< Yeremia 30 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
This is the word, that was maad of the Lord to Jeremye,
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.
and seide, The Lord God of Israel seith these thingis, and spekith, Write to thee in a book, alle these wordis whiche Y spak to thee.
3 Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”
For lo! daies comen, seith the Lord, and Y schal turne the turnyng of my puple Israel and Juda, seith the Lord; and Y schal turne hem to the lond which Y yaf to the fadris of hem, and thei schulen haue it in possessioun.
4 Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:
And these ben the wordis, whiche the Lord spak to Israel, and to Juda,
5 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Vilio vya woga vinasikika: hofu kuu, wala si amani.
For the Lord seith these thingis, We herden a word of drede; inward drede is, and pees is not.
6 Ulizeni na mkaone: Je, mwanaume aweza kuzaa watoto? Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu ameweka mikono yake tumboni kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa, kila uso ukigeuka rangi kabisa?
Axe ye, and se, if a male berith child; whi therfor siy Y the hond of ech man on his leende, as of a womman trauelynge of child, and alle faces ben turned in to yelow colour?
7 Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha! Hakutakuwa na nyingine mfano wake. Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo, lakini ataokolewa kutoka hiyo.
Wo! for thilke day is greet, nether ony is lyk it; and it is a tyme of tribulacioun to Jacob, and of hym schal be sauyd.
8 “‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao na kuvipasua vifungo vyao; wageni hawatawafanya tena watumwa.
And it schal be, in that dai, seith the Lord of oostis, Y schal al to-breke the yok of hym fro thi necke, and Y schal breke hise boondis; and aliens schulen no more be lordis of it,
9 Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao na Daudi mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao.
but thei schulen serue to her Lord God, and to Dauid, her kyng, whom Y schal reyse for hem.
10 “‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli,’ asema Bwana. ‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali, wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na usalama, wala hakuna atakayemtia hofu.
Therfor, Jacob, my seruaunt, drede thou not, seith the Lord, and Israel, drede thou not; for lo! Y schal saue thee fro a fer lond, and thi seed fro the lond of the caitiftee of hem. And Jacob schal turne ayen, and schal reste, and schal flowe with alle goodis; and noon schal be whom he schal drede.
11 Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’ asema Bwana. ‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambamo miongoni mwao nimewatawanya, sitawaangamiza ninyi kabisa. Nitawaadhibu, lakini kwa haki. Sitawaacha kabisa bila adhabu.’
For Y am with thee, seith the Lord, for to saue thee. For Y schal make endyng in alle folkis, in whiche Y scateride thee; sotheli Y schal not make thee in to endyng, but Y schal chastise thee in doom, that thou be not seyn to thee to be gilteles.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.
For the Lord seith these thingis, Thi brekyng is vncurable, thi wounde is the worste.
13 Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako, hakuna dawa ya kidonda chako, wewe hutapona.
Noon is, that demeth thi doom to bynde togidere; the profit of heelyngis is not to thee.
14 Wale walioungana nawe wote wamekusahau, hawajali chochote kukuhusu wewe. Nimekupiga kama vile adui angelifanya, na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya, kwa sababu hatia yako ni kubwa mno na dhambi zako ni nyingi sana.
Alle thi louyeris han foryete thee, thei schulen not seke thee; for Y haue smyte thee with the wounde of an enemy, with cruel chastisyng; for the multitude of thi wickidnesse, thi synnes ben maad hard.
15 Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako, yale maumivu yako yasiyoponyeka? Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi nimekufanyia mambo haya.
What criest thou on thi brekynge? thi sorewe is vncurable; for the multitude of thi wickidnesse, and for thin hard synnes, Y haue do these thingis to thee.
16 “‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa; adui zako wote watakwenda uhamishoni. Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara; wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.
Therfor alle that eeten thee, schulen be deuourid, and alle thin enemyes schulen be led in to caitifte; and thei that distrien thee, schulen be distried, and Y schal yyue alle thi robberis in to raueyn.
17 Lakini nitakurudishia afya yako na kuyaponya majeraha yako,’ asema Bwana, ‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa, Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’
For Y schal heele perfitli thi wounde, and Y schal make thee hool of thi woundis, seith the Lord; for thou, Sion, thei clepeden thee cast out; this is it that hadde no sekere.
18 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo, na kuhurumia maskani yake. Mji utajengwa tena juu ya magofu yake, nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.
The Lord seith these thingis, Lo! Y schal turne the turnyng of the tabernaclis of Jacob, and Y schal haue merci on the housis of hym; and the citee schal be bildid in his hiynesse, and the temple schal be foundid bi his ordre.
19 Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao na sauti ya furaha. Nitaiongeza idadi yao wala hawatapungua, nitawapa heshima na hawatadharauliwa.
And heriyng and the vois of pleiers schal go out of hem, and Y schal multiplie hem, and thei schulen not be decreessid; and Y schal glorifie hem, and thei schulen not be maad thynne.
20 Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa siku za zamani, nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu; nitawaadhibu wale wote wawaoneao.
And the sones therof schulen be as at the bigynnyng, and the cumpeny therof schal dwelle bifore me; and Y schal visite ayens alle that doon tribulacioun to it.
21 Mmoja wao atakuwa kiongozi wao; mtawala wao atainuka miongoni mwao. Nitamleta karibu nami, naye atanikaribia mimi, kwa maana ni nani yule atakayejitolea kuwa karibu nami?’ asema Bwana.
And the duyk therof schal be of it, and a prince schal be brouyt forth of the myddis therof; and Y schal applie hym, and he schal neiye to me; for who is this, that schal applie his herte, that he neiye to me? seith the Lord.
22 ‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.’”
And ye schulen be in to a puple to me, and Y schal be in to God to you.
23 Tazama, tufani ya Bwana italipuka kwa ghadhabu, upepo wa kisulisuli uendao kasi utashuka juu ya vichwa vya waovu.
Lo! the whirlewynd of the Lord, a strong veniaunce goynge out, a tempest fallynge doun, schal reste in the heed of wickid men.
24 Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake. Siku zijazo mtayaelewa haya.
The Lord schal not turne awey the ire of indignacioun, til he do, and fille the thouyt of his herte; in the laste of daies ye schulen vndurstonde tho thingis.

< Yeremia 30 >