< Yeremia 30 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
Yahweh gave me another message. He said,
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.
“[I], Yahweh, the God whom the Israeli people [say they belong to], am telling you that you should write down everything that I have said to you.
3 Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”
[I want you to know that] some day I will free my people, [the people of] Israel and Judah, from being slaves [in Babylon]. I will bring them back to this land that I gave to their ancestors, and this land will belong to them again. [That will surely happen because] I, Yahweh, have said it.”
4 Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:
Yahweh gave [to me] another message concerning [the people of] Israel and Judah.
5 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Vilio vya woga vinasikika: hofu kuu, wala si amani.
This is what he said: “I hear people screaming because they are terrified [DOU]; there is no peace [in the land].
6 Ulizeni na mkaone: Je, mwanaume aweza kuzaa watoto? Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu ameweka mikono yake tumboni kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa, kila uso ukigeuka rangi kabisa?
But think about this: Men certainly do not [RHQ] give birth to babies. Therefore, why do strong men stand there, with their faces very white/pale, with their hands pressed against their stomachs, like women who are about to give birth to babies?
7 Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha! Hakutakuwa na nyingine mfano wake. Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo, lakini ataokolewa kutoka hiyo.
[Terrible things will soon happen]; that will be a terrible day! There has never been such a time. It will be a time when [my] Israeli people will experience great trouble, but [finally] they will be saved [from their sufferings].”
8 “‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao na kuvipasua vifungo vyao; wageni hawatawafanya tena watumwa.
The Commander of the armies of angels says this: “At that time [it will be as though] I will sever/cut the ropes [that are around my people], and I will free them from being (slaves/forced to do what the King of Babylon wants them to do) [MET]. People in other countries will no longer be their bosses.
9 Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao na Daudi mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao.
My people will [again] serve me, Yahweh, their God, and [they will serve a king who is a descendant of] King David; [they will serve the king] whom I will appoint for them.
10 “‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli,’ asema Bwana. ‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali, wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na usalama, wala hakuna atakayemtia hofu.
So, [you people of] Israel who serve me, do not be dismayed/worried [now], because [some day] I will bring you back from distant places; I will bring your descendants [back home] from the land to which they were exiled. [Then you] Israeli people will [again] live peacefully and safely, and there will not be any [nation] that will cause you to be terrified.
11 Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’ asema Bwana. ‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambamo miongoni mwao nimewatawanya, sitawaangamiza ninyi kabisa. Nitawaadhibu, lakini kwa haki. Sitawaacha kabisa bila adhabu.’
I, Yahweh, say that I will be with you and will rescue you; I will completely destroy the nations to which I have scattered you. But I will not completely destroy you. I will punish you [for your many sins], but I will punish you [only] as severely as you deserve: I would be doing wrong if I did not punish you at all.”
12 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.
Yahweh [also] says this: “[You have (suffered very much/endured many disasters)]; [it is as though] you have a terrible wound that cannot be cured.
13 Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako, hakuna dawa ya kidonda chako, wewe hutapona.
There is no one to help you, no one to put a bandage on your wound. There is no [medicine that will] heal you.
14 Wale walioungana nawe wote wamekusahau, hawajali chochote kukuhusu wewe. Nimekupiga kama vile adui angelifanya, na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya, kwa sababu hatia yako ni kubwa mno na dhambi zako ni nyingi sana.
All your allies [MET] have deserted you and they do not want to help you [any more]. [It is true that] I have punished you severely, [like your] enemies would wound you, because you have committed many sins and you are very guilty.
15 Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako, yale maumivu yako yasiyoponyeka? Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi nimekufanyia mambo haya.
[Because that is true], why do you protest about my punishing you, [as though I had caused] a wound that could not be cured [RHQ]? It was necessary for me to punish you, because you had committed many sins and you were very guilty.
16 “‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa; adui zako wote watakwenda uhamishoni. Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara; wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.
But [some day] all those who [are trying to] destroy you will be destroyed; all your enemies will be exiled [to other nations]. All those who have stolen things from you will have their [valuable] possessions stolen, and all those who attack you will be attacked.
17 Lakini nitakurudishia afya yako na kuyaponya majeraha yako,’ asema Bwana, ‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa, Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’
[Everyone] says that you are (outcasts/people that they no longer associate with), and that [you live in] Jerusalem, a city that no one cares about.” But Yahweh says, “I will heal your injuries/wounds and cause you to be healthy again.”
18 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo, na kuhurumia maskani yake. Mji utajengwa tena juu ya magofu yake, nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.
This is what Yahweh says: “I will bring the people of Israel back from the lands to which they were taken and enable them to possess their land and their houses again. [When that happens], Jerusalem will be rebuilt on top of its ruins, and the [king’s] palace will be rebuilt to be like it was before.
19 Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao na sauti ya furaha. Nitaiongeza idadi yao wala hawatapungua, nitawapa heshima na hawatadharauliwa.
People will [again] sing joyfully to thank [me], and I will cause there to be more people [in Jerusalem], not fewer; I will cause them to be honored, not despised.
20 Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa siku za zamani, nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu; nitawaadhibu wale wote wawaoneao.
Their children will [prosper] like they did before. I will cause them to be a group of people [who worship] me, and I will punish any [nation] that oppresses them.
21 Mmoja wao atakuwa kiongozi wao; mtawala wao atainuka miongoni mwao. Nitamleta karibu nami, naye atanikaribia mimi, kwa maana ni nani yule atakayejitolea kuwa karibu nami?’ asema Bwana.
One of their own people will be their king, and I will invite him to come close to me [to worship me], because no one [RHQ] would (dare/have courage) to come close to me [if I did not invite him].
22 ‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.’”
You [Israeli people] will be my people, and I will be your God.”
23 Tazama, tufani ya Bwana italipuka kwa ghadhabu, upepo wa kisulisuli uendao kasi utashuka juu ya vichwa vya waovu.
Yahweh will punish [MTY] [your enemies]; [it will be like a great] storm; it will come down [like] a whirlwind, swirling around the heads of wicked people.
24 Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake. Siku zijazo mtayaelewa haya.
He will not stop being angry until he completely accomplishes [all] that he has planned. In the future, you will understand [all] of this [clearly].

< Yeremia 30 >