< Yeremia 3 >

1 “Kama mtu akimpa talaka mkewe, naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine, je, huyo mume aweza kumrudia tena? Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa? Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi: je, sasa utanirudia tena?” asema Bwana.
Pravijo: »Če človek odpusti svojo ženo in gre ona od njega in postane od nekega drugega moškega, ali se bo on ponovno vrnil k njej? Ali ne bi bila ta dežela silno oskrunjena? Ti pa si igrala pocestnico z mnogimi ljubimci; vendar se ponovno vrni k meni, « govori Gospod.
2 “Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone. Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe? Uliketi kando ya barabara ukiwasubiri wapenzi, ukakaa kama yeye ahamahamaye jangwani. Umeinajisi nchi kwa ukahaba wako na uovu wako.
»Povzdigni svoje oči k visokim krajem in poglej, kje vse nisi bila poležena z [njimi]. Na poteh si sedela zanje, kakor Arabec v divjini in deželo si oskrunila s svojimi vlačugarstvi in svojo zlobnostjo.
3 Kwa hiyo mvua imezuiliwa, nazo mvua za vuli hazikunyesha. Hata hivyo, una uso usio na haya kama wa kahaba; unakataa kutahayari kwa aibu.
Zato so bili nalivi zadržani in ni bilo poznega dežja; in ti imaš vlačugino čelo; odklonila si, da bi bila osramočena.
4 Je, wewe hujaniita hivi punde tu: ‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,
Mar ne boš od tega časa klicala k meni: ›Moj oče, ti si vodič od moje mladosti?‹«
5 je, utakasirika siku zote? Je, ghadhabu yako itaendelea milele?’ Hivi ndivyo unavyozungumza, lakini unafanya maovu yote uwezayo.”
Ali bo svojo jezo hranil na veke? Ali jo bo držal do konca? Glej, govoril si in storil hude stvari, kot ti lahko.
6 Wakati wa utawala wa Mfalme Yosia, Bwana aliniambia, “Umeona kile Israeli asiye mwaminifu amekifanya? Amepanda juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti uliotanda na amefanya uzinzi huko.
Gospod mi je tudi rekel v dneh kralja Jošíja: »Ali si videl to, kar je storila odpadnica Izrael? Odhajala je na vsako visoko goro in pod vsako zeleno drevo in tam igrala pocestnico.
7 Mimi nilifikiri kuwa baada ya kuyafanya yote haya angelinirudia, lakini hakurudi, naye dada yake Yuda mdanganyifu aliona hili.
Potem ko je storila vse te stvari, sem rekel: ›Obrni se k meni.‹ Toda ni se vrnila. In njena verolomna sestra Juda je to videla.
8 Nilimpa Israeli asiye mwaminifu hati yake ya talaka, na kumfukuza kwa ajili ya uzinzi wake wote. Hata hivyo nikaona kuwa Yuda dada yake mdanganyifu hakuogopa. Yeye pia alitoka na kufanya uzinzi.
Videl sem, ko sem jo zaradi vseh vzrokov, s čimer je odpadnica Izrael zagrešila zakonolomstvo, odslovil in ji dal ločitveni list, se njena verolomna sestra Juda kljub temu ni bala, temveč je tudi ona odšla in prav tako igrala pocestnico.
9 Kwa sababu uasherati wa Israeli haukuwa kitu kwake, Yuda aliinajisi nchi kwa kuzini na mawe na miti.
Pripetilo se je skozi lahkomiselnost njenega vlačugarstva, da je omadeževala deželo in zagrešila zakonolomstvo s skalami in z lesom.
10 Pamoja na hayo yote, Yuda dada yake mdanganyifu hakunirudia kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,” asema Bwana.
Vendar se zaradi vsega tega njena verolomna sestra Juda ni obrnila k meni z vsem svojim srcem, temveč hlinjeno, « govori Gospod.
11 Bwana akaniambia, “Israeli asiye mwaminifu ana haki kuliko Yuda mdanganyifu.
Gospod mi je rekel: »Odpadnica Izrael se je bolj opravičila kakor verolomna Juda.
12 Nenda, ukatangaze ujumbe huu kuelekea kaskazini: “‘Rudi, Israeli usiye mwaminifu,’ asema Bwana, ‘sitakutazama tena kwa uso uliokunjamana, kwa kuwa mimi ni mwenye huruma,’ asema Bwana, ‘Sitashika hasira yangu milele.
Pojdi in razglasi te besede proti severu in reci: ›Vrni se, ti odpadnica Izrael, ‹ govori Gospod › in svoji jezi ne bom povzročil, da pade na vas, kajti jaz sem usmiljen, ‹ govori Gospod, › in jeze ne bom držal na veke.
13 Ungama dhambi zako tu: kwamba umemwasi Bwana Mungu wako, umetapanya wema wako kwa miungu ya kigeni chini ya kila mti unaotanda, nawe hukunitii mimi,’” asema Bwana.
Samo priznaj svojo krivičnost, da si se pregrešila zoper Gospoda, svojega Boga in si svoje poti razkropila k tujcem pod vsakim zelenim drevesom in nisi ubogala mojega glasu, ‹ govori Gospod.
