< Yeremia 3 >
1 “Kama mtu akimpa talaka mkewe, naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine, je, huyo mume aweza kumrudia tena? Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa? Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi: je, sasa utanirudia tena?” asema Bwana.
He hath said, If a man send away his wife, and she go from him and become another man’s, will he return unto her, again? would not that land be, utterly defiled? And, thou, hast been unchaste with many neighbours, and yet [thinkest] to return unto me! Declareth Yahweh.
2 “Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone. Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe? Uliketi kando ya barabara ukiwasubiri wapenzi, ukakaa kama yeye ahamahamaye jangwani. Umeinajisi nchi kwa ukahaba wako na uovu wako.
Lift up thine eyes unto the bare heights and see—where thou hast not been unchastely embraced! beside the ways, hast thou sat to them, like the Arabian in the desert, —and hast defiled the land with thine unchastities, and with thy wickedness.
3 Kwa hiyo mvua imezuiliwa, nazo mvua za vuli hazikunyesha. Hata hivyo, una uso usio na haya kama wa kahaba; unakataa kutahayari kwa aibu.
Therefore have been withholden the showers, And, the latter rain, hath not come, —Yet the forehead of an unchaste woman, hast thou, Thou hast refused to be ashamed.
4 Je, wewe hujaniita hivi punde tu: ‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,
Hast thou not from this time, cried unto me, My father! the friend of my youth, art, thou?
5 je, utakasirika siku zote? Je, ghadhabu yako itaendelea milele?’ Hivi ndivyo unavyozungumza, lakini unafanya maovu yote uwezayo.”
Will he maintain his anger to times age-abiding? Will he keep it perpetually? Lo! thou hast spoken thus but hast done wicked things and had thy way!
6 Wakati wa utawala wa Mfalme Yosia, Bwana aliniambia, “Umeona kile Israeli asiye mwaminifu amekifanya? Amepanda juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti uliotanda na amefanya uzinzi huko.
And Yahweh said unto me, in the days of Josiah the king, Hast thou seen what apostate Israel, did? She used to go upon every high mountain and beneath every green tree, and commit unchastity there.
7 Mimi nilifikiri kuwa baada ya kuyafanya yote haya angelinirudia, lakini hakurudi, naye dada yake Yuda mdanganyifu aliona hili.
And I said, after she had been doing all these things, Unto me, shall thou return? and she returned not, —and her treacherous sister Judah saw it!
8 Nilimpa Israeli asiye mwaminifu hati yake ya talaka, na kumfukuza kwa ajili ya uzinzi wake wote. Hata hivyo nikaona kuwa Yuda dada yake mdanganyifu hakuogopa. Yeye pia alitoka na kufanya uzinzi.
Though she saw that for all this, apostate Israel having committed adultery, I had sent her away, and had given a scroll of divorcement unto her, yet her treacherous sister Judah feared not, but, she also, went and committed unchastity.
9 Kwa sababu uasherati wa Israeli haukuwa kitu kwake, Yuda aliinajisi nchi kwa kuzini na mawe na miti.
Yea though it had come to pass that through the levity of her unchastity, she had defiled the land, —and committed adultery with Stone and with Tree,
10 Pamoja na hayo yote, Yuda dada yake mdanganyifu hakunirudia kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,” asema Bwana.
yet, in spite of all this, her treacherous sister Judah returned not unto me, with all her heart, —but, falsely, Declareth Yahweh.
11 Bwana akaniambia, “Israeli asiye mwaminifu ana haki kuliko Yuda mdanganyifu.
Then said Yahweh unto me, —Apostate Israel, hath justified herself, —more than treacherous Judah.
12 Nenda, ukatangaze ujumbe huu kuelekea kaskazini: “‘Rudi, Israeli usiye mwaminifu,’ asema Bwana, ‘sitakutazama tena kwa uso uliokunjamana, kwa kuwa mimi ni mwenye huruma,’ asema Bwana, ‘Sitashika hasira yangu milele.
Go, and proclaim these words, towards the North and say—Return! thou apostate—Israel, Urgeth Yahweh, I will not lower my face against you, —for full of lovingkindness, I am, Declareth Yahweh, I will not maintain [mine anger] unto times age-abiding.
13 Ungama dhambi zako tu: kwamba umemwasi Bwana Mungu wako, umetapanya wema wako kwa miungu ya kigeni chini ya kila mti unaotanda, nawe hukunitii mimi,’” asema Bwana.
Only, acknowledge thine iniquity, that against Yahweh thy God, hast thou transgressed, —and hast gone hither and thither unto foreigners under every green tree, and unto my voice, ye have not hearkened Declareth Yahweh.
