dixième année de Sédécias, roi de Juda; c’est la dix-huitième année de Nabuchodonosor.
2 Wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi katika jumba la kifalme la Yuda.
Alors l’armée du roi de Babylone assiégeait Jérusalem; et Jérémie le prophète était enfermé dans le vestibule de la prison qui était dans la maison du roi de Juda.
3 Basi Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga huko akisema, “Kwa nini unatabiri hivyo? Wewe unasema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteka.
Car Sédécias, roi de Juda, l’avait enfermé, disant: Pourquoi prophétises-tu, disant: Voici ce que dit le Seigneur: Voilà que moi je livrerai cette ville entre les mains du roi de Babylone, et il la prendra?
4 Sedekia mfalme wa Yuda hataweza kuponyoka mikononi mwa Wakaldayo, lakini kwa hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atazungumza naye ana kwa ana na kumwona kwa macho yake mwenyewe.
Et Sédécias, roi de Juda, n’échappera pas à la main des Chaldéens; mais il sera livré entre les mains du roi de Babylone; et sa bouche parlera à sa bouche, et ses yeux verront ses yeux.
5 Atamchukua Sedekia hadi Babeli, mahali atakapoishi mpaka nitakapomshughulikia, asema Bwana. Kama utapigana dhidi ya Wakaldayo, hutashinda.’”
Et il mènera Sédécias à Babylone; et il y sera jusqu’à ce que je le visite, dit le Seigneur; mais, si vous combattez contre les Chaldéens, vous n’aurez aucun succès.
6 Yeremia akasema, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
Et Jérémie dit: La parole du Seigneur m’a été adressée, disant:
7 Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako atakuja kwako na kusema, ‘Nunua shamba langu huko Anathothi, kwa sababu wewe kama jamaa ya karibu ni haki na wajibu wako kulinunua.’
Voilà qu’Hanaméel, fils de Sellum, ton cousin germain, viendra vers toi, disant: Achète-toi mon champ qui est à Anathoth, parce que c’est à toi qu’il appartient de l’acheter, à cause de ta parenté.
8 “Kisha, kama Bwana alivyosema, binamu yangu Hanameli alinijia katika ua wa walinzi na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini. Kwa kuwa ni haki yako kulikomboa na kulimiliki, jinunulie.’ “Nilijua kwamba hili lilikuwa neno la Bwana.
Et Hanaméel, fils de mon oncle, vint à moi, selon la parole du Seigneur, dans le vestibule de la prison, et il me dit: Prends possession de mon champ qui est à Anathoth, en la terre de Benjamin; parce que c’est à toi qu’il appartient de prendre possession de cet héritage, car tu es le proche parent. Or je compris que c’était la parole du Seigneur.
9 Hivyo nikalinunua shamba hilo lililoko Anathothi kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nami nikampimia shekeli kumi na saba za fedha.
Et j’achetai d’Hanaméel, fils de mon oncle, le champ qui est à Anathoth; et je lui pesai l’argent, sept statères et dix pièces d’argent.
10 Nikatia sahihi na kuweka muhuri hati ya kumiliki, nikaweka mashahidi, na kupima ile fedha kwenye mizani.
Et j’écrivis sur la feuille et je la scellai et, je pris des témoins; et je pesai l’argent dans une balance.
11 Nikachukua ile hati ya kununulia, nakala iliyotiwa muhuri yenye makubaliano na masharti, pia pamoja na ile nakala isiyo na muhuri,
Et je pris la feuille d’acquisition scellée, et les stipulations, et ce qui était convenu, et les sceaux mis en dehors.
12 nami nikampa Baruku mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, hati hii mbele ya binamu yangu Hanameli, na mbele ya mashahidi waliokuwa wameweka sahihi kwenye hati hii na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ua wa walinzi.
Et je donnai la feuille d’acquisition à Baruch, fils de Néri, fils de Maasias, sous les yeux d’Hanaméel, mon cousin germain, sous les yeux des témoins qui étaient inscrits sur la feuille d’achat., sous les yeux et en présence de tous les Juifs qui étaient assis dans le vestibule de la prison.
13 “Nilimpa Baruku maelezo haya mbele yao:
Et j’ordonnai à Baruch devant eux, disant:
14 ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Chukua hati hizi, yaani nakala zote zenye muhuri na zisizo na muhuri za hati ya kununulia, na uziweke kwenye gudulia la udongo wa mfinyanzi ili zidumu kwa muda mrefu.
Voici ce que dit le Seigneur des armées. Dieu d’Israël: Prends ces feuilles, cette feuille d’achat scellée, et cette feuille qui est ouverte; et mets-les dans un vase de terre, afin qu’elles puissent se conserver durant de longs jours.
15 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nyumba, mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’
Car voici ce que dit le Seigneur des armées, Dieu d’Israël: On acquerra encore des maisons, des champs et des vignes en cette terre.
16 “Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria hii hati ya kununulia, nilimwomba Bwana:
Et je priai le Seigneur, après que j’eus donné le feuillet d’acquisition à Baruch, fils de Néri, disant:
17 “Ee Bwana Mwenyezi, umeumba mbingu na nchi kwa uwezo wako mkuu na kwa mkono ulionyooshwa. Hakuna jambo lililo gumu usiloliweza.