14 “Rudini, enyi watu msio waaminifu, kwa kuwa mimi ni mume wenu,” asema Bwana. “Nitawachagua ninyi, mmoja kutoka kwenye mji, na wawili kutoka kwenye ukoo, nami nitawaleta Sayuni.
›Obrnite se, odpadli otroci, ‹ govori Gospod. ›Kajti jaz sem poročen z vami. Vzel vas bom enega iz mesta in dva iz družine in vas privedel k Sionu.
15 Kisha nitawapeni wachungaji wanipendezao moyo wangu, ambao watawaongoza kwa maarifa na ufahamu.
Dal vam bom pastirje po svojem srcu, ki vas bodo hranili z znanjem in razumevanjem.
16 Katika siku hizo, idadi yenu itakapokuwa imeongezeka sana katika nchi, watu hawatasema tena, ‘Sanduku la Agano la Bwana,’” asema Bwana. “Halitaingia tena kwenye mawazo yao wala kukumbukwa, hawatalihitaji wala halitatengenezwa jingine.
Zgodilo se bo, ko boste pomnoženi in povečani v deželi, v tistih dneh, ‹ govori Gospod, ›ne bodo več rekli: ›Skrinja Gospodove zaveze.‹ Niti to ne bo prišlo na misel, niti se tega ne bodo spomnili, niti je ne bodo obiskali, niti to ne bo več storjeno.
17 Wakati huo, wataita Yerusalemu kuwa Kiti cha Enzi cha Bwana, nayo mataifa yote watakusanyika Yerusalemu kuliheshimu jina la Bwana. Hawatafuata tena ukaidi wa mioyo yao miovu.
Ob tistem času bodo [prestolnico] Jeruzalem imenovali Gospodov prestol. Vsi narodi bodo zbrani k njej, k imenu Gospoda, k [prestolnici] Jeruzalem. Niti ne bodo več hodili po zamisli svojih zlih src.
18 Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itaungana na nyumba ya Israeli, wao kwa pamoja watakuja kutoka nchi ya kaskazini hadi nchi niliyowapa baba zenu kama urithi.
V tistih dneh bo Judova hiša hodila z Izraelovo hišo in skupaj bodo prišli iz severne dežele k deželi, ki sem jo dal v dediščino vašim očetom.
19 “Mimi mwenyewe nilisema, “‘Tazama jinsi nitakavyowatunza kwa furaha kama wana na kuwapa nchi nzuri, urithi ulio mzuri kuliko wa taifa jingine lolote.’ Nilidhani mngeniita ‘Baba,’ na msingegeuka, mkaacha kunifuata.
Toda rekel sem: ›Kako te bom postavil med otroke in ti dal prijetno deželo, čedno dediščino vojske narodov?‹ Rekel sem: ›Klicala me boš: ›Moj oče‹ in ne boš se odvrnila od mene.‹
20 Lakini kama mwanamke asiye mwaminifu kwa mumewe, vivyo hivyo mmekosa uaminifu kwangu pia, ee nyumba ya Israeli,” asema Bwana.
Zagotovo, kakor žena zahrbtno odide od svojega soproga, tako ste zahrbtno ravnali z menoj, oh hiša Izraelova, ‹ govori Gospod
21 Kilio kinasikika juu ya miinuko iliyo kame, kulia na kuomboleza kwa watu wa Israeli, kwa sababu wamepotoka katika njia zao na wamemsahau Bwana Mungu wao.
›Glas je bil slišan na visokih krajih, jokanje in ponižne prošnje Izraelovih otrok, kajti izkrivili so svojo pot in pozabili Gospoda, svojega Boga.
22 “Rudini, enyi watu msio waaminifu, nami nitawaponya ukengeufu wenu.” “Naam, tutakuja kwako, kwa maana wewe ni Bwana Mungu wetu.
Vrnite se, vi odpadli otroci in ozdravil bom vaša odvračanja.‹« »Glej, mi prihajamo k tebi, kajti ti si Gospod, naš Bog.
23 Hakika zile ghasia za kuabudu sanamu kwenye vilima na milimani ni udanganyifu; hakika katika Bwana, Mungu wetu, uko wokovu wa Israeli.
Resnično, zaman je upati na rešitev duše s hribov in od množice gora. Zares, v Gospodu, našem Bogu, je Izraelova rešitev duš.
24 Tangu ujana wetu miungu ya aibu imeyala matunda ya kazi za baba zetu: makundi yao ya kondoo na ngʼombe, wana wao na binti zao.
Kajti sramota je od naše mladosti požrla trud naših očetov; njihove trope in njihove črede, njihove sinove in njihove hčere.
25 Sisi na tulale chini katika aibu yetu, na fedheha yetu itufunike. Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wetu, sisi na mababa zetu; tangu ujana wetu hadi leo hatukumtii Bwana Mungu wetu.”
Uležemo se v svoji sramoti in naša zmešnjava nas pokriva, kajti grešili smo zoper Gospoda, svojega Boga, mi in naši očetje, od svoje mladosti, celo do današnjega dne in nismo ubogali glasu Gospoda, svojega Boga.«

< Yeremia 3 >