14 “Rudini, enyi watu msio waaminifu, kwa kuwa mimi ni mume wenu,” asema Bwana. “Nitawachagua ninyi, mmoja kutoka kwenye mji, na wawili kutoka kwenye ukoo, nami nitawaleta Sayuni.
Return, ye apostate sons, Urgeth Yahweh, for, I, am become your husband, —therefore will I take you one of a city, and two of a family, and will bring you to Zion;
15 Kisha nitawapeni wachungaji wanipendezao moyo wangu, ambao watawaongoza kwa maarifa na ufahamu.
and will give you shepherds according to mine own heart, —who will feed you with knowledge and discretion.
16 Katika siku hizo, idadi yenu itakapokuwa imeongezeka sana katika nchi, watu hawatasema tena, ‘Sanduku la Agano la Bwana,’” asema Bwana. “Halitaingia tena kwenye mawazo yao wala kukumbukwa, hawatalihitaji wala halitatengenezwa jingine.
And it shall come to pass when ye shall be multiplied and become fruitful in the land, in those days, Declareth Yahweh, They shall say no more, The ark of the covenant of Yahweh, Neither shall it come up on the heart, Neither shall they remember it, Neither shall they miss it, Neither shall it be made any more.
17 Wakati huo, wataita Yerusalemu kuwa Kiti cha Enzi cha Bwana, nayo mataifa yote watakusanyika Yerusalemu kuliheshimu jina la Bwana. Hawatafuata tena ukaidi wa mioyo yao miovu.
At that time, shall they call Jerusalem, The throne of Yahweh, and there shall be gathered unto her all the nations—to the Name of Yahweh, to Jerusalem; and they shall walk no more after the stubbornness of their own wicked heart.
18 Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itaungana na nyumba ya Israeli, wao kwa pamoja watakuja kutoka nchi ya kaskazini hadi nchi niliyowapa baba zenu kama urithi.
In those days, shall the house of Judah go unto the house of Israel, —that they may enter together out of the land of the North, upon the land which I gave as an inheritance unto your fathers.
19 “Mimi mwenyewe nilisema, “‘Tazama jinsi nitakavyowatunza kwa furaha kama wana na kuwapa nchi nzuri, urithi ulio mzuri kuliko wa taifa jingine lolote.’ Nilidhani mngeniita ‘Baba,’ na msingegeuka, mkaacha kunifuata.
Though, I myself, had said, —How can I put thee among the sons, And give thee a land to be coveted, An inheritance of beauty, of the hosts of nations? Yet I said, My father, shalt thou call me, And away from me, shalt thou not turn.
20 Lakini kama mwanamke asiye mwaminifu kwa mumewe, vivyo hivyo mmekosa uaminifu kwangu pia, ee nyumba ya Israeli,” asema Bwana.
But indeed [as] a wife goeth treacherously from her husband, so, have ye acted treacherously with me, O house of Israel, Declareth Yahweh.
21 Kilio kinasikika juu ya miinuko iliyo kame, kulia na kuomboleza kwa watu wa Israeli, kwa sababu wamepotoka katika njia zao na wamemsahau Bwana Mungu wao.
A voice on the bare heights, is heard, The weeping of the supplications of the sons of Israel, —Because they have perverted their way, Have forgotten Yahweh their God.
22 “Rudini, enyi watu msio waaminifu, nami nitawaponya ukengeufu wenu.” “Naam, tutakuja kwako, kwa maana wewe ni Bwana Mungu wetu.
Return ye apostate sons, I will heal your apostasies! Behold us! we have come unto thee, For thou, art Yahweh our God.
23 Hakika zile ghasia za kuabudu sanamu kwenye vilima na milimani ni udanganyifu; hakika katika Bwana, Mungu wetu, uko wokovu wa Israeli.
Surely, to falsehood, pertain the hills The noisy throng on the mountains, —Surely, in Yahweh our God, is the salvation of Israel!
24 Tangu ujana wetu miungu ya aibu imeyala matunda ya kazi za baba zetu: makundi yao ya kondoo na ngʼombe, wana wao na binti zao.
But, the Shameful thing, hath devoured the labour of our fathers from our youth: Their flocks, and their herds, their sons and their daughters.
25 Sisi na tulale chini katika aibu yetu, na fedheha yetu itufunike. Tumetenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wetu, sisi na mababa zetu; tangu ujana wetu hadi leo hatukumtii Bwana Mungu wetu.”
We must lie down in our shame And our reproach, be our covering, For, against Yahweh our God, have we sinned, We and our fathers, from our youth even until this day, —Neither have we hearkened unto the voice of Yahweh our God.