Hélas! hélas! hélas! Seigneur mon Dieu, voilà que vous avez fait le ciel et la terre par votre grande puissance et par votre bras étendu; aucune chose ne vous sera difficile;
18 Wewe huonyesha upendo kwa maelfu, lakini huleta adhabu kwa ajili ya dhambi za baba mapajani mwa watoto wao baada yao. Ee Mungu mkuu na mwenye uweza, ambaye jina lako ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,
Vous qui faites miséricorde à des milliers de créatures, et qui rendez l’iniquité des pères dans le sein de leurs fils après eux, ô le très fort, le grand, et le puissant, le Seigneur des armées est votre nom.
19 makusudi yako ni makuu, na matendo yako ni yenye uwezo. Macho yako yanaona njia zote za wanadamu, nawe humlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake, na kama yanavyostahili matendo yake.
Vous êtes grand dans vos conseils, et incompréhensible dans vos pensées; vous dont les yeux sont ouverts sur toutes les voies des fils d’Adam, afin de rendre à chacun selon ses voies et selon le fruit de ses inventions.
20 Ulitenda ishara za miujiza na maajabu huko Misri, na umeyaendeleza mpaka leo, katika Israeli na miongoni mwa wanadamu wote, nawe umejulikana na kufahamika hivyo mpaka leo.
C’est vous qui avez fait jusqu’à ce jour des signes et des prodiges dans la terre d’Egypte, en Israël et parmi les hommes, et vous avez rendu votre nom célèbre comme il est en ce jour.
21 Uliwatoa watu wako Israeli kutoka Misri kwa ishara na maajabu, kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa na kwa matisho makuu.
Et vous avez tiré Israël votre peuple de la terre d’Egypte, par des signes, et par des prodiges, et par une main forte, et par un bras étendu, et par une grande terreur.
22 Uliwapa nchi hii uliyokuwa umeapa kuwapa baba zao, nchi inayotiririka maziwa na asali.
Et vous leur avez donné cette terre que vous aviez juré à leurs pères de leur donner, une terre où couleraient du lait et du miel.
23 Waliingia na kuimiliki, lakini hawakukutii wala kuifuata sheria yako. Hawakufanya kile ulichowaamuru kufanya. Hivyo ukaleta maafa haya yote juu yao.
Et ils sont entrés, et ils l’ont possédée; et ils n’ont point obéi à votre voix, et ils n’ont pas marché dans votre loi; et ils n’ont rien fait de tout ce que vous leur avez ordonné; et tous ces maux sont venus sur eux.
24 “Tazama jinsi tumezungukwa na jeshi ili kuuteka mji huu. Kwa sababu ya upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo ambao wanaushambulia. Ulilosema limetokea kama vile unavyoona sasa.
Voilà que des fortifications ont été construites contre la cité, afin de la prendre; et la ville a été livrée aux mains des Chaldéens qui combattent contre elle, au glaive, et à la famine, et à la peste, et tout ce que vous avez dit est arrivé, comme vous-même le voyez.
25 Ingawa mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo, wewe, Ee Bwana Mwenyezi, uliniambia, ‘Nunua shamba kwa fedha, na jambo hilo lishuhudiwe.’”
Et vous, Seigneur mon Dieu, vous me dites: Achète le champ avec de l’argent, et prends des témoins, quoique la ville ait été livrée aux mains des Chaldéens.
26 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
Et la parole du Seigneur fut adressée à Jérémie, disant:
27 “Mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza?
Voici que moi je suis le Seigneur, le Dieu de toute chair; est-ce qu’une chose me sera difficile?
28 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa Wakaldayo, na mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ambaye atauteka.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: Voilà que moi je livrerai cette cité aux mains des Chaldéens, et aux mains du roi de Babylone, et ils la prendront.
29 Wakaldayo ambao wanaushambulia mji huu watakuja na kuuchoma moto na kuuteketeza, pamoja na nyumba ambamo watu wamenikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba katika mapaa na kumimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine.
Elles Chaldéens viendront combattant contre cette ville, et ils y mettront le feu, et ils la brûleront, ainsi que les maisons sur les toits desquelles ils sacrifiaient à Baal et faisaient à des dieux étrangers de nombreuses libations pour m’irriter.
30 “Watu wa Israeli na wa Yuda hawakufanya kitu kingine ila uovu mbele zangu tangu ujana wao. Naam, watu wa Israeli hawakufanya kitu kingine ila kunikasirisha kwa kazi ambazo mikono yao imetengeneza, asema Bwana.
Car les fils d’Israël et les fils de Juda faisaient continuellement le mal sous mes yeux dès leur jeunesse; les fils d’Israël qui jusqu’à ce jour me révoltaient par les œuvres de leurs mains, dit le Seigneur.
31 Tangu siku ulipojengwa hadi sasa, mji huu umenikasirisha na kunighadhibisha kiasi kwamba ni lazima niuondoe machoni pangu.
