< Yeremia 30 >

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
The word which came to Jeremiah from Jehovah, saying: —
2 “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.
Thus saith Jehovah, the God of Israel: Write thee all the words which I have spoken to thee in a book.
3 Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”
For behold the days come, saith Jehovah, when I will bring back the captives of my people Israel and Judah, saith Jehovah, and cause them to return to the land which I gave to their fathers, and they shall possess it.
4 Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:
And these are the words which Jehovah spake concerning Israel and concerning Judah.
5 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Vilio vya woga vinasikika: hofu kuu, wala si amani.
Behold, thus saith Jehovah: The voice of trembling do we hear; There is alarm, and no peace.
6 Ulizeni na mkaone: Je, mwanaume aweza kuzaa watoto? Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu ameweka mikono yake tumboni kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa, kila uso ukigeuka rangi kabisa?
Ask ye now and see, Whether a male doth bring forth? Why then do I see every man's hands upon his loins, like a woman in travail? And why are all faces turned into paleness?
7 Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha! Hakutakuwa na nyingine mfano wake. Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo, lakini ataokolewa kutoka hiyo.
Alas! that day is great, So that there is none like it; It is a time of trouble for Jacob, Yet shall he be saved from it.
8 “‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao na kuvipasua vifungo vyao; wageni hawatawafanya tena watumwa.
For in that day, saith Jehovah of hosts, I will break his yoke from his neck, And his bands will I burst asunder, And he shall be subject to strangers no more.
9 Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao na Daudi mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao.
But they shall serve Jehovah, their God, And David, their king, whom I will raise up for them.
10 “‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli,’ asema Bwana. ‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali, wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na usalama, wala hakuna atakayemtia hofu.
Therefore fear thou not, O my servant Jacob, saith Jehovah, And be not thou dismayed, O Israel! For, behold, I will bring thee safe from afar, And thy posterity from the land of their captivity; And Jacob shall return, and be at rest; Yea, he shall be quiet, and none shall make him afraid.
11 Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’ asema Bwana. ‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambamo miongoni mwao nimewatawanya, sitawaangamiza ninyi kabisa. Nitawaadhibu, lakini kwa haki. Sitawaacha kabisa bila adhabu.’
For I will be with thee, saith Jehovah, to save thee; When I shall make a full end of all the nations Whither I have dispersed thee, Yet will I not make a full end of thee; I will correct thee in measure, Yet must I not leave thee wholly unpunished.
12 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.
For thus saith Jehovah: Thy bruise is incurable; Thy wound is mortal.
13 Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako, hakuna dawa ya kidonda chako, wewe hutapona.
No one offereth his help for thy cure; No healing medicines are applied to thee.
14 Wale walioungana nawe wote wamekusahau, hawajali chochote kukuhusu wewe. Nimekupiga kama vile adui angelifanya, na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya, kwa sababu hatia yako ni kubwa mno na dhambi zako ni nyingi sana.
All thy lovers have forgotten thee; They inquire not after thee. For with the wound of an enemy have I smitten thee, With the chastisement of a cruel one, For the multitude of thine iniquities, Because thy sins were increased.
15 Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako, yale maumivu yako yasiyoponyeka? Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi nimekufanyia mambo haya.
Why criest thou because of thy bruise? Thy pain is without remedy. For the multitude of thine iniquities, Because thy sins were increased, Have I done these things to thee.
16 “‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa; adui zako wote watakwenda uhamishoni. Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara; wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.
Yet all they that devour thee shall be devoured, And all thine enemies, yea, all of them, shall go into captivity, And they that spoil thee shall become a spoil, And all that plunder thee will I give up to plunder.
17 Lakini nitakurudishia afya yako na kuyaponya majeraha yako,’ asema Bwana, ‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa, Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’
For I will restore soundness to thee, And I will heal thee of thy wounds, saith Jehovah; For they have called thee the outcast, Zion, whom no man careth for.
18 “Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo, na kuhurumia maskani yake. Mji utajengwa tena juu ya magofu yake, nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.
Thus saith Jehovah: Behold, I will bring back the captives of the tents of Jacob, And I will have pity upon his dwelling-places, And the city shall be builded upon her heap, And the palace shall be inhabited as of old.
19 Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao na sauti ya furaha. Nitaiongeza idadi yao wala hawatapungua, nitawapa heshima na hawatadharauliwa.
And out of them shall go forth thanksgiving, And the voice of them that make merry. And I will multiply them, and they shall not be few, And I will exalt them, and they shall not be low.
20 Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa siku za zamani, nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu; nitawaadhibu wale wote wawaoneao.
And their children shall be as aforetime, And their congregation shall be established before me, And I will punish all that oppress them.
21 Mmoja wao atakuwa kiongozi wao; mtawala wao atainuka miongoni mwao. Nitamleta karibu nami, naye atanikaribia mimi, kwa maana ni nani yule atakayejitolea kuwa karibu nami?’ asema Bwana.
And their princes shall be of themselves, And their governor shall proceed from the midst of them. And I will cause them to approach, and they shall come near to me; For who is he that would dare to come near to me? saith Jehovah.
22 ‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.’”
And ye shall be my people, And I will be your God.
23 Tazama, tufani ya Bwana italipuka kwa ghadhabu, upepo wa kisulisuli uendao kasi utashuka juu ya vichwa vya waovu.
Behold, a whirlwind from Jehovah, Furious doth it go forth, Even a sweeping whirlwind; Upon the head of the wicked shall it rush.
24 Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake. Siku zijazo mtayaelewa haya.
The fierce anger of Jehovah shall not turn back Until he shall have executed, until he shall have accomplished, the purpose of his heart; In a future day ye shall understand it fully.

< Yeremia 30 >