Parce que cette cité est devenue pour moi un objet de fureur et d’indignation, depuis le jour qu’on l’a bâtie, jusqu’au jour où elle disparaîtra de ma présence,
32 Watu wa Israeli na wa Yuda wamenikasirisha kwa uovu wote waliofanya: wao, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao, watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu.
À cause du mal que les enfants d’Israël et les enfants de Juda ont fait, en me provoquant au courroux, eux et leurs rois, leurs princes, et leurs prêtres, et leurs prophètes, les hommes de Juda et les habitants de Jérusalem.
33 Walinigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao. Ingawa niliwafundisha tena na tena, hawakupenda kusikiliza wala kuitikia adhabu.
Et ils ont tourné vers moi le dos et non la face, lorsque je les enseignais au point du jour, et que je les instruisais, et qu’ils ne voulaient pas écouter et recevoir l’instruction.
34 Waliweka miungu yao ya kuchukiza sana katika nyumba iitwayo kwa Jina langu na kuinajisi.
Et ils ont mis leurs idoles dans la maison dans laquelle a été invoqué mon nom. afin de la souiller.
35 Wakajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu kwa ajili ya Baali katika Bonde la Ben-Hinomu, ambapo walitoa wana wao na binti zao kafara kwa Moleki, ingawa kamwe sikuamuru, wala halikuingia akilini mwangu, kwamba watafanya chukizo kama hilo na kumfanya Yuda atende dhambi.
Et ils ont bâti les hauts lieux de Baal qui sont dans la vallée du fils d’Ennom, afin de consacrer leurs fils et leurs filles à Moloch; ce que je ne leur ai pas commandé; et il n’est pas monté jusqu’à mon cœur qu’ils feraient cette abomination, et qu’ils entraîneraient Juda dans le péché.
36 “Mnasema kuhusu mji huu, ‘Kwa upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babeli,’ lakini hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo:
Et maintenant, à cause de cela, voici ce que dit le Seigneur, Dieu d’Israël, à cette cité dont vous dites, vous, qu’elle sera livrée aux mains du roi de Babylone, par le glaive, par la famine et par la peste:
37 Hakika nitawakusanya kutoka nchi zote nilizowafukuzia katika hasira yangu kali na ghadhabu yangu kuu, nitawarudisha mahali hapa na kuwaruhusu waishi kwa salama.
Voilà que moi, je les rassemblerai de toutes les terres dans lesquelles je les ai jetés dans ma fureur, et dans ma colère et dans ma grande indignation, et je les ramènerai en ce lieu, et je les y ferai habiter en assurance.
38 Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
Et ils seront mon peuple, et moi je serai leur Dieu.
39 Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili kwamba waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao.
Et je leur donnerai un seul cœur et une seule voie, afin qu’ils me craignent tous les jours de leur vie, et que bien leur soit à eux et à leurs fils après eux.
40 Nitafanya nao agano la milele: Kamwe sitaacha kuwatendea mema, nami nitawavuvia kunicha mimi, ili kamwe wasigeukie mbali nami.
Et je ferai avec eux une alliance éternelle, et je ne cesserai point de leur faire du bien; et je mettrai ma crainte dans leur cœur, afin qu’ils ne se retirent pas de moi.
41 Nitafurahia kuwatendea mema, na kwa hakika nitawapanda katika nchi hii kwa moyo wangu wote na roho yangu yote.
Et je me réjouirai en eux, lorsque je leur aurai fait du bien; et je les rétablirai en cette terre dans la vérité, de tout mon cœur, et de toute mon âme.
42 “Hili ndilo asemalo Bwana: Kama nilivyoleta maafa haya makubwa kwa watu hawa, ndivyo nitakavyowapa mafanikio niliyowaahidi.
Car voici ce que dit le Seigneur: Comme j’ai amené sur ce peuple tous ces grands maux, ainsi j’amènerai sur eux tous les biens que je leur promets.
43 Kwa mara nyingine tena mashamba yatanunuliwa katika nchi hii ambayo mlisema, ‘Imekuwa ukiwa, isiyofaa, isiyo na watu wala wanyama, kwa sababu imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.’
Elles champs auront encore des possesseurs dans cette terre de laquelle vous dites, vous, qu’elle est déserte, parce qu’il n’y est pas demeure d’homme ni de bête, et qu’elle a été livrée aux mains des Chaldéens.
44 Mashamba yatanunuliwa kwa fedha, na hati zitatiwa sahihi, zitatiwa muhuri na kushuhudiwa katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda na katika miji ya nchi ya vilima, sehemu za magharibi katika miji ya tambarare na katika Negebu, kwa sababu nitarudisha tena mafanikio yao, asema Bwana.”
Les champs seront achetés avec de l’argent, et ils seront inscrits sur la feuille, et un sceau y sera gravé, des témoins seront invoqués, dans la terre de Benjamin et aux environs de Jérusalem; dans les cités de Juda, dans les cités des montagnes, dans les cités de la plaine, et dans les cités qui sont au midi; parce que je ramènerai leurs captifs, dit le Seigneur.

< Yeremia 32 >